Kwa hili la Stiegler’s Gorge nami nasema President Trump, Stop That Wall

Patriot

JF-Expert Member
Feb 11, 2008
5,698
4,693
Wazungu kuendelea kuzuia miradi yetu kwa sababu za ‘nature’ naona bado wamaamini Afrika ibaki kuwa bara la giza ili watoto wao wakijifunza maisha ya watu wa zamani, waje wayaone Afrika. Haikubaliki. Nasubili niungwe mkono na Wamarekani kama wa-TZ wanavyounga mkono Wamarekani kuzuia ujenzi wa hydro power ya Stigler. Ni aibu kwamba kuna wa-TZ wanaodhani US inafahamu sana matatizo yetu au inatutakia mema sana kuliko rais wetu. Walipokuja na Lighting Africa, walikuja na miradi yao ya mitambo ya gesi. Matumaini ilikuwa ni kuvuna toka TZ. Kuna dalili wanaziona kwamba sasa mitambo yao haitahitajika sana tukiwa na hydro kuliko hiyo mitambo ya gesi ambayo ni ya kwao.

Kwa Wa-TZ wenzangu naomba tujadili. Sisi hatuna nafasi ya kushauri yanayotokea US. Iwe ni ukuta wa Texas/Mexico au mitambo yao ya nuklia. Hebu tuelewesheni kuna madhara gani ya ujenzi wa hydro ambayo ni makubwa kiasi cha kupigiwa kelele dunia nzima? Au ni hizo ripoti za WWF ambazo nyingi zimeandikwa na wa-TZ wenzetu, wengine tukiwafahamu ni dhaifu kitaaluma na wengine ikiwa ni sehemu ya upigaji? Lakini pia turudi kwenye maoni ya Rais. Je, machimbo ya Uranium na hiyo hydro, nini kina madhara kuliko kingine? Mbona hawajasema stop uranium mining?

Naomba tujadili, kitaalamu. Tuondoe hisia za kisiasa.
 
Wazungu kuendelea kuzuiya miradi yetu kwa sababu za ‘nature’ naona bado wamaamini Afrika ibaki kuwa bara la giza ili watoto wao wakijifunza maisha ya watu wa zamani, waje wayaone Afrika. Haikubaliki. Nasubili niungwe mkono na Wamarekani kama wa-TZ wanavyounga mkono Wamarekani kuzuia ujenzi wa hydro power ya Stigler. Ni aibu kwamba kuna wa-TZ wanaodhani US inafahamu sana matatizo yetu au inatutakia mema sana kuliko rais wetu. Walipokuja na Lighting Africa, walikuja na miradi yao ya mitambo ya gesi. Matumaini ilikuwa ni kuvuna toka TZ. Kuna dalili wanaziona kwamba sasa mitambo yao haitahitajika sana tukiwa na hydro kuliko hiyo mitambo ya gesi ambayo ni ya kwao.

Kwa Wa-TZ wenzangu naomba tujadili. Sisi hatuna nafasi ya kushauri yanayotokea US. Iwe ni ukuta wa Texas/Mexico au mitambo yao ya nuklia. Hebu tuelewesheni kuna madhara gani ya ujenzi wa hydro ambayo ni makubwa kiasi cha kupigiwa kelele dunia nzima? Au ni hizo ripoti za WWF ambazo nyingi zimeandikwa na wa-TZ wenzetu, wengine tukiwafahamu ni dhaifu kitaaluma na wengine ikiwa ni sehemu ya upigaji? Lakini pia turudi kwenye maoni ya Rais. Je, machimbo ya Uranium na hiyo hydro, nini kina madhara kuliko kingine? Mbona hawajasema stop uranium mining?

Naomba tujadili, kitaalamu. Asiyeyajua mmbo ya ikolojia aachane na thrd hii.

Sawa Mkuu nime kielewa hicho kipengele kwenye Red ,lakini nikuulize kitu ni kwa nini tujenge fikra za moja kwa moja kuwa Wazungu wana fanya haya kwa Sababu ya maslahi yao tu ?

Kwani hii Mikataba ya Upigaji huwa tunashikiwa Bunduki ili ku'Sign ?.

