Kwa hii aibu tunayopata UKAWA kwa kususa Bunge, Mama Regina Lowassa alikuwa sahihi kukataa ubunge

Kada wa CHADEMA

JF-Expert Member
Feb 27, 2016
289
615
Kwa sasa imekuwa ni aibu kubwa kujitambulisha hadharani kuwa mimi ni mwana CHADEMA kutokana na aibu kubwa ambayo wabunge wetu wa UKAWA wanatuletea kule Dodoma. Ndio maana hata zile sare za CHADEMA ambazo ilikuwa ni kawaida kuziona mitaani kwa sasa zimepotea kabisa. Imekuwa ni kawaida katika maisha yetu ya kila siku kuwa mtu anayesusa mara nyingi ndiye anayepata hasara. Ndio maana kuna msemo wa Kiswahili unaosema kuwa UKISUSA SISI TWALA.

Ndivyo inavyotokea Bungeni, maamuzi yetu ya kususa vikao vya bunge eti kwa vile tu hatumpendi Naibu Spika, Daktari Tulia Akson yamekuwa na mafanikio Hasi kwa Kambi ya Upinzani. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, kususa kwetu hakujakwamisha mijadala ya bunge la Bajeti Bungeni. Sana sana imeongeza speed ya wabunge wa CCM kupitisha bajeti hiyo bila kuwa na michango yetu.

Nakumbuka wakati wa Uteuzi wa Wabunge wa Viti Maalum CHADEMA, Baraza la Wanawake CHADEMA walitenga nafasi moja kwa mama yetu Regina Lowasa kutokana na mchango alioutoa kwa umoja huo na chama kwa ujumla wakati wa kampeni za Urais. Hata hivyo, mama yetu alitumia busara kukataa nafasi hiyo. Alikataa si kwa sababu hakupenda kujenga historia kuwa aliwahi kuwa mbunge bali aliona mbali kutokana na hulka za viongozi wa kambi ya Upinzani na hasa mwenyekiti wetu Freeman Mbowe.

Bunge lililopita, CHADEMA tulideka sana Bungeni na mara nyingi tuliweka mpira kwapani. Mama Regina Lowasa aliona hilo kuwa hata Bunge hili, hali na tabia ya viongozi wa upinzani itakuwa ile ile ndo maana akaamua kukataa nafasi hiyo.

Najaribu kutengeneza taswira. Hivi na yeye kama angekuwa Mbunge, angefuata mkumbo wa kususa? Kama angefanya hivyo, hakika tusingemtendea haki mama yetu kwa kumuingiza bungeni then baada ya dakika tano tunamtoa. Hii inga toka inga toka inga toka hakika ingekuwa ni kumtusi mama yetu na Mzee Lowasa.

Hakika CHADEMA tusipobadilika, tutaendelea kuwa na wabunge fuata mkumbo na si wenye maono kama Mama Regina Lowasa
 
Kwa sasa imekuwa ni aibu kubwa kujitambulisha hadharani kuwa mimi ni mwana CHADEMA kutokana na aibu kubwa ambayo wabunge wetu wa UKAWA wanatuletea kule Dodoma. Ndio maana hata zile sare za CHADEMA ambazo ilikuwa ni kawaida kuziona mitaani kwa sasa zimepotea kabisa. Imekuwa ni kawaida katika maisha yetu ya kila siku kuwa mtu anayesusa mara nyingi ndiye anayepata hasara. Ndio maana kuna msemo wa Kiswahili unaosema kuwa UKISUSA SISI TWALA.

Ndivyo inavyotokea Bungeni, maamuzi yetu ya kususa vikao vya bunge eti kwa vile tu hatumpendi Naibu Spika, Daktari Tulia Akson yamekuwa na mafanikio Hasi kwa Kambi ya Upinzani. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, kususa kwetu hakujakwamisha mijadala ya bunge la Bajeti Bungeni. Sana sana imeongeza speed ya wabunge wa CCM kupitisha bajeti hiyo bila kuwa na michango yetu.

Nakumbuka wakati wa Uteuzi wa Wabunge wa Viti Maalum CHADEMA, Baraza la Wanawake CHADEMA walitenga nafasi moja kwa mama yetu Regina Lowasa kutokana na mchango alioutoa kwa umoja huo na chama kwa ujumla wakati wa kampeni za Urais. Hata hivyo, mama yetu alitumia busara kukataa nafasi hiyo. Alikataa si kwa sababu hakupenda kujenga historia kuwa aliwahi kuwa mbunge bali aliona mbali kutokana na hulka za viongozi wa kambi ya Upinzani na hasa mwenyekiti wetu Freeman Mbowe.

Bunge lililopita, CHADEMA tulideka sana Bungeni na mara nyingi tuliweka mpira kwapani. Mama Regina Lowasa aliona hilo kuwa hata Bunge hili, hali na tabia ya viongozi wa upinzani itakuwa ile ile ndo maana akaamua kukataa nafasi hiyo.

