Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
Mhe. Kikwete alikuwa sahihi kukata jina la Membe 2015 kuwa mgombea urais kupitia CCM kwa kweli hana ushawishi wala mvuto wowote kwa watanzania, Kama kikwete angefanya kosa la kumpitisha huyu mtu 2015 Kisha apambane na Lowasa leo tungekuwa tunazungumza Lugha nyingine kabisa kwenye siasa za Tanzania.
Viongozi wa CCM wamekuwa wajanja sana hata uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020 walipoona ameanza chokochoko wakamtimua mapema ili asiharibu mipango ya uchaguzi kumbe waliona mbali Bernad Membe hana ushawishi hata kidogo wa kuwa kwenye nafasi kubwa Kama ya urais.
Hana ushawishi ndani ya chama wala nje ya CCM, kwa kifupi watanzania wamempuuza huyu mtu.
Kiuhalisia ukiacha mtaji mkubwa wa wanachama walio nao CCM zaidi ya mil 15 lakini ukweli ni kwamba mgombea urais anapaswa kuwa na mvuto na kukubalika na hata watu wa vyama vingine na wasio na vyama jambo ambalo Magufuli kwa asilimia kubwa analo japo wengi hawataki kutamka wazi hilo.
Sasa kwa Membe yeye hana vyote viwili kwa pamoja. Najiuliza tu hii amsha amsha ya Tundu Lissu ndio angekutana na mtu dhaifu Kama Membe ccm wangeangukia pua mapema Sana.
Mhe. Zitto umekosea umechukua garasa umeshindwa kufikia akili ya Mbowe 2015 hata kwa 2%.
Viongozi wa CCM wamekuwa wajanja sana hata uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020 walipoona ameanza chokochoko wakamtimua mapema ili asiharibu mipango ya uchaguzi kumbe waliona mbali Bernad Membe hana ushawishi hata kidogo wa kuwa kwenye nafasi kubwa Kama ya urais.
Hana ushawishi ndani ya chama wala nje ya CCM, kwa kifupi watanzania wamempuuza huyu mtu.
Kiuhalisia ukiacha mtaji mkubwa wa wanachama walio nao CCM zaidi ya mil 15 lakini ukweli ni kwamba mgombea urais anapaswa kuwa na mvuto na kukubalika na hata watu wa vyama vingine na wasio na vyama jambo ambalo Magufuli kwa asilimia kubwa analo japo wengi hawataki kutamka wazi hilo.
Sasa kwa Membe yeye hana vyote viwili kwa pamoja. Najiuliza tu hii amsha amsha ya Tundu Lissu ndio angekutana na mtu dhaifu Kama Membe ccm wangeangukia pua mapema Sana.
Mhe. Zitto umekosea umechukua garasa umeshindwa kufikia akili ya Mbowe 2015 hata kwa 2%.