Kwa hali ya ajira ilivyo sasa, Serikali fikirieni upya kuhusu fao la kujitoa kwenye ajira

Paploman

JF-Expert Member
Apr 13, 2019
1,720
3,237
Kuna kundi kubwa sana la vijana wasiokuwa na ajira ama wako kwenye ajira zisizo rasmi na ajira za ujira mdogo. Hawa wote wanategemea siku moja kupata kazi zenye maslahi ya kuridhisha.

Kibaya zaidi kuna watu wameajiriwa serikalini na sekta binafsi lakini sio wote walio na malengo ya kustaafu wakiwa makazini.

Wapo wengi wenye malengo ya kuacha kazi ili wakaendeleze au kuanzisha miradi na biashara za ndoto yao, Changamoto ni sera zenu za mafao (fedha) ambazo ni jasho halali za hawa watumishi sio rafiki, jambo ambalo mtu akifikiria inabidi asitishe mpango wake na kuendelea kuwa kazini.

Hakuna ulazima wa kuzuia kumpa mtu pesa zake kisa ameacha kazi mwenyewe kwa maelezo kwamba atapewa akifikia umri wa miaka 55,, hizo pesa zitakuwa na faida gani tena katika maendeleo ya huyo mtu kwa umri huo? Kijana anaacha kazi ana miaka 35 akiwa ameitumikia hiyo kazi labda kwa miaka 12, asubiri mafao yake kwa miaka 20 zaidi?.Mliwaza nini hapa

Rudisheni fao la kujitoa, Vijana waliojichanga mitaji yao wakaendeleze biashara za ndoto zao na nyie kama serikali mpate nafasi nyingi za kuajiri wapya hata huko sekta binafsi kuna watu wanashindwa kuacha kazi kwa kuhofia kutopata pesa walizozitegemea kuendesha maisha yao nje ya ajira kwenye hii mifuko ya kijamii.

Viongozi wetu sijui mnawaza nini, kwa hali ilivo sasa ya changamoto ya ajira hizi sera zenu zingetakiwa ziwe rafiki kusaidia vijana kujiajiri zaidi ya kulazimisha walioko kwenye ajira wabaki hukohuko mpaka umri wa kustaafu.

Rudusheni hili fao, tuwapishe wengine waajiriwe nao watafute mitaji. Mnahimiza tujiajiri huku mnakatalia mitaji yetu ambayo ni pesa zetu halali, mko serious na mnachokihubiri kweli?
 
Wana kauli yao moja hawa mbuzi wa hii mifuko ya jamii, " Kama umeamua kuacha kazi mwenyewe huna shida na pesa wala kazi, subiri ukifika 55yrs tutakupa"... Boya kabisa Qma.mae zao.

Pesa zangu wanazipangia masharti wao namna ya kunipa, hawa watu kuna siku yao nitamchana mtu sime pale ofisini kwao
 
Wana kauli yao moja hawa mbuzi wa hii mifuko ya jamii, " Kama umeamua kuacha kazi mwenyewe huna shida na pesa wala kazi, subiri ukifika 55yrs"... Boya kabisa Qma.mae zao.

Pesa zangu wanazipangia masharti wao namna ya kunipa, hawa watu kuna siku yao nitamchana mtu sime pale ofisini kwao
Sera za hovyo kabisa, mbona wakubwa wao mafao yao hayana longolongo.

Yaani wanatulazimisha tufie makazini.
 
Free Bilionea shilla
Bring back Ben Saanane still Alive
Who tried to assassinated Hon. Lissu

Who killed Mawazo

8Years rot in jali our religious leaders ,For false accusations ....ooh Jpm must go.
Where is your brain???
 
Pengine kuongeza fursa za ajira, yafuatayo yafanyike:

1. Kila mtu mwenye umri wa miaka 18 <=55, iwe ni takwa la kisheria kujiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii au kujiwekea Akaunti Binafsi ya Kustaafu (IRA).
2. Kama ambavyo yapo mabenki binafsi yanayodhibitiwa na BoT, basi kuwe na Mifuko Binafsi ya hifadhi ya jamii.
3. Kwa waliochangia mifuko ya hifadhi ya jamii iliyoko, wapewe fursa ya kuchagua "kuchukua kiinua mgongo" kwa wakati wowote, bali pensheni watapofikia umri wa kustaafu.
 
Yaani umeongea sawa kabisa,binafsi ni muhanga wa hili,nimefanya kazi kwenye sekta binafsi ya mabeberu si chini ya miaka mitano,Kwanza mnalipwa pesa ndogo
 
Yaani umeongea sawa kabisa,binafsi ni muhanga wa hili,nimefanya kazi kwenye sekta binafsi ya mabeberu si chini ya miaka mitano,Kwanza mnalipwa pesa ndogo
Sasa Hawa watetezi wa wanyonge hawataki kutoa pesa watu wakafanye vibiashara..mpaka 55yrs hahaha
 
Tatizo Kubwa Lipo, Vijana Hawana Ajira
Walio Na Ajira Nyuma Yao Kuna Ndugu, Jamaa, Marafiki, Wapendwa Hawana Kitu
Ukipata Chochote Ukianza Kumwaga Unabaki Mtupu. Jibu Ni Kuwa Hata Wenye Ajira Ni Kama Hawana.


