fizo talent
JF-Expert Member
- Oct 17, 2017
- 2,257
- 3,882
Habari za weekend wakuu,
Nielekee kwenye mada moja kwa moja, leo nikiwa katika usafiri wa umma maarufu kama daladala inayofanya safari zake Chanika to Machinga Complex nilishuhudia tukio ambalo gari aina Harrier ikiwa barabarani katika eneo ambalo barabara ni mbovu, hivyo alilazimika kusubiri gari inayotoka mjini ipite ili na yeye aweze kupita.
Kilichotokea akiwa hana hili wala lile dereva bodaboda akiwa amepakia vijana wenzie wawili maarufu kama mshkaki walikuja wakaigonga ile gari kwa nyuma na taa ya nyuma ya gari kupasuka pale pale na hapo ilikuwa ni eneo la stendi kuna boda boda nyingine zimepaki pembeni japo kwa haraka haraka inaonekana yule aliyegonga ile gari hapaki katika kituo kile.
Baada ya tukio, maana dereva na abiria wake wote walianguka na kosa alilofanya dereva wa ile gari ajali ilivyotokea hakutoka pale pale katika gari yake, basi dereva wa ile pikipiki aliamka na kunyanyua pikipiki yake na kufanikiwa kuiwasha na kukimbia kwa mwendo mkali kabisa, madereva wa pikipiki wengine wa hapo kijiweni wakawa wanamuangalia tu.
Dereva wa gari kuja kutoka dereva wa pikipiki kashatokomea na hapo madereva wa pikipiki hata kusogea eneo la tukio hawakusogea.
Abiria tuliokuwa kwenye usafiri wote tulipigwa na butwaa, ingetokea dereva boda boda ndio amegongwa na mwenye gari kukimbia hapo angefukuziwa na akishikwa lazima achezee na kipigo kwanza.
Haki yako ipiganie wewe mwenyewe kwanza na sio kutegemea msaada wa wasamaria wema, unaweza ukapoteza haki yako kwa kuwategemea walimwengu.
Weekend njema!
Nielekee kwenye mada moja kwa moja, leo nikiwa katika usafiri wa umma maarufu kama daladala inayofanya safari zake Chanika to Machinga Complex nilishuhudia tukio ambalo gari aina Harrier ikiwa barabarani katika eneo ambalo barabara ni mbovu, hivyo alilazimika kusubiri gari inayotoka mjini ipite ili na yeye aweze kupita.
Kilichotokea akiwa hana hili wala lile dereva bodaboda akiwa amepakia vijana wenzie wawili maarufu kama mshkaki walikuja wakaigonga ile gari kwa nyuma na taa ya nyuma ya gari kupasuka pale pale na hapo ilikuwa ni eneo la stendi kuna boda boda nyingine zimepaki pembeni japo kwa haraka haraka inaonekana yule aliyegonga ile gari hapaki katika kituo kile.
Baada ya tukio, maana dereva na abiria wake wote walianguka na kosa alilofanya dereva wa ile gari ajali ilivyotokea hakutoka pale pale katika gari yake, basi dereva wa ile pikipiki aliamka na kunyanyua pikipiki yake na kufanikiwa kuiwasha na kukimbia kwa mwendo mkali kabisa, madereva wa pikipiki wengine wa hapo kijiweni wakawa wanamuangalia tu.
Dereva wa gari kuja kutoka dereva wa pikipiki kashatokomea na hapo madereva wa pikipiki hata kusogea eneo la tukio hawakusogea.
Abiria tuliokuwa kwenye usafiri wote tulipigwa na butwaa, ingetokea dereva boda boda ndio amegongwa na mwenye gari kukimbia hapo angefukuziwa na akishikwa lazima achezee na kipigo kwanza.
Haki yako ipiganie wewe mwenyewe kwanza na sio kutegemea msaada wa wasamaria wema, unaweza ukapoteza haki yako kwa kuwategemea walimwengu.
Weekend njema!