Kwa hali ya jinsi hii: Maendeleo ya kijamii na kiuchumi itabakia kuwa ndoto

nsimba

JF-Expert Member
Oct 7, 2010
782
55
Main%20E.jpg


Standard Three pupils of Chinyarira Primary School in Nanyumbu District, Mtwara Region, while away the time outside their classroom, as captured by our correspondent yesterday. (Photo:Correspondent Happy Severine)
 
hapa ndio tunashughulikia kilimo kwanza Elimu baadaye. Hivyo hata mwalimu alikuwa kaenda shamba lake la mfano.
 
Tukisema nchi yetu haihitaji viongozi kama kikwete wanadhani tunamchukia,kama hajui sababu za uwepo wa hali hii unadhani atawasaidiaje watanzania hawa?
 
haya ndio matatizo ya kuchanganya siasa na utaalam,mtoto wamkulima mimi huwa namuonaga kama kilaza tu.alipo kuja na sera yakilimo kwanza alishauriana na nani?sidhani kama ali consult kwa watu wamambo ya project planing.,au aliota usiku asubuhi ndio ikawa gia yakuja kuwadanganya nayo wadanganyika.hapa kitu walicho patia hawa wanafunzi ni uniform tu,tena kwakua ni dili la mwalimu mkuu na afisa elimu wa kijiji au wilaya,na huko ndiko sisiemu wanakopata wanachama wengi kupita maelezo,kama hiyo ndio darasa elimu inayotolewa itafananaje!?huo upumbavu wanaofanya huko kusini hawawezi fanya pande za kama kaskazini, na hiyo dhambi itawatafuna tu,kama siowao basi vizazi vyao.huko nafikiri hakuna mbunge wala wakuu wa serekali that y kunakua na madudu namna hiyo,mwenzao kakimbillia kaskazini kajenga lushoto kasri ambayo hata ulaya hakuna.jenga nyumbani kwanza nje baadae,ubinafsi wa sisiemu huo,kwani mkapa hakuimarisha mambo huko?hao hata tusiwalaumu tukiwambia wahamie watasema hawatujui kwani hata redio huko utakuta hazishiki.
 
Kweli mkuu maendeleo hayaji n'go! Nyerere hakuwa mjinga alivyoona kuwa nchi hii inahitaji viwanda akaanzisha viwanda vidogo vidogo na kutaifisha viwanda vingi na kuanzisha vingi tu! Elimu bure mpaka chuo kikuu na kazi unapangiwa ukimaliza. Sasa hivi vyote ndoto. Mamluki wameuza viwanda yyote na bado kidogo watanganganyika tutakuwa wageni katika nchi yetu. Tusubiri tu!!!!! Nchi inaendelea kwa mapinduzi ya viwanda (Industrial Revolution" sio kilimo!! Nchi zote ulimwenguni zimeendelea kwa sababu ya viwanda.
 
unanitia machungu,serekali haina kiwanda hatakimoja,! aibu tupu.wameuza vyote na vingine wameshiriki kuviua.kiongozi wa nchi anasema hajui umasikini wa nchi yake hajui unatokana na nini,je atajua vipi namna ya kumaliza hilo tatizo?na msaidizi wake nae kaja na kauli hiyohiyo kua hajui umasikini wa nchi yake unatokana au unasababishwa na nini,hivi hawa watu tuwaeleweje jamani kama mambo yenyewe ndio haya.tusitegemee utatuzi wa hili jambo kutoka kwao kwani wameshasema hawajui na kwa tafsiri ingine ni kwamba kutatua umaskini kwa nchi wameshindwa.wangekua wastaarabu wange stepdown kuwapa nafasi wanaowezakufanya hivyo.
 
Back
Top Bottom