Kwa Dunia ya Sasa DNA ni muhimu. Msipuuze!

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,327
51,831
KWA DUNIA YA SASA "DNA" NI MUHIMU. MSIPUUZE!

Na, Robert Heriel.

Unajua kuna watu wanafikiri kizamani Sana, watu hawa hawakubali kuwa Dunia inabadilika. Watu hawa huitwa CONSERVATIVE, yaani wasiobadilika, au wasiokubali mabadiliko.

Dunia ya Sasa ni tofauti na yazamani Kwa mambo mengi, mathalani masuala ya kiutamaduni, kimaadili, kisayansi, kiutawala, tabia ya nchi, muingiliano baina ya watu na watu, muingiliano baina ya watu na wanyama, Lugha, miundombinu, mitindo ya maisha, ndoa n.k.

Katika kipengele kimoja cha Mahusiano ya ndoa na uzazi pia yapo mabadiliko makubwa Sana ambayo kimsingi watu wenye akili hawawezi kuyapuuza.

Ndoa za zamani na sasa zinatofautiana Kwa kiasi kikubwa.
Uzazi wa zamani na sasa haufanani.

Ingawaje masuala ya kubambikiana watoto hayajaanza Zama zetu, yalianza tangu zamani isipokuwa Zama zetu mambo haya yamezidi na lazima kizazi cha sasa kijichunge Sana.

Kupima DNA ni muhimu na inaweza kuwa lazima ikiwa mtoto ataonekana hana viashiria vyovyote vya mfanano na Baba.

Mtoto azaliwapo Jambo la pili baada ya kushukuru, kinachofuata ni kuangalia maumbile yake kuwa kafanana na Wazazi wake hasa Baba au laa,
Wanawake wengi hufurahi na kujivunia mtoto anapofanana na Baba/mumewe, bila Shaka wanafikiri hiyo itaongeza upendo na kuaminiwa na Mumewe.

Hata hivyo hakuna Raha Kwa Baba/Mwanaume aipatayo kama kufanana na Mwanaye, ingawa mtoto anaweza asifanane complete na Baba yake kimaumbile hasa Sura lakini yapo mambo Kuongea, Kutembea, kucheka, na tabia zingine.

Kusema kitanda hakizai haramu ni misemo ya kihuni na watu wasio na mbegu za kuzalisha. Misemo hiyo ilisemwa zamani na Wazee wakiume waliokuwa na matatizo ya uzazi, na hii ilitumika kuficha udhaifu wao huo, pia ulitumika na wahuni waliotaka kuhalalisha uhuni wa kuibiana Wake.

DNA NI MUHIMU KWA SABABU KUU ZIFUATAZO;

1. WANAWAKE WA SASA HAWANA UTU, WANAJALI NA WANATAMAA YA PESA
Ingekuwa wanawake wa kizazi hiki kinajali Utu basi pasingekuwa na haja ya kupima hayo madubwasha. Ila Kwa hawa wanawake wa siku hizi wasio waaminifu, Wabinafsi, wapenda pesa, ni muhimu kupima DNA. Wanawake wa siku hizi hawachelewi kukugeuka, hawachelewi kukuacha solemba hasa wakishaona watoto wameshakuwa wakubwa.

Kama mwanaume unakazi nzuri na unamuelekeo mzuri wa maisha basi wewe ndiye unapaswa uwe Makini zaidi katika mambo haya. Ni rahisi Sana kubambikiziwa mtoto, iwe ukiwa ndani ya Ndoa au nje ya Ndoa.

2. MAISHA YA SASA NI MAGUMU MNO.
Hakuna asiyejua ugumu WA maisha ya sasa hasa maisha ya mjini. Kila kitu ni pesa, maisha ni ghali mno.
Hakuna mtu asiyejua kuwa Kulea mtoto ni kupoteza nguvu katika uwekezaji wa maisha ya baadaye ya mtoto.
Kumpa chakula, kumpa mavazi, kumpa elimu Bora, kunahitaji nguvu ya akili, mwili, hisia na nguvu ya kiuchumi.

Unasomesha watoto unaodhani ni wako Kwa shida na kujibana, alafu wakifika umri Fulani wa kujitambua unakuja kugundua sio wako. Inaumiza mno, inaharibu akili na hisia.
Ni Bora ungejua tokea mwanzo wakiwa wadogo ili uamue kusuka au kunyoa.