Wewe binafsi umeomba wasio na Elimu ya ikolojia waachane na hii thred ,it means haujui Madhara ya huo Mradi.Sasa ni kwa nini uje na hitimisho la moja kwa moja kuwa hamna Madhara?.

Gesi ya Mtwara ilipo gunduliwa tuliambiwa suala la Umeme itakuwa ni Historia ,hebu tueleze Matokeo ni kama hivi yalivyo?.
 
Kwanini tusiunde timu ya wazalendo wetu wafanye analysis na watupe report kamili juu ya madhara yatakayopatikana?Ina maana hatuna wataalamu ambao wanaweza kutuambia ukweli?Kupanga ni kuchagua,tukiamua tufumbe macho twende hivyo liwalo na liwe basi sawa,lakini tufanye hivyo tukiwa na tathimini halisi ya madhara!
 
Kwanini tusiunde timu ya wazalendo wetu wafanye analysis na watupe report kamili juu ya madhara yatakayopatikana?Ina maana hatuna wataalamu ambao wanaweza kutuambia ukweli?Kupanga ni kuchagua,tukiamua tufumbe macho twende hivyo liwalo na liwe basi sawa,lakini tufanye hivyo tukiwa na tathimini halisi ya madhara!

Timu ya wataalamu utashangaa Lusinde, Msukuma na Kessy wamo ndanu ya timu
 
Sawa Mkuu nime kielewa hicho kipengele kwenye Red ,lakini nikuulize kitu ni kwa nini tujenge fikra za moja kwa moja kuwa Wazungu wana fanya haya kwa Sababu ya maslahi yao tu ?

Kwani hii Mikataba ya Upigaji huwa tunashikiwa Bunduki ili ku'Sign ?.

Wewe binafsi umeomba wasio na Elimu ya ikolojia waachane na hii thred ,it means haujui Madhara ya huo Mradi.Sasa ni kwa nini uje na hitimisho la moja kwa moja kuwa hamna Madhara?.

Gesi ya Mtwara ilipo gunduliwa tuliambiwa suala la Umeme itakuwa ni Historia ,hebu tueleze Matokeo ni kama hivi yalivyo?.
Nawe sasa una mbio kuliko wengine. Unaona umuhimu wa hiyo red fonts? Ktk maandishi hayo umeona sehemu iliyoandikwa kwamba hakuna madhara? Tulia usome ukiwa huna presha. Kila mradi una madhara. KInachotafutwa huwa ni kulinganisha faida na madhara. Faida zimeshatajwa na serikali. Je, kwa hili madhara ni yapi?
 
Nawe sasa una mbio kuliko wengine. Unaona umuhimu wa hiyo red fonts? Ktk maandishi hayo umeona sehemu iliyoandikwa kwamba hakuna madhara? Tulia usome ukiwa na huna presha. Kila mradi una madhara. KInachotafutwa huwa ni kulinganisha faida na madhara. Faida zimeshatajwa na serikali. Je, kwa hili madhara ni yapi?

Mkuu unapo sema tunapigiwa kelele Dunia nzima ina maana tunapigiwa kwa kusifiwa au ?.Mantiki ya Bandiko lako unalifahamu kweli.

Jibu niliyo kuuliza hapo juu ,usilete blah blah hapa.
 
Mkuu unapo sema tunapigiwa kelele Dunia nzima ina maana tunapigiwa kwa kusifiwa au ?.Mantiki ya Bandiko lako unalifahamu kweli.

Jibu niliyo kuuliza hapo juu ,usilete blah blah hapa.
Hebu jielimishe bhana! Unachosha! Unauliza nini wewe? Leo hii hujui kelele ni nini?
 
