Kwa hili la kutishwa kwa Zitto Kabwe, Bunge si sehemu salama!

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Mbunge ni nani?
Mbunge ni mwakilishi wa walipa kodi ambaye anawajibika kwa wananchi na kwa Bunge kwa kuwa ndicho chombo cha uwakilishi wa wananchi.

Unapomtishia Mbunge wa wananchi usalama wa maisha yake, unawatishia wananchi waliomtuma pale. Hakujipeleka pale kama walivyo wabunge wa “Jimbo la Ikulu”, alikwenda kwa matakwa ya wananchi kusimamia maslahi ya umma.

Bunge letu ni la mfumo wa vyama vingi, hata iweje litapinga hoja za upinzani bungeni kwa hoja na si vinginevyo. Ndiyo maana kwa kupitia wingi wao(majority) Bunge limekuwa likipitisha maamuzi mengi yasiyo na tija kwa kuwa kiti cha Spika kinaongozwa na MNEC wa CCM na mwanachama wa chama hicho aliyeshindwa kuzuia mihemuko ya kichama.

Tumeona mara nyingi wakosoaji wa mifumo ya kiuongozi ndani ya bunge wamekuwa wahanga wakubwa wa mfumo huo kwa kudhalilishwa mara kwa mara na kutishiwa maisha yao hasa pale wanapo pambania maslahi mapana ya wananchi.

Hakuna asiyejua umuhimu wa kambi ya upinzani bungeni, umuhimu wake ndiyo unao lirudisha bunge kwenye mstari kwa kulikumbusha majukumu yake ya kibunge kwani ndicho chombo cha uwakilishi wa wananchi.

Ukitazama Bunge letu, huwezi amini kama ni chombo cha uwakilishi wa wananchi chenye majukumu ya kuisimamia serikali na kuishauri. Mijadala iliyoko pale, wabunge wa upinzani wanaikosoa serikali na kuielekeza na wabunge wa chama kinachotawala wanapinga na kuitetea serikali ya chama chao iliyoko madarakani, ndiyo maana kwa dhana hii Bunge letu linaonekana dhaifu.

Kwa udhaifu huu, chombo hiki kimeshindwa kwa makusudi kuwasimamia wabunge wake hususani wa upinzani pale wanapotishwa na watendaji wa mhimili wa serikali kutoka kitengo maalumu (intelligence special unit).

Kwa kitendo cha kumtishia mwakilishi wa wananchi bungeni kama alivyothibitisha mh. Zitto Zuberi Kabwe, ni kinyume na haki na kinga za mamlaka ya bunge kwa wabunge. Ikiwa Mbunge anatishwa sisi tuliomtuma ajatuwakilishe tupo salama kwa kiwango gani!!!!

Ni wakati wa kiti kulitazama jambo hili kwa upana wake, huenda maadui wa bunge wakatumia fursa hii kulichafua bunge zaidi wakidhani wanalisaidia.

Hoja za wabunge hujibiwa kwa hoja na si vitisho, tukiruhusu hawa wasiojulikana kuliingilia bunge letu tutaharibu afya ya mjadala.

Kwa kuwa Bunge si idara ya serikali bali ni mhimili unaojitegemea, halina budi kurudi kwenye majukumu yake ya kiutendaji kwa mujibu wa katiba, sheria na kanuni, kwa kuachana na ubabe usio na tija kwa maslahi ya taifa.

Tunamtaka Mh. Spika aunde Kamati ya kuchunguza matukio yanayotishia uhai wa wabunge wake ili kurudisha imani na Bunge letu kuwa salama kwa wabunge wake wote bila kujali itikadi, vinginevyo ukimya huu wa bunge tafsiri yake ni kubariki vitendo hivi vya vitisho.
 
Sasa hakuna bunge la wananchi, bali kuna bunge la serikali

Halafu mjinga fulani anayeliongoza bunge akiwa amejificha uchochoroni ndio anajiita mzalendo kuliko watu wote!

Wakiambiwa madhaifu yao wanang'aka kama wamechukuliwa wake zao

Kwa hili bunge la hovyo na gharama zake za uendeshaji ni ufisadi mkubwa mno kuendelea kuwa nalo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wangemfyekelea mbali tu huyo walahi
Viva kijana shupavu, MAMA TANZANIA HATAKI TENA UJINGA WALAHI
Zito lime chacha sasa kazi yake ni kujaribu kuchafua serikali, aah wapi, kagonga mwamba walahi
Zito kwishney walahi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Elimination schedule in categories
Powerful/famous people
Powerful/famous politicians
Powerful/famous businessmen
Aggressive journalists
Fearless critics
Unstoppable whistle blowers
Free young speakers
Anybody who seem to be trouble maker

*Pls learn to know your category n schedule.... Then get prepared... They are up on their heels coming.. .. Fully equipped
tapatalk_1545605978560.jpeg


Jr
 
TL kayashinda mauti sehemu Salama,hivyo si Salama sana Kwa wapinga ufisadi, muhimu wavae body camera kisha warushe sura zao kwenye mitandao jamii iwashugulikie.TL Ben walianza hivihivi wakilalamika kabla hayajawakuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani hairuhusiwi kuingia na bastola kwenye viwanja vya bunge?

Yule jamaa aliyewafyatulia risasi wasiojulikana kesi yake imefika wapi?

Deep down kila binadamu ni muoga.
Wamemuhifadhi ghalani yeye na mke wake ili wafilisike baada ya biashara zao kukosa usimamizi kisha wataachiwa baada ya kufilisika kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom