NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,853
Kumbuka pambano la Mandonga halikuwa pambano kuu, lilikuwa ni pambano la ufunguzi tu hivyo pesa aliyopewa inaweza isifikie hata iliyotajwa/
Pambano lilijaza nyomi ya wakenya zaidi ya elfu 6 waliojaza ukumbi wa KICC jijini Nairobi.
Kwa wale ambao hawakuweza kufika hasa wa Mombasa, Nakuru, Kisumu, n.k iliwabidi wanunue tiketi za kuchekia pambano online.
Mgao wa mabondia wengine ukiwachanganya wote huenda hata haukufikia milioni 10 maana mchezo huu nchini Kenya hauna Mashabiki wengi
Ukiachana na Mandomga, Wapiganaji wengine watakuwa wamekula laki 3 hadi 8 na wenye afadhali wamelamba milioni 1.5 hasa wa pambano kuu ... Mchezo wa ngumi kwa Kenya bado ni mchanga mashabiki wachache hivyo malipo ni kiduchu
Kama Mandonga kalipwa milioni 5 kiukweli anasindikiza kitu anachopigania kifaidiwe na wengine, ni heri atafutiwe meneja