Kwa hii style Single Parent haitakuja Kufa

Akili Unazo!

JF-Expert Member
Feb 18, 2009
3,930
4,892
Vitenge doti 1,viatu pea 1,kilemba,Sabuni miche 2,Mafuta ya kupakaa,fedha tsh.10000, mahari: majembe 2 au tsh:20000,blanketi 2 kubwa na mashuka 2,mbuzi 2 beberu au tsh:200000,mbuzi wa 5 au tsh:250000,ng'ombe 4 au tsh:600000,fungu la fedha 800000,soda thelathini tsh:30000,mfuko au begi la Mali sawa tsh:15000, : MKAJA WA MAMA 100000,MSHENGA TSH:30000 NA FUNGA MLANGO TSH:250000
 
Vitenge doti 1,viatu pea 1,kilemba,Sabuni miche 2,Mafuta ya kupakaa,fedha tsh.10000, mahari: majembe 2 au tsh:20000,blanketi 2 kubwa na mashuka 2,mbuzi 2 beberu au tsh:200000,mbuzi wa 5 au tsh:250000,ng'ombe 4 au tsh:600000,fungu la fedha 800000,soda thelathini tsh:30000,mfuko au begi la Mali sawa tsh:15000, : MKAJA WA MAMA 100000,MSHENGA TSH:30000 NA FUNGA MLANGO TSH:250000
Hujalazimishwa

Ndio ukubwa na hishima
 
Kuna mzee mmoja alikataa mshikaji wangu wakati anaenda kuposa,

Jamaa alipeleka kama 1.3M bila kitu chochote ili ajitetee akijakupata vingine ataenda kumalizia, yule mzee akamtolea nje mwana, yule mwana kazira kaoa mwingine alafu yule binti wa mzee kazalishwa akiwa pale pale home kwao
 
kama kipato kwa mwaka hakizizi milioni 10, ni ufara kutoa mahali ya zaidi ya m2,

binafsi kipato hakizidi m8, nilipotaka kuoa wakwe wakang'ang'ania m2.4 nilikataa nikapiga chini kabisa, kumbe dogo alikuwa kijacho tayari, amehamia kwangu tayari na ile m1.2 niliyotaka kuwapa wakaikataa nimeifungua kiduka wife/mchumba anadunduliza ya mboga.


tupingeni mahali jamani, kama vipi watoe wao
 
Njoo huku pwani, wamakonde na wazaramo wanajua mahaba kwelikweli na mahari hatulipi kwa Ng'ombe wala Mbuzi. 50,000 hadi 100,000 unamchukua mke. Achana na watu wa bara hawajui kupika, washamba, kitandani zero lakini mahari milion mia.
 
kama kipato kwa mwaka hakizizi milioni 10, ni ufara kutoa mahali ya zaidi ya m2,

binafsi kipato hakizidi m8, nilipotaka kuoa wakwe wakang'ang'ania m2.4 nilikataa nikapiga chini kabisa, kumbe dogo alikuwa kijacho tayari, amehamia kwangu tayari na ile m1.2 niliyotaka kuwapa wakaikataa nimeifungua kiduka wife/mchumba anadunduliza ya mboga.


tupingeni mahali jamani, kama vipi watoe wao
Safi sana mkuu, huwa napatwa na kigugumizi kwa nini wanataka kuanza maisha(bwana na bibi harusi) ndo wananyang'anywa na kuchukua wazee ( upande wa bibi harusi) ambao tyari weshajipanga, na kama bado hawajajipanga ni jukumu la bwana harusi kuwapanga kwa kupitia maali??!

Kama logic ni fadhira za malezi ya binti yao, kwani wazazi wa bwana harusi yanalipwa na nani?? Na usikute bibi harusi ana tabia mbaya kimalezi kuliko hata bwana harusi!
 
Toa kidogo tu waambie nyingine unaendelea kutafuta alafu beba mzigo kaendelee kufaidi. kwanza kuna baadhi ya makabila ukitoa zote wanakupiga faini eti umewadharau
 
Njoo huku pwani, wamakonde na wazaramo wanajua mahaba kwelikweli na mahari hatulipi kwa Ng'ombe wala Mbuzi. 50,000 hadi 100,000 unamchukua mke. Achana na watu wa bara hawajui kupika, washamba, kitandani zero lakini mahari milion mia.
Buda hao watoi wa mwambao hawawazidi dada zetu huku bara.
 
Kwenye utamaduni na mila kuna utamu wake, kama hautaki kuoa kaa ulivyo.

Itakubidi utoe tu...mbona zamani au hata baadhi ya makabila wanatoa hadi ng'ombe thelathini?
Kuna jamaa mmoja alioa singida mwezi april,2017 aliambiwa pamoja na mahari aliyotoa pia watapewa shamba huko ukweni ekari 2 yeye na mkewe wazilime hadi kuvuna halafu wawaachie wakwe hayo mavuno au wajenge nyumba ya block....hivyo jamaa kwa sababu alikuwa nazo(pesa) akaamua kuwajengea nyumba.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom