Kwa heri Nkurunziza, tutakukumbuka daima

Mohamed Ismail

JF-Expert Member
Mar 16, 2014
214
229
Baniani Mbaya, Kiatu chake Dawa
_______________________

Watu wengi wamekuwa wakimzungumzia Pierre Nkurunzinza kwa namna moja pekee ya uwi (ubaya) ambao kila mmoja anao tunapishana viwango tu. Lakini ukimtumpia jicho la tija hususani kwa Burundi na Tanzania; Pierre alikuwa ana tija.

Mosi, aliifanya Burundi kuwa nchi inayoweza kutawalika kutoka kwenye tawala za kibabe na kivita na walau kuwa taifa ustaarabu wa kiwango chake. Ndani ya uongozi wa Nkurunzinza, Burundi kwa mara ya kwanza ilikuwa na uwezo wa kutoa kikosi cha askari (wanajeshi) kwenda kulinda amani. Kwa nchi iliyokuwa ina uchovu wa vita vya wenyewe kwa wenyewe kuweza kutoa kikosi cha kulinda amani kwenda nchi nyingine si jambo dogo (watu wa ulinzi wanaelewa zaidi). Nkurunzinza aliirudisha Burundi katika hali ya kuwa taifa na alikuwa mzalendo kindakindaki wa nchi yake. Nchi iliyokuwa haina Ikulu ikawa nayo (kwa usaidizi wa waChina), kukawa na ujenzi wa miundombinu na kupungua kwa wakimbizi wanaoikimbia nchi yao.

Pili, kwa Tanzania, kutengemaa kwa Burundi kulikuwa ni afua kwa mikoa ya mipakani. Mikoa ya Kigoma na Kagera ilikuwa maskani ya wakimbizi wa kiRundi waliokuwa sehemu ya chanzo cha uharibifu wa mazingira, gharama za kuwatunza na ujangili uliokuwa unahatarisha usalama wa mikoa hiyo.

Ndani ya Burundi ya Nkurunzinza, malaki ya raia wa Burundi waliokuwa wakimbizi nchini Tanzania waliweza kurudi nchini mwao tangu kipindi cha Rais Kikwete hadi wakati huu wa Rais Magufuli. Tuliona Rais Kikwete alivyotumia "busara" kuhakikisha Nkurunzinza anarudi Burundi baada ya mapinduzi dhidi yake yaliyofanyika wakati wa Mkutano wa EAC wa mwaka 2015 nchini Tanzania. Vilevile, tumeona namna Rais Magufuli na Nkurunzinza walivyokutana Ngara mwaka 2017 na kufanya mikataba yenye lengo la kuhimiza waRundi warudi kwao kuijenga nchi yao.

Miaka kama miwili iliyopita tuliona Rais Museveni na Rais Magufuli wakiiambia Rwanda iache kuingilia mambo ya ndani ya Burundi. Kauli hiyo ilikuwa inaonesha namna Afrika Mashariki ilivyokuwa inauona umuhimu wa utulivu wa Burundi kwa eneo zima la Maziwa Makuu.

Leo hii si ajabu kuona Tanzania na Kenya kurusha bendera nusu mlingoti kwa ajili ya Rais Pierre Nkurunzinza. Chambilecho wahenga: baniani mbaya kiatu chake dawa.

Tangulia kamanda.

Gervas A. Kasiga (Rutakirwa)
Idodomiya
13-06-2020
 
Hilo jamaa kifo chake nimekifurahia sana kwa mambo mawili.
1. Kinatuma ujumbe kwa wadharau Corona wote na kutoa onyo kali sana kwao kuwa "Usimjaribu bwana Mungu wako"

2. Aliyekufa ni Dikteta. Sina upendo wowote na madikteta hivyo acha niendelee kusherehekea hizi siku tatu tulizopewa!

Wacha niendelee kula throat sanitizer huku nikisubiri muda muafaka nifyatue TANZIA ya uhakika hapa.
 
Nkurunzinza kafanya Makubwa sana Burundi ambayo kina Major Pierre Buyoya hawakuweza

Kaweza kuituliza Nchi kwa Miaka 15 ya Urais wske japokuwa kuna matukio ya hapa na pale

Kaimarisha uhusiano mwema kwa muda wote na Tanzania

Kajitahidi sana kupunguza hisia za Ukabila ndani ya Burundi

Huwezi kupewa Taifa kama Burundi lililotoka kwny Umwagaji Damu wa Nusu Karne halafu utawale kwa misingi yote ya kidemokrasia na uhuru kama vile US au Ghana.

Hata hayo Mataifa leo tunayosifia kwa demokrasia na Uhuru yalianzia inapopita Burundi sasa

Hata Tanzania walipita kina Nyerere na kina Karume na yapo ya kimafia mengi walifanya kuifanya Tanzania kuwa hapa ilipo
 
Sijawahi kuwa na huruma na madikteta. Halafu naona unawapenda sana madikteta. Uzi wako unaonesha ma dictator wawili
 
MUNGU haoni ma traitors Kama lisu mbowe zito akawachukua? Wamekaa kuwatumikia mabeberu tu hawana faida yeyote
 
Yaani Muuwaji na Mtesaji Watu nae huwa anatakiwa Kukumbukwa na kuanza Kupambwa hivi kuwa alikuwa ni Kiongozi mzuri sana nchini Burundi?
 
Nampongeza Nkurunzinza R.I.P,Kagame,Museven na viongozi woote kwa kuwanyoosha wajinga wajinga na vizabizabina wenye tabia za kutaka kuvuruga amani ya mataifa yao.
 
Back
Top Bottom