Asikudanganye mtu kuwa mtoto ni mtoto, sio kweli, mtoto ni Yule uliyemzaa tuu, huyo ndiye mtoto wako. Duniani na Akhera inafahamika hivyo. Kwa binadamu na wanyama iko hivyo.

Kulea ni uwekezaji wa Mali, akili, hisia na nguvu kwa mtoto. Kumbuka unadhani ni mtoto wako, alafu uje kugundua sio wako. Usiombe.

Kuhusu Kulea mtoto ilimradi hata Kama sio wako kwani anaweza kuja kukusaidia siku za usoni hapo ni Probability, na uwezekano wa kusaidiwa na mtoto ambaye sio wako ni Asilimia ndogo Sana. Watoto wa hivi ni 1 Kwa 100. Huitwa Exceptional.

Mifano ipo mingi mno, wala sitaki kuwataja wakina Diamond hapa, ninayomifano yakutosha katika hili.

3. NDOA ZA SIKU HIZI SIO MPAKA KIFO KIWATENGANISHE, KUACHANA NI MUDA WOWOTE.
Pima DNA Kwa mtoto usiyemuelewa, au Kama huwaelewi watoto wako wote, Pima wote.
Ndoa za siku hizi sio mpaka kifo. Ingekuwa ndoa ni mpaka kifo basi ungejua kuwa utasaidiwa na watoto kupitia Mama Yao.
Na kikawaida watoto hata wakwako wa damu mi wepesi kusaidia nyumbani Kwa sababu ya nguvu ya Mama.

Lakini embu piga akili hapa, watoto sio wako, umewalea mpaka wamekuwa watu wazima umri wa kutafuta labda ni miaka 25+, washajua wewe sio Baba Yao, mara mama yao/mkeo anakuletea za kuleta muachane, na hii ipo sana.
Unafikiri hao watoto wataendelea kuwa watoto wako? Embu tumia akili hata ya kuzaliwa, inawezekana kweli?

Ndoa za siku hizi sio salama Sana, sio permanent isipokuwa ni ndoa za kutafuta pakijiegesha maisha yaende watoto wakue, wakishaanza kujitegemea Mama anaanza kusumbua kwani anajua atakimbilia Kwa watoto wake.

Ikiwa ukishaachana na Mkeo mnagawana Mali Kama nyumba, mahari, viwanja na mashamba, embu fikiria kuna watoto wasiowako Kwa huyo mwanamke, huoni Kama shida itakukumba siku hizo?.
Unafikiri ukishaachana na Mkeo hao watoto wasiowako kibaiolojia wataendelea kuwa wako? Embu tumia akili hata ya kwendea chooni tuu.

4. MATOTO YA SASA HIVI HAYANA ADABU.
Unajua kuna watu wanaakili za kitoto Sana. Yaani wanawaza Kama vile wametoka kulala hivi. Ati anasema nikishamlea na kumsomesha basi huyo ni mtoto wangu, hivi hiyo ni akili au matope?

Mtoto wako ni Yule uliyemzaa, Damu yako, huko kwingine ni kujigeuza mtu asiyeweza kufikiri vizuri. Na mtazamo huo sio Kwa kizazi cha watoto wa Utandawazi ambao hawana adabu hata Kwa Baba na Mama zao wa damu kabisa.

Ukile mtoto asiyewako Kwanza huna mamlaka naye kibinadamu, kiunyama, kijini, kimizimu na Kimungu. Huna mamlaka yoyote Ile katika maisha yake hasa akishakua mkubwa.

5. UTAKUWA MTUMWA WA MKE WAKO.
Ikitokea umelea mtoto asiyewako na Mungu akambariki, amini usiamini utakuwa MTUMWA wa Mke wako.
Unajua kuna watu hawataki kukubali kuwa uzee upo, na Hilo ni tatizo la Sisi wanaume tuliowengi.
Mtoto asiyewako mwenye mamlaka naye ni Mama yake sio wewe Baba.
Sasa hapo itategemea na hekima ya Mke wako.
Kama ni garagaja, basi utumwa kwako hauepukiki.