Baadhi Umri Umewatupa Huku Mambo Ya Lazima Kuyafanya Kama Kuwa Na Family Yapo Vile Vile Yakiwahitaji
 
Tatizo Kubwa Lipo, Vijana Hawana Ajira
Walio Na Ajira Nyuma Yao Kuna Ndugu, Jamaa, Marafiki, Wapendwa Hawana Kitu
Ukipata Chochote Ukianza Kumwaga Unabaki Mtupu. Jibu Ni Kuwa Hata Wenye Ajira Ni Kama Hawana.


Baadhi Umri Umewatupa Huku Mambo Ya Lazima Kuyafanya Kama Kuwa Na Family Yapo Vile Vile Yakiwahitaji
Tena ukiwa na hiyo ajira Kila ndugu tumainai like kwako ukithubutu kusema huna unaonekana una roho mbaya wangejua pesa unayopata hata wewe na familia yako haikutoshi...mishahara haiongezeki Bali majukumu yanaongezeka Kila uchao
 
Kuna kundi kubwa sana la vijana wasiokuwa na ajira ama wako kwenye ajira zisizo rasmi na ajira za ujira mdogo. Hawa wote wanategemea siku moja kupata kazi zenye maslahi ya kuridhisha.

Kibaya zaidi kuna watu wameajiriwa serikalini na sekta binafsi lakini sio wote walio na malengo ya kustaafu wakiwa makazini.

Wapo wengi wenye malengo ya kuacha kazi ili wakaendeleze au kuanzisha miradi na biashara za ndoto yao, Changamoto ni sera zenu za mafao (fedha) ambazo ni jasho halali za hawa watumishi sio rafiki, jambo ambalo mtu akifikiria inabidi asitishe mpango wake na kuendelea kuwa kazini.

Hakuna ulazima wa kuzuia kumpa mtu pesa zake kisa ameacha kazi mwenyewe kwa maelezo kwamba atapewa akifikia umri wa miaka 55,, hizo pesa zitakuwa na faida gani tena katika maendeleo ya huyo mtu kwa umri huo? Kijana anaacha kazi ana miaka 35 akiwa ameitumikia hiyo kazi labda kwa miaka 12, asubiri mafao yake kwa miaka 20 zaidi?.Mliwaza nini hapa

Rudisheni fao la kujitoa, Vijana waliojichanga mitaji yao wakaendeleze biashara za ndoto zao na nyie kama serikali mpate nafasi nyingi za kuajiri wapya hata huko sekta binafsi kuna watu wanashindwa kuacha kazi kwa kuhofia kutopata pesa walizozitegemea kuendesha maisha yao nje ya ajira kwenye hii mifuko ya kijamii.

Viongozi wetu sijui mnawaza nini, kwa hali ilivo sasa ya changamoto ya ajira hizi sera zenu zingetakiwa ziwe rafiki kusaidia vijana kujiajiri zaidi ya kulazimisha walioko kwenye ajira wabaki hukohuko mpaka umri wa kustaafu.

Rudusheni hili fao, tuwapishe wengine waajiriwe nao watafute mitaji. Mnahimiza tujiajiri huku mnakatalia mitaji yetu ambayo ni pesa zetu halali, mko serious na mnachokihubiri kweli?
kma ume contribute kwa muda wa miezi isiyo chini ya miezi 180 unaeza kujitoa ukapata mafao yako ila kuna penalty utapigwa ya kujitoa koz hizo pesa sio kwamba zinatunzwa bali wanafanya investment ambayo kwa mwanachama wa mfuko husika inakua faida kutokana na investment on return ikileta faida maana yake mnufaika utapata fao la uzeeni kubwa na utakula vizuri 75% ya pension yako kila mwezi.
kwa mwenye kuhitaji kujua zaidi kuhusu mafao unaweza ni pm by nssf consaltant
 
Wana kauli yao moja hawa mbuzi wa hii mifuko ya jamii, " Kama umeamua kuacha kazi mwenyewe huna shida na pesa wala kazi, subiri ukifika 55yrs tutakupa"... Boya kabisa Qma.mae zao.

Pesa zangu wanazipangia masharti wao namna ya kunipa, hawa watu kuna siku yao nitamchana mtu sime pale ofisini kwao
Hahaahaaa mkuu kwa kweli hawa watu ni shida sana.
 
Back
Top Bottom