Kwa hali hii timu za waarabu zitatawala sana,. Simba na yanga igeni mfano huu

py thon

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
2,471
4,424




TIMU ZA N.AFRICA ZITAENDELEA KUTAWALA

-Ukizungumzia soka la bara la Africa Maarufu kama CAF champions league lazima utagusa ukanda wa Afrika kaskazini sababu klabu kutoka ukanda huo wamekuwa wakitawala michuano haya kwa muda mrefu wakipata changamoto kwa vilabu 2 tu ambazo ni TP Mazembe kutoka DRC na mamelody kutoka Afrika kusini .Nini siri ya vilabu hivi kutesa soka la bara ka Afrika

1.Wydad Casablanca
2.Al Ahly
3.Es Setif
4.Esperance de tunis
5.Etoel du sahel
6.USM Alger
7.Mc Alger

Vilabu hivi ama magwiji hawa wamekuwa wakifika nusu fainali ya CAF kila wakati na kuchukua makombe na vilabu kutoka ukanda mwingine ni Mazembe na Mamelody Sundowns tu ndio wamekuwa wakiwapa changamoto vinara hawa kutoka Afrika kaskazini

Kuna watu wanasema vilabu vya Afrika kaskazini wakiwaita kwa jina maarufu "waarabu" kuwa wana fitina la hasha sio kweli nimewafuatilia sana


1.Licha ya timu hizi kucheza soka la kuvutia lakini silaha yao kubwa ni mashabiki ,ukienda away kucheza na vilabu hivi tegemea kufungwa magoli mengi kuanzia 4-na kuendelea.

2.Mashabiki kuanzia dakika ya 1-90 wanashangilia kwa nguvu ,makelele ,wanawasha moto mekundu ,wanapiga ngoma kwa nguvu na spirit ya wachezaji inakuwa juu sana nawapa assignment tafuta matokeo ya nyumbani ya vilabu niliyoorodhesha hapo juu utaona wanashinda 9,7,6


2.Turudi bongo nilikuwa natizama game ya yanga na Township rollers la haula uwanja ulikuwa na ma gap mengi ,mapengo mengi na pia hao mashabiki waliokuwepo wanashangilia kwa matukio haswa kwenye mashambulizi ya kustukiza au kanzu tobo ila muda mwingi wapo kimya kama maiti mpaka unajiuliza mantiki ya mashabiki kwenda uwanjani ni nini sasa ukiwa kimya muda mwingi mpaka goli liingie huko sio kuiunga timu na kuipa nguvu


Hebu vilabu vyetu pendwa simba na yanga igeni mfano kutoka Al ahly hapo chini au WAC Casablanca hapo juu ,mnavyoona timu zinapigwa goli 5,6,7 huko kwao na kufika fainali kila mwaka sio wanajua sana ila makelele ,pressure ya mashabiki huchangia kwa kiasi kikubwa na hakuna fitna yeyote.






Au tizama Al Ahly walivyocheza na yanga mpaka yanga wakapoteana uwanjani walishindwa kuendana na presha



NB:Mashabiki wa simba na yanga msiwe maiti uwanjani badilikeni
 
Umesahau uzalendo pia unakuta shabiki wa yanga anaenda game LA simba ili akashabikie timu pinzani na kuwazomea wasimba.
 
hilo ni moja lakini kuna mengi pia yanayofanya timu za warabu zifanye vizuri kwanza wenzetu hawana ujanja kwenye makuzi ya wachezaji wao ,wanaanza kuwa chini ya uangalizi maalum toka wakiwa na miaka 9 tena chini ya jopo la makocha wenye viwango vya juu na hpo watafundishwa vitu muhimu technically na tactically ikiwemo pia displini ya ndani na nje ya uwanja, Anaandaliwa tokea mdogo kuwa mpira ni kazi yake na lazima aiheshimu....by the time hyo mtoto akifikisha miaka 18 tayari anakuwa kashaiva kila eneo na anakuwa yupo tayari kwa ajili ya ushindani tofauti kbsa na sisi ambapo wachezaji wanajikuza wenyewe kwenye viwanja vya wavuta bangi bila usimamizi wowote mwisho wa siku output haiwezi kuwa sawa na yule aliyekuzwa kwa mfumo ambao ni rasmi
 
Waarabu wapo juu bwana hakuna cha fitina wa nini. Tuna kawaida tukifungwa tunaanza zengwe mara oh kama kawaida yao waarabu kubebwa. In short wenzetu wanatumia akili uwanjani sio porojo.
 




TIMU ZA N.AFRICA ZITAENDELEA KUTAWALA

-Ukizungumzia soka la bara la Africa Maarufu kama CAF champions league lazima utagusa ukanda wa Afrika kaskazini sababu klabu kutoka ukanda huo wamekuwa wakitawala michuano haya kwa muda mrefu wakipata changamoto kwa vilabu 2 tu ambazo ni TP Mazembe kutoka DRC na mamelody kutoka Afrika kusini .Nini siri ya vilabu hivi kutesa soka la bara ka Afrika

1.Wydad Casablanca
2.Al Ahly
3.Es Setif
4.Esperance de tunis
5.Etoel du sahel
6.USM Alger
7.Mc Alger

Vilabu hivi ama magwiji hawa wamekuwa wakifika nusu fainali ya CAF kila wakati na kuchukua makombe na vilabu kutoka ukanda mwingine ni Mazembe na Mamelody Sundowns tu ndio wamekuwa wakiwapa changamoto vinara hawa kutoka Afrika kaskazini

Kuna watu wanasema vilabu vya Afrika kaskazini wakiwaita kwa jina maarufu "waarabu" kuwa wana fitina la hasha sio kweli nimewafuatilia sana


1.Licha ya timu hizi kucheza soka la kuvutia lakini silaha yao kubwa ni mashabiki ,ukienda away kucheza na vilabu hivi tegemea kufungwa magoli mengi kuanzia 4-na kuendelea.

2.Mashabiki kuanzia dakika ya 1-90 wanashangilia kwa nguvu ,makelele ,wanawasha moto mekundu ,wanapiga ngoma kwa nguvu na spirit ya wachezaji inakuwa juu sana nawapa assignment tafuta matokeo ya nyumbani ya vilabu niliyoorodhesha hapo juu utaona wanashinda 9,7,6


2.Turudi bongo nilikuwa natizama game ya yanga na Township rollers la haula uwanja ulikuwa na ma gap mengi ,mapengo mengi na pia hao mashabiki waliokuwepo wanashangilia kwa matukio haswa kwenye mashambulizi ya kustukiza au kanzu tobo ila muda mwingi wapo kimya kama maiti mpaka unajiuliza mantiki ya mashabiki kwenda uwanjani ni nini sasa ukiwa kimya muda mwingi mpaka goli liingie huko sio kuiunga timu na kuipa nguvu


Hebu vilabu vyetu pendwa simba na yanga igeni mfano kutoka Al ahly hapo chini au WAC Casablanca hapo juu ,mnavyoona timu zinapigwa goli 5,6,7 huko kwao na kufika fainali kila mwaka sio wanajua sana ila makelele ,pressure ya mashabiki huchangia kwa kiasi kikubwa na hakuna fitna yeyote.






Au tizama Al Ahly walivyocheza na yanga mpaka yanga wakapoteana uwanjani walishindwa kuendana na presha



NB:Mashabiki wa simba na yanga msiwe maiti uwanjani badilikeni


%100 sure
 
Ukweli ukiacha hayo watu tunasema fitina ila waarabu mpira wanaupiga mwingi sana alfu mashabiki wao ni balaaa kuna gem nilikuwa naangalia ya super cup..Waydad Casablanca na Tp Mazembe aiseee jamaaa ni shidaaa na mashabiki mda wote wananiangilia..
 
Ukweli Ni Kwamba Tunahitaji Miaka 300 ili Tuweze Kuwafika Waarabu Kisoka.
Staa Wa Tanzania Ni Mbwana Samata Anaecheza Ligi Ya Wakulima Belgium. Wakati Wenzetu Kina Zamalek, Alhaly na Wengineo Wanatoa Kina Ben Yedder, Mo Salah, Elneny na Wengineo Ambao Wapo Uengereza, Spain, Ujerumani, Italy na Ufaransa.

So, Hatuna Uwezo Wa Kuwafikia Waarabu Wanaocheza Kombe La Dunia Wakati Tz AFCON Ni Kitendawili.

Sisi Turidhike na Kujiita [HASHTAG]#Wakimataifa[/HASHTAG].
 
Back
Top Bottom