MkuuMtarajiwa
Member
- Sep 7, 2010
- 57
- 10
Ni siku kazaa sasa zimepita tangu Meya wa Jiji la Dar es Salaam kutoa kauli ya kuhudhi, kudhalilisha, kutukana na isiyo vumilika kwa wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam. Sito thubutu kuiandika hapa jamvini ila nimejiuliza kama wabunge wetu tuliowachagua kwa njia ya kura wanaambiwa wanafikiri kwa kutumia .........Je wapigakura wao kabla ya kwenda kupiga kura walikuwa wanafikiri kwa kutumia nini??? na sasa baada ya kuwaweka madarakani wanafikiri kwa kutumia nini?? Lakini ni lini atajifunza kuwa kumtukana kiongozi ni kuwatukana wale anaowaongoza?
Kwa kitendo cha kuwadhalilisha wabunge wetu wa mkoa wa Dar es Salaam, nafikiri ni muda muafaka kwa wananchi kumwambia wazi wazi kuwa ametudhalilisha sisi wakazi wa Dar, na wapiga kura wa hawa wabunge. Amepoteza uhalali wa kukalia kiti cha Umeya katika jiji na mkoa alioudhalilisha. Kuwa kiongozi si madaraka na dhihaka, ni dhamana ni utumishi, ni wito, ni USHUHUDA wa Maisha yako na si maneno yako.
Kujibizana na wabunge kwa staili ya ukimwaga mboga mimi nitamwaga ugali tuliyoishuudia ni kielelezo tosha cha uongozi usiostahili kuwepo sehemu yoyote ile nchini, sembuse Dar, no i mean Kata ya kivukoni, oooohhhhh no (hivi ukulu ipo kata gani vile) na wapiga kura wa kata ya kivukoni mbunge wao ni nani vile, si ndiye yule Mh. Zungu. Aaaaakkkhhhhh naomba kuuliza, hivi mtu kama anaishi IKULU pale magogoni, Diwani wake ni nani vile na mbunge wake ni yupi???? soooorrrrryyyyy nimegafirika, Tafadhali FIKIRI na CHukua Hatua.
Kwa kitendo cha kuwadhalilisha wabunge wetu wa mkoa wa Dar es Salaam, nafikiri ni muda muafaka kwa wananchi kumwambia wazi wazi kuwa ametudhalilisha sisi wakazi wa Dar, na wapiga kura wa hawa wabunge. Amepoteza uhalali wa kukalia kiti cha Umeya katika jiji na mkoa alioudhalilisha. Kuwa kiongozi si madaraka na dhihaka, ni dhamana ni utumishi, ni wito, ni USHUHUDA wa Maisha yako na si maneno yako.
Kujibizana na wabunge kwa staili ya ukimwaga mboga mimi nitamwaga ugali tuliyoishuudia ni kielelezo tosha cha uongozi usiostahili kuwepo sehemu yoyote ile nchini, sembuse Dar, no i mean Kata ya kivukoni, oooohhhhh no (hivi ukulu ipo kata gani vile) na wapiga kura wa kata ya kivukoni mbunge wao ni nani vile, si ndiye yule Mh. Zungu. Aaaaakkkhhhhh naomba kuuliza, hivi mtu kama anaishi IKULU pale magogoni, Diwani wake ni nani vile na mbunge wake ni yupi???? soooorrrrryyyyy nimegafirika, Tafadhali FIKIRI na CHukua Hatua.