Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Jana nilisoma katika safu hizi, barua ndefu iliyoandikwa na Jenerali Ulimwengu kwa JK. Nianze kwa kukiri kwamba barua ya aina hiyo hiyo, niliwahi kuiona katika gazeti la Rai ama mwishoni mwa mwaka 2005 au mwanzoni mwa mwaka 2006. Kwa maoni yangu,barua hii ilipotokea kwa hiyo mara ya kwanza, ilikuwa inastahili. Lakini kwasasa, kwa baadhi yetu barua hiyo inatia kichefuchefu, kwani inapindisha ukweli ulivyo. Mwaka 2005 wakati JK anaingia madarakani watu wengi tuliamini ya kwamba sasa tumempata mkombozi wa kweli, ambaye angeliondoa nchi yetu katika shimo la ukoloni mamboleo, ambamo ilitumbukizwa na utawala wa Mkapa, na kuielekeza katika njia ya uhuru kamili kiuchumi. Miaka mitano ya uongozi wake, imekuwa ni ya kukatisha tamaa kwa yeyote yule mwenye mapenzi mema na nchi yetu. Chini ya uongozi wake siyo tu kwamba nchi yetu imeendelea kupoteza rasilimali nyingi kwa uporaji na matumizi mabaya ya serikali, lakini pia kuna kila dalili zinazodhihilisha ya kuwa nchi yetu kama taifa imepoteza mwelekeo.Hali hiyo imesababisha watu wengi kupoteza imani waliyokuwa nayo kwa JK. Kwanini basi, mtu kama Jenerali, kwa wakati huu tulionao, anaamua kupindisha ukweli huo na kuaanza kumuita JK mkombozi! naomba kwa yeyote mwenye jibu anitegulie kitendawili hicho.