Esoterica
Member
- Jun 18, 2011
- 48
- 11
Wakuu,
Ninaangalia mijadala ya leo bungeni tangu saa 3 asubuhi. Wabunge wengi waliochangia hotuba ya Ngeleja leo wamesema hawaungi mkono hoja; wamo Mh Naomi Kaihula, Dr Kigwangala, Shelukindo, Bulaya, Sendeka, Nasor, nk..
Vilevile kutokana na hali hii Mh Lukuvi nimemuona akihaha toka eneo moja hadi jingine kufanya mijadala na watu mbali mbali. Alianza kwa kuteta na Mh Adam Malima pamoja na Ghasia, kisha akahamia ktk eneo jingine na kuteta na kina Sendeka pia nikamuona Mh Diana Kilolo akimuacha swahiba na jirani yake EL na kwenda kuteta na Mh J Makamba huku akiwa amechuchumaa. Hatimaye Mh Pinda aliteta kwa hisia kali na Mh Wasira (Mzee wa Kusinzia).
Ninahisi vikao hivi visivyo rasmi na mashinikizo ya wabunge yanaonyesha hali si shwari. Pia Mchana huu kuna vikao vya ki-chama vya CCM na CDM ninafikiri vina lengo la kuweka misimamo ya kichama.
Je Ngeleja na serikali itapona leo?
Wakuu ninaomba kuwasilisha.................................
Ninaangalia mijadala ya leo bungeni tangu saa 3 asubuhi. Wabunge wengi waliochangia hotuba ya Ngeleja leo wamesema hawaungi mkono hoja; wamo Mh Naomi Kaihula, Dr Kigwangala, Shelukindo, Bulaya, Sendeka, Nasor, nk..
Vilevile kutokana na hali hii Mh Lukuvi nimemuona akihaha toka eneo moja hadi jingine kufanya mijadala na watu mbali mbali. Alianza kwa kuteta na Mh Adam Malima pamoja na Ghasia, kisha akahamia ktk eneo jingine na kuteta na kina Sendeka pia nikamuona Mh Diana Kilolo akimuacha swahiba na jirani yake EL na kwenda kuteta na Mh J Makamba huku akiwa amechuchumaa. Hatimaye Mh Pinda aliteta kwa hisia kali na Mh Wasira (Mzee wa Kusinzia).
Ninahisi vikao hivi visivyo rasmi na mashinikizo ya wabunge yanaonyesha hali si shwari. Pia Mchana huu kuna vikao vya ki-chama vya CCM na CDM ninafikiri vina lengo la kuweka misimamo ya kichama.
Je Ngeleja na serikali itapona leo?
Wakuu ninaomba kuwasilisha.................................