Najaribu kutengeneza taswira. Hivi na yeye kama angekuwa Mbunge, angefuata mkumbo wa kususa? Kama angefanya hivyo, hakika tusingemtendea haki mama yetu kwa kumuingiza bungeni then baada ya dakika tano tunamtoa. Hii inga toka inga toka inga toka hakika ingekuwa ni kumtusi mama yetu na Mzee Lowasa.

Hakika CHADEMA tusipobadilika, tutaendelea kuwa na wabunge fuata mkumbo na si wenye maono kama Mama Regina Lowasa

Huo ndio upinzani, au unadhani upinzani ni kugonga meza tu?
 
Point taken. Kada wa CHADEMA siku zote katika ubora wako japo wenzako hawakupendi. Huo ndo uhalisia
 
Hahahahaha dogo naona unaiga style ya Mzee tupa tupa, kamwe hutaweza njoo na sound mpya!!
 
Nimesoma heading yako tuu nakuona ni upuuzi hivyo sijasoma zaidi kwani utakuwa upuuzi zaidi.
Usipotoshe kama wanavyopotosha waji.nga wengine.
UKAWA HAWAJASUSIA BUNGE BALI WAMEMSUSIA TULIA. Ndio maana bunge likisimamiwa na wenyeviti au Ndugai angekuwepo wanaingia ukumbini.
Na kwa kiburi cha Tulia kaamua kuto wapa nafasi wenyeviti ili akiingia yeye watoke. Ni ujinga uliopitiliza kiwango cha hekima ya kawaida.
 
Nimesoma heading yako tuu nakuona ni upuuzi hivyo sijasoma zaidi kwani utakuwa upuuzi zaidi.
Usipotoshe kama wanavyopotosha waji.nga wengine.
UKAWA HAWAJASUSIA BUNGE BALI WAMEMSUSIA TULIA. Ndio maana bunge likisimamiwa na wenyeviti au Ndugai angekuwepo wanaingia ukumbini.
Na kwa kiburi cha Tulia kaamua kuto wapa nafasi wenyeviti ili akiingia yeye watoke. Ni ujinga uliopitiliza kiwango cha hekima ya kawaida.
Kwa bahati mbaya sana CCM wametujua. Ndo maana wamemuweka Dr Tulia kuongoza vikao vyote. Hapo ndipo tuliponasa. Tumesusa wenzetu wanakula kimya kimya
 
Hahahahaha dogo naona unaiga style ya Mzee tupa tupa, kamwe hutaweza njoo na sound mpya!!
Bora mzee tupatupa yeye ni kweli mwana ccm haswa ila huyu ni msanii kaweka jina tu wakati anafahamika kuwa ni mwana ccm tangu kitambo sana ,,,,, go on magufuri tuko pamoja kutokomeza mafisadi hasa tukianza na wale mapapa siku ukiamua rais wangu
 
Ni uhakika kama huyo Mama angekubali huo uteuzi, mengi yangesemwa zaidi ya haya ni vizuri alipokataa ili kuipunguzia soko single ya "chama kuuzwa". Kumbuka kuna aina nyingi za kuonyesha kutoridhishwa na hali iliyopo hata katika mahali pa kazi au mshuleni kunakuwa na migomo pale wanaoona hawatendewi haki.
 
Yaani wasione aibu wabunge wa ccm wanaotetea wasikatwe kodi kiinua mgongo chao waje waone wa ukawa ambao mtaani tunawaona mashujaa? kwakifupi bunge halina mvuto kwasasa hata kwenye taarifa za habari hakuna la maana lolote la kuonyesha kutoka bungeni.

"" Sana sana imeongeza speed ya wabunge wa CCM kupitisha bajeti hiyo bila kuwa na michango yetu.""

Nashukuru kwa kutambua mchango wa maoni ya majembe ya ukawa kwa hiyo sentensi yako kada wa ccm ukijivika koti la chadema
 
Hii tabia ya kususa susa wameitoa wapi..?mbona Baba wa baba zao hatukuwaona wanasusa..mmh wasijeambukiza wajukuu ikawa kama tupo enzi zilee za chama kimoja..!
 
Bora mzee tupatupa yeye ni kweli mwana ccm haswa ila huyu ni msanii kaweka jina tu wakati anafahamika kuwa ni mwana ccm tangu kitambo sana ,,,,, go on magufuri tuko pamoja kutokomeza mafisadi hasa tukianza na wale mapapa siku ukiamua rais wangu
Utasubiri sana aamue mkuu, lakini haitotokea. Wajanja akina jk washamuweka mfukoni. Yeye ataendelea kudili na wanafunzi wa certificate tu
 
Point taken. Kada wa CHADEMA siku zote katika ubora wako japo wenzako hawakupendi. Huo ndo uhalisia
Naona mmejazana kwenye kachumba kenu hapo Lumumba mnapeana ukada wa vyama vingine na kufanya propaganda za kitoto kabisa
lumumba.jpg
 
Ukawa muendelee na msimamo huo huo hadi solution ipatikane, mkirudi nyuma Ma-CCM yatawadharau na kuwaona ni watu wa Ku-beep tu na kuachia.

MKAZE HIVYO HIVYO MPAKA WAO WACHOKE.
 
Back
Top Bottom