Kwa hili la vita dhidi ya ukabila, jameni tuwaige Watanzania

Mimi simtetei Jommo Kenyatta, tena ukinichunguza sana huwa napenda mambo yawekwe bayana ili kama taifa tujue wapi tulianza kunyeshewa na mvua, huwa ninadiriki kufuata historia nje ya mambo tuliyoaminishwa kwenye vitabu tangu enzi zile. Wewe hapo ndiye mwenye matatizo kwamba hutaki mawazo nje ya kile mwalimu wa shule alikufundisha, maana nimekupeleka kwenye blog ya Mtanzania ambaye ameandika kwa kina mambo mengi kuihusu nchi yako, wewe umeingia uvivu wa kusoma na kuona heri unin'gan'ganizie badala ya kupangua hoja za huyo Mtanzania.
Kwa jinsi watanzania karibu wote humu JF wanavyopinga hoja yako, ni dalili tosha kwamba yale yote niliyokueleza kuhusu ukabila Tanzania na jinsi Nyerere alivyoufutilia mbali ni sahihi, sasa kwa kukusaidia zaidi, ukitaka kuifahamu Tanzania vizuri sana, jaribu kujiuliza maswali yafuatayo
1)Tanzania, kama zilivyo nchi zengine zote za ukanda huu, ukabila ulikuwepo hata kabla ya kuja kw wakoloni, je nani aliwaunganisha watanzania na kumaliza ukabila?, waarabu, mjerumani, waingereza, Nyerere, au wananchi wenyewe tu walijikuta wanakuwa kitu kimoja automatically?
2)Kiswahili kilizaliwa katika pwani ya Afrika mashariki, je ilikuwaje kiswahili kienee na kupenya kwa kasi huku Tanzania lakini kisiweze kupenya huko Kenya, ni nani hasa aliyekieneza Tanzania na asifanye hivyo huko Kenya, au Mungu anaipendelea zaidi Tanzania kuliko Kenya kwa kueneza kiswahili Tanzania ambayo ilikuwa ni silaha muhimu kufuta ukabila?
3)Kama hoja yako ya kwamba mkoloni hasa wa uingereza hakuona umuhimu wa kutugawa, lakini kumbuka alitukuta tumeshagawanyika kutokea enzi za mababu zetu, je nani alituunganisha kama muingereza hakuona umuhimu wa kutugawa zaidi?
4)Kwanini Rwanda na Burundi ambao pia waliwekwa chini ya uangalizi wa Belgium, ambaye hakuona sababu ya kuwagawa kama Tanzania, kwanini wanaendelea na ukabila wao uleule wa kabla ya kuja kwa wakoloni?
 
Nayaheshimu maoni yako, lakini nimekutana na Watanzania wazee walioishi miaka hiyo ya Nyerere na ambao husema kwamba wakati anatokea Butiama, tayari Watanganyika walikua wamoja. Hawakatai kwamba hakuwa wa msaada kwenye kupigana na ukabila, na alichangia pakubwa, lakini alikuta tayari watu wanaishi kwa ushirikiano.

Mgawanyiko na vurugu za baina ya makabila ni jambo la zamani sana kwenye Afrika yetu hii, lakini mimi naongea kuhusu mambo ya hapo kabla na baada ya uhuru. Inawezekana siijui sana historia ya Tanzania, lakini kuna baadhi ya Watanzania ambao hudiriki kuandika mambo mengi kinyume na jinsi wengi wenu huwa mumeamini au kutaka kuaminisha, hebu soma hapa Nyerere Hakuendeleza Kiswahili, Bali Magufuli Ndiye Anakiendeleza Kiswahili..!!!!
Leo nimepata muda na kuisoma kwa undani hii habari, kwanza nianze kwa kusema kwamba, MK254 wewe ninahisi unao uwezo mkubwa wa kuweza kusoma habari na ukaichakata na kujua huyo muhandisi ni mtu wa aina gani, sitegemei habari kama hii unaweza kuitumia kama habari rejea kwako ili kuipa nguvu hoja yako, you are much better than this guy.

