Elice Elly
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 1,268
- 1,593
Jana Jumapili Chama cha Mapinduzi walikuwa na mkutano katika eneo la Stand ya Mlandege.
Katika mkutano ule alikuwepo pia Humphrey Polepole,Mbunge wa viti Maalum wa CCM ambaye jina lake sikulisikia vizuri,madiwani wa CCM, na baadhi ya VIONGOZI wa CCM.
Mimi pamoja na Baadhi ya vijana Tulikuwa eneo la Shule ya Msingi Mlandege tukiwa tunawasubiri wenzetu ili tukafanye mazoezi katika uwanja wa mpira wa Shule ya msingi Mlandege, ghafla walitokea vijana wawili wakatuuliza nyinyi hamuendi kusikiliza mkutano?
Tukawaambia sisi tunawasubiri wenzetu tunaenda kufanya mazoezi, wakatuambia kama hamuendi mkutanoni basi ondokeni katika eneo hili.
Tuliwajibu kwa ustaarabu kuwa sisi tupo katika eneo hili la Shule tunaenda kufanya mazoezi. Ghafla tukasikia mawe yameanza kurushwa kuelekea tuliko,mengine yalitupata na mengine yalitua kwenye paa la Shule.
Kumbe wale vijana walikuwa ni kundi Kubwa na wengine walikuwa ndani ya Noah.Hata tulipoamua kuondoka waliendelea kuwazonga baadhi yetu na binti mmoja walimvua mpaka mtandio wake,na Baadaye waliendelea kumnyanyasa mpaka alipopata msaada toka kwa wananchi wema.
Tukio lile limenifanya nikose usingizi,natafakari na kujiuliza ina Mikutano yetu ya siasa tumefikia hatua ya kulazimisha watu wahudhurie?
Je, watu wanaofanya shughuli zao jirani na eneo la mikutano ya vyama wanalazimika kuacha shughuli zao kwenda kwenye mikutano?
Kama Leo wanatumia nguvu kulazimisha watu waende mikutanoni mwakani itakuwaje?
Lakini swali jingine ni kwamba nani aliwatuma wale vijana wadogo kuja kutufanyia vurugu watu ambao tulikuwa kwenye majukumu yetu? Wale vijana wamefundishwa na Nani kuyatenda Yale waliyotenda?
Kama Leo katika umri ule wanatumika kuwafanyia watu vurugu,wakisha kuwa watu wazima watatumia tena mawe au watafanya makubwa zaidi?
Kwa kweli tunahitaji Neema ya Mungu vinginevyo tunatengeneza makundi hatari sana katika nchi yetu.
Katika mkutano ule alikuwepo pia Humphrey Polepole,Mbunge wa viti Maalum wa CCM ambaye jina lake sikulisikia vizuri,madiwani wa CCM, na baadhi ya VIONGOZI wa CCM.
Mimi pamoja na Baadhi ya vijana Tulikuwa eneo la Shule ya Msingi Mlandege tukiwa tunawasubiri wenzetu ili tukafanye mazoezi katika uwanja wa mpira wa Shule ya msingi Mlandege, ghafla walitokea vijana wawili wakatuuliza nyinyi hamuendi kusikiliza mkutano?
Tukawaambia sisi tunawasubiri wenzetu tunaenda kufanya mazoezi, wakatuambia kama hamuendi mkutanoni basi ondokeni katika eneo hili.
Tuliwajibu kwa ustaarabu kuwa sisi tupo katika eneo hili la Shule tunaenda kufanya mazoezi. Ghafla tukasikia mawe yameanza kurushwa kuelekea tuliko,mengine yalitupata na mengine yalitua kwenye paa la Shule.
Kumbe wale vijana walikuwa ni kundi Kubwa na wengine walikuwa ndani ya Noah.Hata tulipoamua kuondoka waliendelea kuwazonga baadhi yetu na binti mmoja walimvua mpaka mtandio wake,na Baadaye waliendelea kumnyanyasa mpaka alipopata msaada toka kwa wananchi wema.
Tukio lile limenifanya nikose usingizi,natafakari na kujiuliza ina Mikutano yetu ya siasa tumefikia hatua ya kulazimisha watu wahudhurie?
Je, watu wanaofanya shughuli zao jirani na eneo la mikutano ya vyama wanalazimika kuacha shughuli zao kwenda kwenye mikutano?
Kama Leo wanatumia nguvu kulazimisha watu waende mikutanoni mwakani itakuwaje?
Lakini swali jingine ni kwamba nani aliwatuma wale vijana wadogo kuja kutufanyia vurugu watu ambao tulikuwa kwenye majukumu yetu? Wale vijana wamefundishwa na Nani kuyatenda Yale waliyotenda?
Kama Leo katika umri ule wanatumika kuwafanyia watu vurugu,wakisha kuwa watu wazima watatumia tena mawe au watafanya makubwa zaidi?
Kwa kweli tunahitaji Neema ya Mungu vinginevyo tunatengeneza makundi hatari sana katika nchi yetu.