Mie kwa hili namuunga mkono Rais kwa 100%. Kama ni hiyo mbuga kuharibika acha tu iharibike kwakuwa tunazo nyingi pia. Wanyama wataishi kutokana na mazingira mapya. Tunafadhiliwa miradi ya kusambaza umeme kama vile mcc kupitia REA ili baadae tushindwe katika kuzalisha na wenyewe ndio waweke mitambo yao. Mie katika hili sina mjadala kabisa aendelee tu mpaka kieleweke. Na hata kama hela hazitoshi afanye utaratibu kila mfanyakazi achangie 5% ya mshahara wake kwa miezi 2 au zaidi mbali na kodi (najua hapa nitaeleweka vibaya)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nawe sasa una mbio kuliko wengine. Unaona umuhimu wa hiyo red fonts? Ktk maandishi hayo umeona sehemu iliyoandikwa kwamba hakuna madhara? Tulia usome ukiwa na huna presha. Kila mradi una madhara. KInachotafutwa huwa ni kulinganisha faida na madhara. Faida zimeshatajwa na serikali. Je, kwa hili madhara ni yapi?

Rais wetu wakati tunaimbishwa wimbo wa gas kama wendawazimu ndio alikuwa anagonga meza huko bungeni mpaka mkono unataka kuvunjika, ni kipi leo ahamie kwenye umeme wa maji kama vile alikuwa jela wakati wa ngonjera za uchumi wa gas? Tunataka umeme wa kutosha hilo halina mjadala, lakini haiingii akilini mtu akalipe 6.5t kuharibu mazingira, aache kuingiza hizo hela kwenye gas. Huenda ikawa ww uko kwenye 10% ya huu umeme wa hydro, hivyo unatetea maana ulikosa 10% kwenye mradi wa gas.

Halafu kabla ya juzi rais kusaini mradi wa stiegler gorge kwa 6.5t, kila siku alikuwa anasema huo mradi utakuwa wa shilingi 3t na pesa zipo tena za ndani, kama sio mradi wa upigaji yeye na nyie genge lake iweje huo mradi ndani ya muda mfupi bei ifike hadi 6.5t tena za mkopo? Mkitaka tuwe pamoja tuambiwe kwanini tuache kuingiza hizo 6.5t kwenye gas na mazingira yabaki salama, kinyume na hapo wazungu wako sawa kwani viongozi wetu nao ni wapigaji kama wapigaji wengine.
 
Sawa Mkuu nime kielewa hicho kipengele kwenye Red ,lakini nikuulize kitu ni kwa nini tujenge fikra za moja kwa moja kuwa Wazungu wana fanya haya kwa Sababu ya maslahi yao tu ?

Kwani hii Mikataba ya Upigaji huwa tunashikiwa Bunduki ili ku'Sign ?.

Wewe binafsi umeomba wasio na Elimu ya ikolojia waachane na hii thred ,it means haujui Madhara ya huo Mradi.Sasa ni kwa nini uje na hitimisho la moja kwa moja kuwa hamna Madhara?.

Gesi ya Mtwara ilipo gunduliwa tuliambiwa suala la Umeme itakuwa ni Historia ,hebu tueleze Matokeo ni kama hivi yalivyo?.

Achana na watu wajinga wajinga, wanachafua na kuharibu walikotoka na kukimbikiq kuharibu sehemu nyingine na hawataki kujuliza huko walikontoka wamekosea wapi na kutoa ufafanuzi wa kina kwanini imekuwa tofauti na maelezo ya awali.

Nakumbuka sana ile kauri ya kwa gesi hii tuliyonayo mradi huu utafanya bei kuwa rahisi, kukatika umeme itakuwa historia, na watu watapikia umeme kuachana nanmkaa na kuni kuokoa mazingira.

Wengi hatuamini kinacho hubiriwa sasa kama kitakuwa kweli.
 
Sawa Mkuu nime kielewa hicho kipengele kwenye Red ,lakini nikuulize kitu ni kwa nini tujenge fikra za moja kwa moja kuwa Wazungu wana fanya haya kwa Sababu ya maslahi yao tu ?

Kwani hii Mikataba ya Upigaji huwa tunashikiwa Bunduki ili ku'Sign ?.

Wewe binafsi umeomba wasio na Elimu ya ikolojia waachane na hii thred ,it means haujui Madhara ya huo Mradi.Sasa ni kwa nini uje na hitimisho la moja kwa moja kuwa hamna Madhara?.