Inaonekana huyu jamaa huko Europe alikoishi wazungu walimnyanyasa sana kiasi cha kujenga chuki iliyopitiliza kwa wazungu, pia amekuwa ni mtu mwenye kutoa lawama hovyo siziso na references zozote zile zaidi ya kusema mambo aliyoyasikia tu, hayo yote ya kwamba Afrika ndiyo watu wa mwanzo duniani kuwa na vyuo vikuu, kufanya operesheni ya uzazi, kutengeneza mashua, kuanza kuhesabu, ni maneno tu aliyoambiwa na watu hana ushahidi wowote ule, nimeshangazwa sana na wewe kutumia habari hii kama reference yako, unajidhalilsha sana, labda nizungumzie kuhusu hili la kwamba watanganyika walifuta ukabila na Kiswahili kilienezwa na train enzi za mjerumani,
1)Kenya ndiyo iliyoanza kujenga reli toka Mombasa kuelekea Nairobi hadi Uganda, kwanini Kiswahili kisienee Kenya hadi Uganda kama train ndiyo iliyokuwa sababu ya kueneza kiswahili?
3)Kwanini mjerumani awaunganishe watanzania pekee lakini ashindwe kuwaunganisha Rwanda na Burundi kwa kuwa wote walikuwa chini ya koloni la mjerumani ikijulikana kama The Germany east africa?

Ninarudia kusema, I hope you are better tha this man, don't downgrade your self please
 
Umeongea vyema....Raisi wetu hufanya mambo kwa sababu zinazoeleweka japo Mara kadhaa pia mambo hufanyika na tusielewe kwanini...
Kimara walikua na mpango wa kupanua barabara hadi chalinze Ni jambo lililokuepo japo limechelewa kutokana n.a. kutokua na fedha...kwahyo ndio wamelifanya sasa japo limeleta vilio sana kwa walioathirika japo kuna baadhi walishalipwa fedha za fidia. ..

Kuna nyumba 17000 zilikua zivunjwe bonde la mto msimbazi na aliagiza zisivunjwe kwahyo ilo lililotokea uko kwao nadhani linafanana na la msimbazi...

Ukabila uku kwetu hauna nafasi japo yapo makabila ambayo hua ni kama yanaangaliwa sana kutokana na kujipenyeza katika kila idara Yaani yamekua chachu kwa makabila mengine...
Kwani wewe ni wa kabila gani? Tunamjua kama mtanzania tu. Kwani tunatambika. 35% ya watu wa TANZANIA tumeona makabila tofauti. Na karibu makabila yatapoteza lugha zao. Watoto awajui tena lugha zao
 
Umeeleweka ila nina wasiwasi sana maana lugha yako kiswahili chako na uandishi wako hauoneshi hata chembe ya ukenya inaonesha ww kijana wa mjini tu hapa Tz.
 
Tatizo kubwa huwa nakua nalo kwa Watanzania, hampendi kusoma, yaani unakurupuka kujibu hoja bila kusoma. Mimi nimekuletea hiyo blog nikitegemea utasoma hadi mwisho, wewe umesoma paragraph moja ukakimbilia kujibu.
Tumia muda wako uisome yote, baada ya hapo ujibu kwa hoja ili kupangua hoja za huyo mwandishi.

tupe taarifa ya utafiti wako ambayo inaonesha waTanzania hawapendi kusoma.
 
Vita dhidi ya ukabila vianze kwetu sisi huku mashinani, nina uhakika viongozi wataishia kutuunga mikono, lakini kama tukiishi kuwasubiri hao waje na sera zozote, watakua wanatutumia kama mtaji.
Suluhisho ni kutengeneza sheria kali za kuzuia ukabila na vitendo vyake kama alivyofanya kagame
 
sipati picha mngekua tribes nyingi kama sisi........nadhani kenya pangekua moja yamaeneo yetu yakuchungia mifugo tu........
 
Back
Top Bottom