6. UFALME WAKO KUTAWALIWA NA MWANAUME MWINGINE.
Kuruhusu mtoto asiyewako ndani ya nyumba yako ni kuuza Ufalme wako Kwa mwanaume mwingine.
Ndio maana hata Kwa Wanyama Kama Simba hawezi ruhusu kitu Kama hicho kitokee. Ikiwa Simba anajua matokeo ya mambo hayo sembuse Sisi binadamu.

Labda awe mtoto wa kike, lakini akiwa wakiume ndio mbaya Kabisa.

Na Kwa bahati mbaya au nzuri kabisa, Wale watoto ambao sio wako au utakaowatelekeza wengi wao huwa na Nyota zaidi kuliko watoto wa nyumbani, na hii ni kutokana na kuwa wamechukua nyota ya walipotoka na hapo walipo.


DNA ni muhimu iwe ya kienyeji au ya kisasa hasa Kwa watoto usiowaelewa.

Hata hivyo, mambo haya hupaswa kufanyika mapema mtoto akiwa mdogo kabisa. Ili kupunguza uchungu na madhara kwako Mwanaume.


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Unaongelea conservatism kana kwamba ni ki2 kibaya? Kwanza unatakiwa uelewe kwamba bila uwepo wa conservatism binadamu angekua ashajieliminate duniani karne nyingi zilizopita.
 
Unaongelea conservatism kana kwamba ni ki2 kibaya? Kwanza unatakiwa uelewe kwamba bila uwepo wa conservatism binadamu angekua ashajieliminate duniani karne nyingi zilizopita.


Sasa hapa tunazungumzia ishu ya mabadiliko makubwa katika masuala ya mahusiano ya ndoa na uzazi
 
KWA DUNIA YA SASA "DNA" NI MUHIMU. MSIPUUZE!

Na, Robert Heriel.

Unajua kuna watu wanafikiri kizamani Sana, watu hawa hawakubali kuwa Dunia inabadilika. Watu hawa huitwa CONSERVATIVE, yaani wasiobadilika, au wasiokubali mabadiliko.

Dunia ya Sasa ni tofauti na yazamani Kwa mambo mengi, mathalani masuala ya kiutamaduni, kimaadili, kisayansi, kiutawala, tabia ya nchi, muingiliano baina ya watu na watu, muingiliano baina ya watu na wanyama, Lugha, miundombinu, mitindo ya maisha, ndoa n.k.

Katika kipengele kimoja cha Mahusiano ya ndoa na uzazi pia yapo mabadiliko makubwa Sana ambayo kimsingi watu wenye akili hawawezi kuyapuuza.

Ndoa za zamani na sasa zinatofautiana Kwa kiasi kikubwa.
Uzazi wa zamani na sasa haufanani.

Ingawaje masuala ya kubambikiana watoto hayajaanza Zama zetu, yalianza tangu zamani isipokuwa Zama zetu mambo haya yamezidi na lazima kizazi cha sasa kijichunge Sana.

Kupima DNA ni muhimu na inaweza kuwa lazima ikiwa mtoto ataonekana hana viashiria vyovyote vya mfanano na Baba.

Mtoto azaliwapo Jambo la pili baada ya kushukuru, kinachofuata ni kuangalia maumbile yake kuwa kafanana na Wazazi wake hasa Baba au laa,
Wanawake wengi hufurahi na kujivunia mtoto anapofanana na Baba/mumewe, bila Shaka wanafikiri hiyo itaongeza upendo na kuaminiwa na Mumewe.

Hata hivyo hakuna Raha Kwa Baba/Mwanaume aipatayo kama kufanana na Mwanaye, ingawa mtoto anaweza asifanane complete na Baba yake kimaumbile hasa Sura lakini yapo mambo Kuongea, Kutembea, kucheka, na tabia zingine.

Kusema kitanda hakizai haramu ni misemo ya kihuni na watu wasio na mbegu za kuzalisha. Misemo hiyo ilisemwa zamani na Wazee wakiume waliokuwa na matatizo ya uzazi, na hii ilitumika kuficha udhaifu wao huo, pia ulitumika na wahuni waliotaka kuhalalisha uhuni wa kuibiana Wake.