Gesi ya Mtwara ilipo gunduliwa tuliambiwa suala la Umeme itakuwa ni Historia ,hebu tueleze Matokeo ni kama hivi yalivyo?.
Kuhusu gesi ya Mtwara mnamuonea Magufuli, walioingia mkataba wa gesi ya Mtwara ni CCM (Chama Cha Mapinduzi), huu mradi wa Stigilas goji unaanzishwa na chama kipya japo nacho kinaitwa Ccm (Chama Cha Magufuli).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais wetu wakati tunaimbishwa wimbo wa gas kama wendawazimu ndio alikuwa anagonga meza huko bungeni mpaka mkono unataka kuvunjika, ni kipi leo ahamie kwenye umeme wa maji kama vile alikuwa jela wakati wa ngonjera za uchumi wa gas? Tunataka umeme wa kutosha hilo halina mjadala, lakini haiingii akilini mtu akalipe 6.5t kuharibu mazingira, aache kuingiza hizo hela kwenye gas. Huenda ikawa ww uko kwenye 10% ya huu umeme wa hydro, hivyo unatetea maana ulikosa 10% kwenye mradi wa gas.

Halafu kabla ya juzi rais kusaini mradi wa stiegler gorge kwa 6.5t, kila siku alikuwa anasema huo mradi utakuwa wa shilingi 3t na pesa zipo tena za ndani, kama sio mradi wa upigaji yeye na nyie genge lake iweje huo mradi ndani ya muda mfupi bei ifike hadi 6.5t tena za mkopo? Mkitaka tuwe pamoja tuambiwe kwanini tuache kuingiza hizo 6.5t kwenye gas na mazingira yabaki salama, kinyume na hapo wazungu wako sawa kwani viongozi wetu nao ni wapigaji kama wapigaji wengine.
Kama ni kisingizio cha mazingira, hakuna kitu hapo! Huwezi kutamka tu mazingira bila kueleza hasa yatakuwaje? Sema mazingira yatakuwaje?

Pamoja na kwamba unatumia lugha ya kushambulia, naomba nitumie lugha ya upole. Ukisoma taarifa ya huyo mama wa Amerika anayesema stop Stiegler, anashauri twende kwenye renewable energy. Wewe unafahamu kwamba hydro ni renewable na gas siyo renewable? Je, unafahamu gas tusipoitumia leo itabaki kwa miaka ijayo? Kuna nini wanalazimisha kwenda kwenye gesi sasa hivi? Nakushauri usumbue kichwa kusoma taarifa za nyuma na ujio wa Obama na kufunguliwa mradi wa gesi pale ubungo na kumbuka wamiliki ni wamarekani. Leo hii ndo watushauri kutumia gesi zaidi?
 
Kama ni kisingizio cha mazingira, hakuna kitu hapo! Huwezi kutamka tu mazingira bila kueleza hasa yatakuwaje? Sema amazingira yatakuwaje?

Pamoja na kwamba unatumia lugha ya kushambulia, naomba nitumie lugha ya upole. Ukisoma taarifa ya huyo mama wa Amerika anayesema stop Stiegler, anashauri twende kwenye renewable energy. Wewe unafahamu kwamba hydro ni renewable na gas siyo renewable? Je, unafahamu gas tusipoitumia leo itabaki kwa miaka ijayo? Kuna nini wanalazimisha kwenda kwenye gesi sasa hivi? Nakushauri usumbue kichwa kusoma taarifa za nyuma na ujio wa Obama na kufunguliwa mradi wa gesi pale ubungo na kumbuka wamiliki ni wamarekani. Leo hii ndo watushauri kutumia gesi zaidi?

Brother naona unazunguka na maneno tu, nimekuambia rais wetu chini ya miaka minne iliyopita alikuwa anaimba uchumi wa gas na hakuna popote alipinga suala lile. Leo tuna deni la mkopo wa gas kisha anahamia kwenye hydro tena kwa mkopo, kwani asituambie shida iko wapi kuendeleza kile alichokisifia muda mfupi? Huna maelezo yoyote zaidi ya kuokoteza maneno, mara Obama mara sijui nini. Rais ni msema kweli, atokeze aseme kwanini sio gas bali hydro tena kwa mkopo huku figure zake zikiwa na utata. Kinyume na hapo huo mradi ni upigaji kama huo anaoukimbia.
 
