barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Ni wakati sahihi kwa Waziri wa Mambo ya ndani,ndugu Lameck Mwigulu Nchemba kuachia ngazi na kuwaachia wengine nafasi hiyo.
Mauwaji ya Kibiti na Rufiji kwa ujumla wake,na katika mfufululizo usio na woga unaobeba maisha na damu za raia kikatiri,ni ajabu kuona Waziri mwenye dhamana,aliyefunga safari kwenda mpaka Kibiti,akatema nyongo na "mikwara" mingi akiwa bado yupo ofisini.
Kuachia ngazi sio kushindwa,kuachia kiti sio udhaifu,kuwapisha wengine sio dhambi.Ni dhana ya uwajibikaji wa kawaida katika ofisi za umma na jamii ya wastarabu.
Kwa namna Mwigulu alivyowaahidi watu wa Kibiti na Rufiji yote,kwa namna ziara yake alivyopambwa kwa mbwembwe na matamko ya vitisho kwa "wauwaji" ni wazi kuwa kwa sasa Mwigulu alipaswa kuwa na cheo cha ubunge tu na uwaziri awe ameukabidhi kwa aliyemteua ili ijazwe na mtu mwingine.
RPC wa Pwani katumia mbinu zote,lakini amezidiwa,mpaka sasa askari wake kadhaa wanashinda ndani kwa kuogopa kuwafuata ahela wenzao.Hata msafara wa RPC katika miji ya Kibiti na Rufiji unatembea kwa wasiwasi kama mgambo mwenye rungu na sime.RPC na Mwigulu wangekaa pembeni ili kuleta wengine wenye mikakati mipya.
Huu ni mtazamo,ni mtazamo katika kuelekea kupata kisa hasa cha kwa nini ndugu zetu wanatolewa roho kikatiri huko Kibiti.
Hili la dhuluma ya polisi na viongozi wa vijiji kwa wananchi kwa kipindi kirefu,lisiachwe likapita kimyakimya.Dhurma inauma,dhurma hujenga chuki kwa muda mrefu,dhuluma hupandikiza roho ya kisasi isiyo na mwisho.
Beria(barrier) nyingi za mazao ya msituni kama mkaa,kuni na mbao ilikuwa katika maeneo haya.Wananchi wengi wa maeneo haya walitopea katika hali ya kudhurumiwa mali zao na polisi pamoja na viongozi wa kiserikali ambao walikuwa na madaraka ya kufanya hivyo.Wengi waligeuka masikini kwa mitaji yao kupokwa na wengine kuzikimbia familia zao sababu ya mitaji yao kutolewa kama rushwa kwa viongozi wa vijiji,vitongoji na wilaya kwa msaada wa polisi.
Kuanzia maafisa wa misitu,polisi wa barabarani na polisi wa kawaida na viongozi wa vijiji na vitongoji waliokuwa na uwezo wa kuidhinisha vibali vya mazao ya misitu walicheza na dhuluma hii.Ukikutana na mtu wa Kibiti aliye mjini,atakwambia udhulumaji wa aina hii ulisubiri muda tu.Watu walishachoka sana.Hii iwe moja ya "hypothesis" ya kuona kiini cha mgogoro wa Mkuranga,Rufiji na Kibiti.
Watu walishapanga kwa muda mrefu,wakawa hawana mtetezi,wakamua kwa pamoja....Ukiweka Ugoko,Wao wanaweka chuma!!
Mauwaji ya Kibiti na Rufiji kwa ujumla wake,na katika mfufululizo usio na woga unaobeba maisha na damu za raia kikatiri,ni ajabu kuona Waziri mwenye dhamana,aliyefunga safari kwenda mpaka Kibiti,akatema nyongo na "mikwara" mingi akiwa bado yupo ofisini.
Kuachia ngazi sio kushindwa,kuachia kiti sio udhaifu,kuwapisha wengine sio dhambi.Ni dhana ya uwajibikaji wa kawaida katika ofisi za umma na jamii ya wastarabu.
Kwa namna Mwigulu alivyowaahidi watu wa Kibiti na Rufiji yote,kwa namna ziara yake alivyopambwa kwa mbwembwe na matamko ya vitisho kwa "wauwaji" ni wazi kuwa kwa sasa Mwigulu alipaswa kuwa na cheo cha ubunge tu na uwaziri awe ameukabidhi kwa aliyemteua ili ijazwe na mtu mwingine.
RPC wa Pwani katumia mbinu zote,lakini amezidiwa,mpaka sasa askari wake kadhaa wanashinda ndani kwa kuogopa kuwafuata ahela wenzao.Hata msafara wa RPC katika miji ya Kibiti na Rufiji unatembea kwa wasiwasi kama mgambo mwenye rungu na sime.RPC na Mwigulu wangekaa pembeni ili kuleta wengine wenye mikakati mipya.
Huu ni mtazamo,ni mtazamo katika kuelekea kupata kisa hasa cha kwa nini ndugu zetu wanatolewa roho kikatiri huko Kibiti.
Hili la dhuluma ya polisi na viongozi wa vijiji kwa wananchi kwa kipindi kirefu,lisiachwe likapita kimyakimya.Dhurma inauma,dhurma hujenga chuki kwa muda mrefu,dhuluma hupandikiza roho ya kisasi isiyo na mwisho.
Beria(barrier) nyingi za mazao ya msituni kama mkaa,kuni na mbao ilikuwa katika maeneo haya.Wananchi wengi wa maeneo haya walitopea katika hali ya kudhurumiwa mali zao na polisi pamoja na viongozi wa kiserikali ambao walikuwa na madaraka ya kufanya hivyo.Wengi waligeuka masikini kwa mitaji yao kupokwa na wengine kuzikimbia familia zao sababu ya mitaji yao kutolewa kama rushwa kwa viongozi wa vijiji,vitongoji na wilaya kwa msaada wa polisi.
Kuanzia maafisa wa misitu,polisi wa barabarani na polisi wa kawaida na viongozi wa vijiji na vitongoji waliokuwa na uwezo wa kuidhinisha vibali vya mazao ya misitu walicheza na dhuluma hii.Ukikutana na mtu wa Kibiti aliye mjini,atakwambia udhulumaji wa aina hii ulisubiri muda tu.Watu walishachoka sana.Hii iwe moja ya "hypothesis" ya kuona kiini cha mgogoro wa Mkuranga,Rufiji na Kibiti.
Watu walishapanga kwa muda mrefu,wakawa hawana mtetezi,wakamua kwa pamoja....Ukiweka Ugoko,Wao wanaweka chuma!!