Kwa herini JF, mod ondoa jina langu kwa huzuni kubwa!

Mwikimbi

JF-Expert Member
Mar 8, 2008
1,762
825
Nimekuwa senior expert member wa jf kwa miaka mitatu. Hata ivo sina budi nkuwaaga kwa sababu zifuatazo

mnamo wiki mbili zilizopita niliweka bandio hapa kuhusu ahadi za jk kufikia trilioni 90, nilikuwa nimefanya utafiti wa kina kwa muda wa wiki3, niliweka bandiko kwa kuwa nilitegemea kupata mawzo yenu jf the great thinkers, hata hivo bandiki langu lilipotea baada ya posts kama tatu hivi, cha kushangaza ni kuwa kesho yake bandiko lile lilitokea gazeti laq mtanzania daima.


Jana nimeweka bandiko lingine kuhusu jinsi watanznia wanavyojadili kuhusu jinsia ya ana makinda badala ya mustakabali wa taifa letu nayo imepotea.

Leo nikaandika rasmi kulalamika kwa mods, na thread yenyewe imepotea tena haionekani.

Tafadhali mods naomba aidha uifungie au unipe maelekezo kuhusu makosa yangu, aidha kama hali ni hii ni kuwa hapa jf kuna mafioso au mafiadi walikubuhu na kama hali ni hii sina ujanja bali kuwaaga. Bado mimi ni mkweli kwa taifa langu, naomba mwanakijiji na wengine minisaidie

mwikimbi

mbeya

leo
 
Wewe tambaa tu wala huna haja ya kuaga. Wengi wetu tunajua kuwa ma mods wana "suck".
 
mwaya,labda nuksi tu ila naamini watakujibu na hata ukiondoka naamini utarudi maana hapa ndo home
 
Nenda tuu mwahego inaonekana wamekuchoka sasa na wewe unangoja kufukuzwa...? chapa yebo bob hukusoma alama za nyakati lol
 
Watu kwa malalamiko siwawezi! Jamani, Mwikimbi na uzoefu wako hapa JF umeshindwa kutumia SEARCH button kuona thread unayoilalamikia ipo wapi mkuu? Watu mbona mnatawaliwa na hasira these days? Uchaguzi huu umewachanganya sana wakuu? Mbona mambo bado?

Mimi nime-search kwa keyword "AHADI" na nikachagua zije topic titles tu nikapata hiki:

Ahadi za Kikwete zafikia Trillion tisini (90 trillion tsh)

Sasa unataka kusema mods wamekuchakachua mkuu? Be fair!

Wengine mnaweza kufuatilia posts za mlalamikaji (kwa ushahidi) via: Search Results - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Mtu ukikuta huoni posts zako tufahamishe tukusaidie wakuu, halafu thread kama hii imeanzishwa jukwaa la siasa, ikihamishwa najua pia ni UONEVU MKUBWA ndani ya JF!
 
Mwikimbi, your yesterday's post was merged with the one disussing the profile of Speaker Makinda. You didn't have to start another thread on the topic already being discussed and was still "live". Thanks.
 
Ndugu yangu mbona makeke namna hiyo? Binafsi nimekuwapo hapa kwa zaidi ya miaka minne sijawahi kuona post inapotea bila sababu. Na hata ikipotea huwa ama imetunzwa mahala au imeunganishwa na nyingine. Inapolazimika kuifuta kabisa huwa mod anatoa taarifa kwa mwandishi kuwa post imekwenda nje ya mipaka inaondolewa. Kama hukuarifiwa kuwa post yako inaondolewa ni wazi haikufutwa, Jitahidi ufanye search nzuri tu kwa kutumia keyword zinazotosheleza.

Na ukitaka kuondoka, basi huna haja ya kufungua thread za kujaza database bure tu, wewe ondoka kimya kimya kama wafanyavyo wengine wengi kama akina Brazameni.
 
Sasa kama kunatokea kuamishwa au kuunganishwa kwa post, kwanini wahusika hawafahamishwi!?
 
Sasa kama kunatokea kuamishwa au kuunganishwa kwa post, kwanini wahusika hawafahamishwi!?
Mara nyingi zinakuwa zinajieleza mkuu, mfano:

trashed.jpg

merged.jpg
 
Mwikimbi, your yesterday's post was merged with the one disussing the profile of Speaker Makinda. You didn't have to start another thread on the topic already being discussed and was still "live". Thanks.

Kumbe Silencer bado upo? Daaah!!!
 
Nami nakumbuka wakati MJ kafariki nilichonga shairi moja matata sana kumhusu nikaweka na picha yake flani. Baada ya muda sikuliona tena! Nilihoji sana ila sikupata reply HATA MOJA! toka kwa MODS. Niliboreka mno sema tu niliuchuna
 
Nimekuwa senior expert member wa jf kwa miaka mitatu. Hata ivo sina budi nkuwaaga kwa sababu zifuatazo

mnamo wiki mbili zilizopita niliweka bandio hapa kuhusu ahadi za jk kufikia trilioni 90, nilikuwa nimefanya utafiti wa kina kwa muda wa wiki3, niliweka bandiko kwa kuwa nilitegemea kupata mawzo yenu jf the great thinkers, hata hivo bandiki langu lilipotea baada ya posts kama tatu hivi, cha kushangaza ni kuwa kesho yake bandiko lile lilitokea gazeti laq mtanzania daima.


Jana nimeweka bandiko lingine kuhusu jinsi watanznia wanavyojadili kuhusu jinsia ya ana makinda badala ya mustakabali wa taifa letu nayo imepotea.

Leo nikaandika rasmi kulalamika kwa mods, na thread yenyewe imepotea tena haionekani.

Tafadhali mods naomba aidha uifungie au unipe maelekezo kuhusu makosa yangu, aidha kama hali ni hii ni kuwa hapa jf kuna mafioso au mafiadi walikubuhu na kama hali ni hii sina ujanja bali kuwaaga. Bado mimi ni mkweli kwa taifa langu, naomba mwanakijiji na wengine minisaidie

mwikimbi

mbeya

leo

umechemsha mkuu... hiyo analysis nimeiona kwenye forums na blogs and e-group zaidi ya kumi, sasa sijui na wao uliwatumia au vipi!!! Nakushauri ukituma uweke copyright na uhusidhe lawyers kama hutaki kuwa copied

Pia ukirudi piga hodi kwa vigelegele, kama ulivyoaga kwa huzuni
 
unavyoaga unaonekana sitaki nataka we chapa lapa kama nakuona vile unaenda huku shingo inakuuma kwa kuangalia nyuma kama kuna anayekuita urudi
 
pole rafiki ila uvumilivu unahitajika popote ktk maisha.usiondoke vumilia tulijenge taifa letu linalochechemea!
 
Hata ukiondoka bwana Mwakimbi huko Mbeya mnakazi muhimu ya kuimalisha Chadema!! Slaa kisha wapandia mbegu zimeota sasa ni juu yenu wasokile mpalilie ili mpate mavuno mengi 2015!! Mkipalilia vizuri hata Rungwe mnaweza kuchukua kwani wabunge wao watakuwa wamechoka ile mbaya!!
 
Mkuu usiondoke bado tunakuhitaji, kero zipo kila mahali,, cha muhimu punguza jazba wakati wa kukabiliana nazo.. Una uhakika kuwa hutaimiss JF lakini?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom