Keyboard Warrior
JF-Expert Member
- Aug 5, 2014
- 985
- 2,884
Tukubali tukatae vyama vya upinzani awamu hii vimekuwa all talk and no action.
Wanasiasa na viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani wamekuwa watu wakulalama tu mtandaoni lakini hakuna hatua zozote wanazochukua kutokana na mambo wanayofanyiwa.
Ni kweli usiopingika kuwa katika kipindi hiki vyama vya upinzani vimekuwa vikichezewa rafu za kila aina, lakini hakuna kitu wamefanya, wanasiasa wamebaki kulialia na kulalama mtandaoni... sasa wananchi walalamike, halafu na wanasiasa waliowachagua walalamike tena, sasa nani atamsaidia mwenzake.
Kama vyama vya upinzani vingekuwa serious kweli basi tungeona haya yanafanyika, serikali ilipopiga marufuku mikutano ya siasa ambayo ni kinyume kabisa na katiba, tungeona hata vyama vya upinzani vikifungua kesi ya katiba kupiga hilo... lakini wapi, hakuna aliefanya hivyo.
Kwenye uchaguzi mdogo wa kata ulioisha hizi karibuni, vyama vya upinzani vimefanyiwa kila aina ya hujuma.. lakini mpaka sasa hatujasikia hata chama kimoja cha upinzani kikikata shauri mahakamani kupinga matokeo.
Tukubali tukatae, mahakamani ndo sehemu pekee vyama vya upinzani vinaweza vikawa na chance ya kupata haki zao. Kwasababu tumesikia mara kadhaa wapinzani wakishinda kesi za ubunge na udiwani mahakamani. So they have a chance there, lakini kama wakitegemea huruma za chama tawala watalia na kusaga meno.
Pia ni dhahiri bila mabadiliko ya kifumo na kisheria kwenye masuala ya uchaguzi, itakuwa ni ngumu kwa vyama vya upinzani kushinda au kutangazwa washindi kwenye chaguzi mbalimbali, lakini pamoja na malalamiko hayo, bado hakuna hata mwanasiasa mmoja wa upinzani aliethubutu kupeleka muswada binafsi bungeni, ili kuchochea kupatikana kwa tume na mfumo huru wa uchaguzi. Hata kama the odds zitakuwa against them, lakini hata kujaribu tu. Hakuna.
Sio siri CCM imechokwa ila vyama vya upinzani vina-disappoint kwa kutochukua hatua zozote na kuishia kulalamika tu kila siku. Inabidi vizinduke na kuanza kuchukua hatua mbalimbali za kisheria na sio kila siku kuitisha press conference tu na kutoa matamko halafu basi.
Wanasema insanity is doing the same thing and expecting different results. So its obvious approach ya sasa hivi ya vyama vya upinzani havifanyi kazi,kwa hiyo wajaribu njia nyingine.
Tunataka kusikia kesi mbalimbali za kikatiba na kisheria kupinga mambo yanayofanywa na serikali ya awamu hii, na hata kupeleka miswada bungeni kurekebisha kasoro za kimfumo na kisheria. Hata kama it wont work out ila wawe na uthubutu hata wakujaribu kufanya hayo. Hicho ndo wananchi wanataka kuona.
Wanasiasa na viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani wamekuwa watu wakulalama tu mtandaoni lakini hakuna hatua zozote wanazochukua kutokana na mambo wanayofanyiwa.
Ni kweli usiopingika kuwa katika kipindi hiki vyama vya upinzani vimekuwa vikichezewa rafu za kila aina, lakini hakuna kitu wamefanya, wanasiasa wamebaki kulialia na kulalama mtandaoni... sasa wananchi walalamike, halafu na wanasiasa waliowachagua walalamike tena, sasa nani atamsaidia mwenzake.
Kama vyama vya upinzani vingekuwa serious kweli basi tungeona haya yanafanyika, serikali ilipopiga marufuku mikutano ya siasa ambayo ni kinyume kabisa na katiba, tungeona hata vyama vya upinzani vikifungua kesi ya katiba kupiga hilo... lakini wapi, hakuna aliefanya hivyo.
Kwenye uchaguzi mdogo wa kata ulioisha hizi karibuni, vyama vya upinzani vimefanyiwa kila aina ya hujuma.. lakini mpaka sasa hatujasikia hata chama kimoja cha upinzani kikikata shauri mahakamani kupinga matokeo.
Tukubali tukatae, mahakamani ndo sehemu pekee vyama vya upinzani vinaweza vikawa na chance ya kupata haki zao. Kwasababu tumesikia mara kadhaa wapinzani wakishinda kesi za ubunge na udiwani mahakamani. So they have a chance there, lakini kama wakitegemea huruma za chama tawala watalia na kusaga meno.
Pia ni dhahiri bila mabadiliko ya kifumo na kisheria kwenye masuala ya uchaguzi, itakuwa ni ngumu kwa vyama vya upinzani kushinda au kutangazwa washindi kwenye chaguzi mbalimbali, lakini pamoja na malalamiko hayo, bado hakuna hata mwanasiasa mmoja wa upinzani aliethubutu kupeleka muswada binafsi bungeni, ili kuchochea kupatikana kwa tume na mfumo huru wa uchaguzi. Hata kama the odds zitakuwa against them, lakini hata kujaribu tu. Hakuna.
Sio siri CCM imechokwa ila vyama vya upinzani vina-disappoint kwa kutochukua hatua zozote na kuishia kulalamika tu kila siku. Inabidi vizinduke na kuanza kuchukua hatua mbalimbali za kisheria na sio kila siku kuitisha press conference tu na kutoa matamko halafu basi.
Wanasema insanity is doing the same thing and expecting different results. So its obvious approach ya sasa hivi ya vyama vya upinzani havifanyi kazi,kwa hiyo wajaribu njia nyingine.
Tunataka kusikia kesi mbalimbali za kikatiba na kisheria kupinga mambo yanayofanywa na serikali ya awamu hii, na hata kupeleka miswada bungeni kurekebisha kasoro za kimfumo na kisheria. Hata kama it wont work out ila wawe na uthubutu hata wakujaribu kufanya hayo. Hicho ndo wananchi wanataka kuona.