Wazungu kuendelea kuzuiya miradi yetu kwa sababu za ‘nature’ naona bado wamaamini Afrika ibaki kuwa bara la giza ili watoto wao wakijifunza maisha ya watu wa zamani, waje wayaone Afrika. Haikubaliki. Nasubili niungwe mkono na Wamarekani kama wa-TZ wanavyounga mkono Wamarekani kuzuia ujenzi wa hydro power ya Stigler. Ni aibu kwamba kuna wa-TZ wanaodhani US inafahamu sana matatizo yetu au inatutakia mema sana kuliko rais wetu. Walipokuja na Lighting Africa, walikuja na miradi yao ya mitambo ya gesi. Matumaini ilikuwa ni kuvuna toka TZ. Kuna dalili wanaziona kwamba sasa mitambo yao haitahitajika sana tukiwa na hydro kuliko hiyo mitambo ya gesi ambayo ni ya kwao.

Kwa Wa-TZ wenzangu naomba tujadili. Sisi hatuna nafasi ya kushauri yanayotokea US. Iwe ni ukuta wa Texas/Mexico au mitambo yao ya nuklia. Hebu tuelewesheni kuna madhara gani ya ujenzi wa hydro ambayo ni makubwa kiasi cha kupigiwa kelele dunia nzima? Au ni hizo ripoti za WWF ambazo nyingi zimeandikwa na wa-TZ wenzetu, wengine tukiwafahamu ni dhaifu kitaaluma na wengine ikiwa ni sehemu ya upigaji? Lakini pia turudi kwenye maoni ya Rais. Je, machimbo ya Uranium na hiyo hydro, nini kina madhara kuliko kingine? Mbona hawajasema stop uranium mining?



Naomba tujadili, kitaalamu. Asiyeyajua mmbo ya ikolojia aachane na thrd hii.




Tatizo lililopo ambalo Watz wengi hatulijui ni kwamba, wazungu wanao mpango wa kupunguza idadi ya watu weusi au kufanya watu weusi tusizaliane sana na hatimaye kuwazidi kwa idadi, katika kutimiza jambo wamefanya mambo kadhaa zikiwemo chanjo feki kudhuru afya zetu nk,

Njia nyingine ni kutuacha sisi tukiharibu mazingira yetu wenyewe mfano ukataji mkubwa wa miti kwa ajili ya nishati, kwa hivyo wanajua baada ya miaka kama 50 ijayo ardhi yetu itakuwa jangwa na maisha yatakuwa magumu mno kwa kukosa nishati na maji kutokana na ukataji miti mkubwa.

Sasa wanapoona tumepata njia ya kutatua shida ya nishati eti wanakuja kutuonea "HURUMA"!!! eti, tutaharibu mazingira!!?,Mazingira ya dunia "world heritage" !!.

Kwa kuanzisha mradi huo wa stieglier tutaokoa kwa kiwango kikubwa sana matumizi ya kuni na mkaa katika kupikia kwani umeme utakuwa mwingi na nafuu ambapo watu wata opt kutumia umeme kupikia badala ya kuni/mkaa na hivyo kulinda mazingira ukizingatia kwamba idadi ya watu wetu inaongezeka, as usual, exponentially.

Upande wa pili ni kushamiri kwa shughuli za viwanda kwa sababu umeme utakuwa mwingi na rahisi.

Cha msingi ni kusimamia ahadi za kupunguza bei ya umeme ili watu wengi wamudu kuupata.

Jambo la kuzingatia ni kwamba uhai waTembo wa selous si bora kuliko uhai wa roho moja ya Mtz.

Huwa napingana na serikali hii katika mambo kadhaa lakini kwa hili la stieglier naiunga mkono.

Umeme kwanza, hao hao wanaotupinga huko kwao umeme ni bwelele na cheap kinoma, kwanini hawataki tuwe kama wao??!!, Akili kichwani.

