Kwa hali hii ya kisiasa CCM mjiandae kisaikolojia kulipoteza jimbo la Segerea na mengine mengi

Bata batani

JF-Expert Member
Nov 11, 2011
3,182
3,547
Kabla sijazungumza naomba nitoe sifa za jimbo la Segerea.

Jimbo la Segerea lina kata 13, CCM hawana kata hata moja.

Jimbo la Segerea lina madiwani 13 na ndio jimbo pekee nchini Tanzania CCM hawana diwani hata mmoja.

Jimbo la Segerea lina mitaa 51, CUF ana mitaa 19, CHADEMA ina 22 na CCM wana mitaa 9 ambayo hadi sasa hawajui kama watabaki nayo

Tunawaomba wapinzani 2020 makosa yale makosa yaliyofanywa na kina Mtatiro na Anatropia ya kugawana kura 2015 yasijirudie tena

Jimbo la Segerea tumeshajiandaa na mageuzi ya 2020
 
Kwanza kwa hali ilivyokuwa 2015 sidhani kama bona kalua atagombea tena maana wakati ule aliokota dodo chini ya muarobaini
Jimbo la Segerea ni jimbo gumu sana nakumbuka enzi za Mahanga pale Buguruni ilibidi atumie akili ya ziada
 
2020 Magu hawezi kushinda urais achilia mbali ccm kushinda segerea.Hatuwezi kuendelea na rais anayeturudisha zama za kale za mawe za vibatari na mishumaa!
 
Hasira za Nini ? Kuna haja gani kuficha majina ? Sisi-M tuliruhusu mfumo wa vyama vingi ili kuuthibitishia ulimwengu kuwa inji yetu ni kiziwi wa demokuurashia. Kwa hiya majimbo mengi injimaamushi ni kuyaweka chini ya upinzani ni kuonyesha kwa vitendo kuwa tunaheshimu maamushi ya watawala wetu. Kwa hiyo yifikapo chaaguzi zijavyo tuhakikishe madiwani wote injini wanatoka upinzani kama watawala watakuwa bado hawajapiga marufuku hadharani upinzani.
 
2020 hamtaamini na macho yenu, chadema watachukua jimbo moja tu la ubunge ambaye ni Mbowe na Act atatoa mbuge mmoja tu Zitto' madiwani wote watakuwa wa ccm
 
Huko Segerea kama kuna Polisi jiandaeni na mazoezi mapema. Maana hao ndio wapiga kura, wengine washiriki tu
 
mwaka 2020 wagombea wote wa upinzani watakamatwa na polis siku moja kabla yakupiga kura na kuswekwa lupango. ccm bila polis hakuna kitu...
 
Kumbuka kipindi kile ulikuwa upepo was EL ila kwa sasa yule Dada anachukua jimbo asubuh sana
 
Back
Top Bottom