DNA NI MUHIMU KWA SABABU KUU ZIFUATAZO;

1. WANAWAKE WA SASA HAWANA UTU, WANAJALI NA WANATAMAA YA PESA
Ingekuwa wanawake wa kizazi hiki kinajali Utu basi pasingekuwa na haja ya kupima hayo madubwasha. Ila Kwa hawa wanawake wa siku hizi wasio waaminifu, Wabinafsi, wapenda pesa, ni muhimu kupima DNA. Wanawake wa siku hizi hawachelewi kukugeuka, hawachelewi kukuacha solemba hasa wakishaona watoto wameshakuwa wakubwa.

Kama mwanaume unakazi nzuri na unamuelekeo mzuri wa maisha basi wewe ndiye unapaswa uwe Makini zaidi katika mambo haya. Ni rahisi Sana kubambikiziwa mtoto, iwe ukiwa ndani ya Ndoa au nje ya Ndoa.

2. MAISHA YA SASA NI MAGUMU MNO.
Hakuna asiyejua ugumu WA maisha ya sasa hasa maisha ya mjini. Kila kitu ni pesa, maisha ni ghali mno.
Hakuna mtu asiyejua kuwa Kulea mtoto ni kupoteza nguvu katika uwekezaji wa maisha ya baadaye ya mtoto.
Kumpa chakula, kumpa mavazi, kumpa elimu Bora, kunahitaji nguvu ya akili, mwili, hisia na nguvu ya kiuchumi.

Unasomesha watoto unaodhani ni wako Kwa shida na kujibana, alafu wakifika umri Fulani wa kujitambua unakuja kugundua sio wako. Inaumiza mno, inaharibu akili na hisia.
Ni Bora ungejua tokea mwanzo wakiwa wadogo ili uamue kusuka au kunyoa.

Asikudanganye mtu kuwa mtoto ni mtoto, sio kweli, mtoto ni Yule uliyemzaa tuu, huyo ndiye mtoto wako. Duniani na Akhera inafahamika hivyo. Kwa binadamu na wanyama iko hivyo.

Kulea ni uwekezaji wa Mali, akili, hisia na nguvu kwa mtoto. Kumbuka unadhani ni mtoto wako, alafu uje kugundua sio wako. Usiombe.

Kuhusu Kulea mtoto ilimradi hata Kama sio wako kwani anaweza kuja kukusaidia siku za usoni hapo ni Probability, na uwezekano wa kusaidiwa na mtoto ambaye sio wako ni Asilimia ndogo Sana. Watoto wa hivi ni 1 Kwa 100. Huitwa Exceptional.

Mifano ipo mingi mno, wala sitaki kuwataja wakina Diamond hapa, ninayomifano yakutosha katika hili.

3. NDOA ZA SIKU HIZI SIO MPAKA KIFO KIWATENGANISHE, KUACHANA NI MUDA WOWOTE.
Pima DNA Kwa mtoto usiyemuelewa, au Kama huwaelewi watoto wako wote, Pima wote.
Ndoa za siku hizi sio mpaka kifo. Ingekuwa ndoa ni mpaka kifo basi ungejua kuwa utasaidiwa na watoto kupitia Mama Yao.
Na kikawaida watoto hata wakwako wa damu mi wepesi kusaidia nyumbani Kwa sababu ya nguvu ya Mama.

Lakini embu piga akili hapa, watoto sio wako, umewalea mpaka wamekuwa watu wazima umri wa kutafuta labda ni miaka 25+, washajua wewe sio Baba Yao, mara mama yao/mkeo anakuletea za kuleta muachane, na hii ipo sana.
Unafikiri hao watoto wataendelea kuwa watoto wako? Embu tumia akili hata ya kuzaliwa, inawezekana kweli?

Ndoa za siku hizi sio salama Sana, sio permanent isipokuwa ni ndoa za kutafuta pakijiegesha maisha yaende watoto wakue, wakishaanza kujitegemea Mama anaanza kusumbua kwani anajua atakimbilia Kwa watoto wake.

Ikiwa ukishaachana na Mkeo mnagawana Mali Kama nyumba, mahari, viwanja na mashamba, embu fikiria kuna watoto wasiowako Kwa huyo mwanamke, huoni Kama shida itakukumba siku hizo?.
Unafikiri ukishaachana na Mkeo hao watoto wasiowako kibaiolojia wataendelea kuwa wako? Embu tumia akili hata ya kwendea chooni tuu.

4. MATOTO YA SASA HIVI HAYANA ADABU.
Unajua kuna watu wanaakili za kitoto Sana. Yaani wanawaza Kama vile wametoka kulala hivi. Ati anasema nikishamlea na kumsomesha basi huyo ni mtoto wangu, hivi hiyo ni akili au matope?

Mtoto wako ni Yule uliyemzaa, Damu yako, huko kwingine ni kujigeuza mtu asiyeweza kufikiri vizuri. Na mtazamo huo sio Kwa kizazi cha watoto wa Utandawazi ambao hawana adabu hata Kwa Baba na Mama zao wa damu kabisa.

Ukile mtoto asiyewako Kwanza huna mamlaka naye kibinadamu, kiunyama, kijini, kimizimu na Kimungu. Huna mamlaka yoyote Ile katika maisha yake hasa akishakua mkubwa.

5. UTAKUWA MTUMWA WA MKE WAKO.
Ikitokea umelea mtoto asiyewako na Mungu akambariki, amini usiamini utakuwa MTUMWA wa Mke wako.
Unajua kuna watu hawataki kukubali kuwa uzee upo, na Hilo ni tatizo la Sisi wanaume tuliowengi.
Mtoto asiyewako mwenye mamlaka naye ni Mama yake sio wewe Baba.
Sasa hapo itategemea na hekima ya Mke wako.
Kama ni garagaja, basi utumwa kwako hauepukiki.

6. UFALME WAKO KUTAWALIWA NA MWANAUME MWINGINE.
Kuruhusu mtoto asiyewako ndani ya nyumba yako ni kuuza Ufalme wako Kwa mwanaume mwingine.
Ndio maana hata Kwa Wanyama Kama Simba hawezi ruhusu kitu Kama hicho kitokee. Ikiwa Simba anajua matokeo ya mambo hayo sembuse Sisi binadamu.

Labda awe mtoto wa kike, lakini akiwa wakiume ndio mbaya Kabisa.

Na Kwa bahati mbaya au nzuri kabisa, Wale watoto ambao sio wako au utakaowatelekeza wengi wao huwa na Nyota zaidi kuliko watoto wa nyumbani, na hii ni kutokana na kuwa wamechukua nyota ya walipotoka na hapo walipo.


DNA ni muhimu iwe ya kienyeji au ya kisasa hasa Kwa watoto usiowaelewa.

Hata hivyo, mambo haya hupaswa kufanyika mapema mtoto akiwa mdogo kabisa. Ili kupunguza uchungu na madhara kwako Mwanaume.


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam

DNA test lengo ni kudhibiti (ku-control) mtu/watu.

Biashara ya kudhibiti watu Mungu mwenyewe aliamua kuachana nayo akatupatia amri 10 ili tupambane nazo..hukumu baadae.

Endelea na matumizi ya DNA test ili uteseke maisha yako yote.
 
DNA test lengo ni kudhibiti (ku-control) mtu/watu.

Biashara ya kudhibiti watu Mungu mwenyewe aliamua kuachana nayo akatupatia amri 10 ili tupambane nazo..hukumu baadae.

Endelea na matumizi ya DNA test ili uteseke maisha yako yote.
Usidhani wote watateseka wakijua watoto si wao. Hivi unatumia maka-lio kufikiria? Mbona logic zako za kitoto hivyo?
 
Sasa hapa tunazungumzia ishu ya mabadiliko makubwa katika masuala ya mahusiano ya ndoa na uzazi
Nimesoma paragraph yako ya kwanza na nimeamua niweke sawa kabla sijaendelea kusoma. Nimeshidwa kuendelea kusoma sababu ya lugha uliyotumia kwenye paragraph husika.
 
Mjifunze kutoka kwa kijana mwenzenu mwanamuziki aitwae Diamond.
 
DNA test lengo ni kudhibiti (ku-control) mtu/watu.

Biashara ya kudhibiti watu Mungu mwenyewe aliamua kuachana nayo akatupatia amri 10 ili tupambane nazo..hukumu baadae.

Endelea na matumizi ya DNA test ili uteseke maisha yako yote.


MUNGU yupi?
Yahweh?
Allah?
Baha?
Baal?
Endor?

Au Mungu yupi ili nijue tunajadiliana vipi hapa
 
Back
Top Bottom