Wanatamani wahamie huku Afrika baada ya vita kuu ya 3 ya dunia kwa sababu kule kwao mazingira hayatakuwa sslamu kutokana na "nuclear fallout " hao wazungu Wanaimezea mate sana Africa.
 
Kwa kuanzisha mradi huo wa stieglier tutaokoa kwa kiwango kikubwa sana matumizi ya kuni na mkaa katika kupikia kwani umeme utakuwa mwingi na nafuu ambapo watu wata opt kutumia umeme kupikia badala ya kuni/mkaa na hivyo kulinda mazingira ukizingatia kwamba idadi ya watu wetu inaongezeka, as usual, exponentially.

Upande wa pili ni kushamiri kwa shughuli za viwanda kwa sababu umeme utakuwa mwingi na rahisi.
Huu wimbo si mlishatuimbia kipindi kile cha gas ya mtwara, nini kinachokufanya uamini hizi drama
Tena mkatuambia kupikia kuni na mkaa itakuwa historia kwasababu watu tutaunganishiwa mabomba ya gas hadi majumbani ha ha ha ha
 
Wazungu kuendelea kuzuiya miradi yetu kwa sababu za ‘nature’ naona bado wamaamini Afrika ibaki kuwa bara la giza ili watoto wao wakijifunza maisha ya watu wa zamani, waje wayaone Afrika. Haikubaliki. Nasubili niungwe mkono na Wamarekani kama wa-TZ wanavyounga mkono Wamarekani kuzuia ujenzi wa hydro power ya Stigler. Ni aibu kwamba kuna wa-TZ wanaodhani US inafahamu sana matatizo yetu au inatutakia mema sana kuliko rais wetu. Walipokuja na Lighting Africa, walikuja na miradi yao ya mitambo ya gesi. Matumaini ilikuwa ni kuvuna toka TZ. Kuna dalili wanaziona kwamba sasa mitambo yao haitahitajika sana tukiwa na hydro kuliko hiyo mitambo ya gesi ambayo ni ya kwao.

Kwa Wa-TZ wenzangu naomba tujadili. Sisi hatuna nafasi ya kushauri yanayotokea US. Iwe ni ukuta wa Texas/Mexico au mitambo yao ya nuklia. Hebu tuelewesheni kuna madhara gani ya ujenzi wa hydro ambayo ni makubwa kiasi cha kupigiwa kelele dunia nzima? Au ni hizo ripoti za WWF ambazo nyingi zimeandikwa na wa-TZ wenzetu, wengine tukiwafahamu ni dhaifu kitaaluma na wengine ikiwa ni sehemu ya upigaji? Lakini pia turudi kwenye maoni ya Rais. Je, machimbo ya Uranium na hiyo hydro, nini kina madhara kuliko kingine? Mbona hawajasema stop uranium mining?

Naomba tujadili, kitaalamu. Asiyeyajua mmbo ya ikolojia aachane na thrd hii.
Kuchimbwa uranium Selous bila kuzingtia athari zake kimazingira haukuwa uamuzi wa busara na hakuhalalishi mradi wa Steigler's Gorge. Two wrongs don't make one right! Jibuni swali kwa nini gesi ya Mtwara isitumike kuongeza uzalishaji wa umeme?
Haya ni maswali toka kwa wadau wa maendeleo na mazingira ambao wana hoja za msingi. Tunakoenda dunia itahitaji kulinda vyanzo vya maji kwakuwa idadi ya watu inaongezeka na ukame unaongezeka. Katika maamuzi yetu leo lazima tuzingatie mahitaji ya sasa na ya vizazi vijavyo. Hakuna anaebisha kwamba nia ya JPM kuhusu kuongeza uzalishaji wa umeme ni nzuri; bali kwamba njia mbadala kama gesi, upepo, jua na themo zisingetosha au zina athari gani kimazingira?
Mwisho kwakuwa uamuzi umeshafanyika hoja hizi zibaki kama record kwa dunia ya sasa na vizazi vijavyo.
Democracy ni maamuzi ya wengi, ila Mwalimu Nyerere alisema kwamba pamoja na hivyo maoni ya wachache yasikilizwe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom