Kwa hili la mmundo wa muungano wetu tumwache baba wa taifa alale kwa amani.

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,681
1,698
Sasa naamini wanaotaka muungano wetu uvunjike ni wale wanaopendelea muundo huu wa sasa wa muungano uendelee. Ukiwauliza watoe sababu za kuuendeleza wakati pana manung'uniko na sasa panawengine wanawaza uvunjike, jibu wanakupa jepesi tu Baba wa taifa aliishasema ni gharama na kuwa na serikali tatu ni kuuwa muungano basi. Hawana mawazo yao mbadala ya kuwaza kwanza baba wa taifa alitoa maoni hayo kwa wakati gani na hawaoni kuwa alitilia shaka uundwaji wa erikali tatu kwa jazba ndio kuuwa muungano, hawafikirii hayo. Muungano lazima uboreshwe kwa kuwa na serikali TATU, wote wanaopendekeza hilo hawajasema utavunjika ila ni KUUBOSHA ili kupunguza (si kumaliza) malalamiko yake. Nawasihi sana wanaomtumia baba wa taifa letu kwa suala hili WAACHE ili aendelee kulala kwa amani huko aliko. Wengine walikuwa madarakani na hawakutaka/hawataki kurejesha Azimoi la Arusha ambalo baba wa taifa alisema yeye alitembea na vitabu viwili tuu 1-Azimio la Arusha (sio katiba wala ilani ya chama chake) na 2-Biblia takatifu (hii kwa imani yake yake ya dini). Suala sasa lilikuwa ni kuipongeza tume kwa kusikiliza maoni ya wananchi (sio vyama) na kuona mbali kwa angalau miaka hamsini ijayo ya taifa letu ila tuwaulize kama Zanzibar na Tanganyika ndio wazazi wa Tanzania ilikuwaje katika rasimu hii majina hayo hayamo? Hii hata mwandishi mkongwa Ahmed Rajabu kalitilia shaka.Nawasilisha.......
 
Yapo mengi yamevunjwa na muasisi ni Baba wa Taifa! Iweje habari ya muungano pekee? Palipo na mirija ya ulaji wa wachache, baba wa Taifa anatajwa kweli kweli. Lakini ambapo kuna sera za kubana maslahi ya wachache....kimyaaa!!
 
umenena mwanangu baadhi watu hasa watawala wanaogopa mabadiliko sijui kwanini.hawataki kwenda na nyakati kuna baadhi ya watu wanafikiri bado fikara za mwaka 1960 zanafaa 2013.Mungano wa sasa umetufaa kwa wakati huo lakini sio sasa.
 
Back
Top Bottom