Kwa haya tuna kila sababu ya kuipongeza CCM

zema21

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
619
251
Hivi kwanini nisiwapongeze CCM ikiwa mwenyekiti wenu anakiri hadharani chama chenu kinategemea jeshi la polisi kukandamiza haki za wengine?
angalia rushwa ndani ya chama chako mbona mmeshindwa kuidhibiti, wote mmeishia kulia lia tu toka kwa wanachama mpaka mwenyekiti wenu?
Serikali gani inayoshabikia utoroshwaji wa fedha kwenda nje ya nchi mkiambiwa zirudi mnahaha wote mnapata kigugumizi? mnakuja na mbinu mbali mbali za kutetea toka alipojaribu AG kuzima mjadala bungeni akashindwa sasa mnamtumia waziri!!!!? kumbe nyie ndo wamiliki wa hizo fedha kwanza tunakosea sana tukiwaomba mfanye uchunguzi manake nikuwaambia mjichunguze wenyewe.
Serikali gani inayoshabikia kuleta mabepari wakati babu zetu akina Mkwawa pamoja na kutokuwa na elimu wala utaalamu wowote walihaha kuwafukuza? eti nyie mnawaleta mkisingizia ni wawekezaji,kwani watanzania wenyewe na elimu zetu hatuwezi kufanya hizo kazi wanazofanya hao mabepari mnaoenda kila siku kuwachukua ulaya na kwinginepo mkiwaita wawekiezaji?
Mi nilidhani elimu tunayoipata inatusaidia kumbe hamna lolote, kina mkwawa wakalipambana mno kuwang'oa wazungu bila hata kuwa na silaha yoyote ya kisasa!. Mwishoni nyerere akafanikiwa 9[SUP]th[/SUP] December . Akaona haitoshi akaja na azimio la Arusha. Leo sisi tupo kama tumechanganyikiwa kila penye ardhi nzuri, rasilimali watanzania wanafukuzwa kesho yake jamaa anapanda ndege kwenda kuwaleta wazungu.
Mnaishia kujisifu mmeunganisha mtandao wa barabara kwa nchi nzima.. hivi kama watu tunalipa kodi hiyo ni haki yetu kabisa hamna lolote la kujisifu hapo..
Ardhi yetu yote mnauza kila kukicha, rasilimali nyingine kama madini kila siku zinauzwa, mnaacha mandege ya kijeshi toka nchi nyingine yanatua bongo kuja kuchukua twiga wetu na kuwasafirisha .................. Nani atawapenda?
ukiachilia mbali maisha magumu mliyotusababishia.. watu tunashindwa kumudu gharama za maisha...............
vijana hamuwajali kabisa! graduate wapo utitiri wanazunguka na bahasha mtaani kila kukicha wakiwa na nyuso za kukata tamaa.. wala hawana matumaini kabisa.
Ile kashfa ya watu kukusanywa mtaani baada ya kutoa fedha zao kisha (toka laki 2 mpaka laki 8) kupelekwa mpaka CCP moshi wanaanza mafunzo ya upolisi baada ya siku tatu wanaofukuzwa eti kwamba majina yao hayapo kwenye database ndo malengo yenu kuwatapeli vijana wetu kwa tatizo la ajira mnalolipalilia nyinyi.

 
Hivi kwanini nisiwapongeze CCM ikiwa mwenyekiti wenu anakiri hadharani chama chenu kinategemea jeshi la polisi kukandamiza haki za wengine?
angalia rushwa ndani ya chama chako mbona mmeshindwa kuidhibiti, wote mmeishia kulia lia tu toka kwa wanachama mpaka mwenyekiti wenu?
Serikali gani inayoshabikia utoroshwaji wa fedha kwenda nje ya nchi mkiambiwa zirudi mnahaha wote mnapata kigugumizi? mnakuja na mbinu mbali mbali za kutetea toka alipojaribu AG kuzima mjadala bungeni akashindwa sasa mnamtumia waziri!!!!? kumbe nyie ndo wamiliki wa hizo fedha kwanza tunakosea sana tukiwaomba mfanye uchunguzi manake nikuwaambia mjichunguze wenyewe.
Serikali gani inayoshabikia kuleta mabepari wakati babu zetu akina Mkwawa pamoja na kutokuwa na elimu wala utaalamu wowote walihaha kuwafukuza? eti nyie mnawaleta mkisingizia ni wawekezaji,kwani watanzania wenyewe na elimu zetu hatuwezi kufanya hizo kazi wanazofanya hao mabepari mnaoenda kila siku kuwachukua ulaya na kwinginepo mkiwaita wawekiezaji?
Mi nilidhani elimu tunayoipata inatusaidia kumbe hamna lolote, kina mkwawa wakalipambana mno kuwang'oa wazungu bila hata kuwa na silaha yoyote ya kisasa!. Mwishoni nyerere akafanikiwa 9[SUP]th[/SUP] December . Akaona haitoshi akaja na azimio la Arusha. Leo sisi tupo kama tumechanganyikiwa kila penye ardhi nzuri, rasilimali watanzania wanafukuzwa kesho yake jamaa anapanda ndege kwenda kuwaleta wazungu.
Mnaishia kujisifu mmeunganisha mtandao wa barabara kwa nchi nzima.. hivi kama watu tunalipa kodi hiyo ni haki yetu kabisa hamna lolote la kujisifu hapo..
Ardhi yetu yote mnauza kila kukicha, rasilimali nyingine kama madini kila siku zinauzwa, mnaacha mandege ya kijeshi toka nchi nyingine yanatua bongo kuja kuchukua twiga wetu na kuwasafirisha .................. Nani atawapenda?
ukiachilia mbali maisha magumu mliyotusababishia.. watu tunashindwa kumudu gharama za maisha...............
vijana hamuwajali kabisa! graduate wapo utitiri wanazunguka na bahasha mtaani kila kukicha wakiwa na nyuso za kukata tamaa.. wala hawana matumaini kabisa.
Ile kashfa ya watu kukusanywa mtaani baada ya kutoa fedha zao kisha (toka laki 2 mpaka laki 8) kupelekwa mpaka CCP moshi wanaanza mafunzo ya upolisi baada ya siku tatu wanaofukuzwa eti kwamba majina yao hayapo kwenye database ndo malengo yenu kuwatapeli vijana wetu kwa tatizo la ajira mnalolipalilia nyinyi.

Baada ya kulalamika sana inatakiwa umalize na ushauri,we unadhani nini kifanyike?Au na wewe utasema hujui nini kifanyike?
 
Baada ya kulalamika sana inatakiwa umalize na ushauri,we unadhani nini kifanyike?Au na wewe utasema hujui nini kifanyike?
hakuna cha kushauri zaidi ya kuhakikisha mnaichia serikali 2015 kupitia kura ya kila mtanzania
 
Hawa ni akina Chifu Mangungo! Historia itaendelea kuwahukumu wao na vizazi vyao baada yao!!!
 
Back
Top Bottom