Kwa CHADEMA na Viongozi wake hasa Freeman Mbowe na Dr Slaa....

STEIN

JF-Expert Member
Aug 29, 2010
1,770
553
Kwanza kabisa nianze kwa kuwapongeza viongozi wa CDM na Wanachama wake kwa kuweza kupambambana na mafisadi mapapa kama tulivyoona kwenye mchakato wa uchaguzi hivi karibuni.. Ni ushindi wa Wanyonge dhidi ya mafisadi wa nchi hii... Pamoja kwamba inaaminika ndiyo uchaguzi uliotumia Pesa nyingi sana kuliko uchaguzi wowote ule uliofanyika nchi hii...

Kumbuka ilikuwa ni vita ya pamoja CCM na Lowasa dhidi ya CDM/Nassari kwa hiyo kulikuwa na sources za pesa kutoka CCM na Lowasa kama namna ya kuwaonyesha kwamba yeye bado anakubalika....

Sasa ukweli umeonekana na wana Arumeru wamekombolewa kutoka mikononi mwa Wakoloni CCM,
Sasa CDM imeonyesha kwamba inaweza kuchukua nchi hii hata CCM wakitumia mbinu zote ambazo hazijawahi tumika...

Maana CDM inakubalika Kanda ya Ziwa(Mwanza, Mara, Shinyanga, Bukoba)... Kanda ya Kaskazini(Arusha, Kilimanjaro, Manyara).... Nyanda za Juu Kusini (Mbeya, Iringa na Njombe), Kanda ya Mashariki (Dar, Morogoro).... na Mokoa ya Kigoma, Songea etc... kama kuna sehemu nyingine nimesahau basi wadau waongezee na nini kifanyike....

Ushauri wangu kwa Dr Slaa na Mbowe
1. Kwa kuwa CDM imefikia mafanikio haya, Kwa kuwa watanzania tumefikia mafanikio haya wao wakiwa viongozi wakuu wa CDM wanatakiwa kupanga timu nzuri yenye watu wenye influence na misimamo katika hizo sehemu kabla ya kufikia 2014.

2. Wafanye Reseach ya kwa nini watanzania wengi hawapigi kura na kuleta proposal ya jinsi gani ya kuwashawishi watu kukubali kupiga kura na kulinda kura....

3. Ifanyike Operation moja ya kumzungusha inchi Nzima Mh Nasari katika kuhakikisha moto huu uliowasha Arumeru hauzimiki hadi 2015..

Mwisho natoa Pongezi kwa mashujaa wetu kwa mapambo najua kuna walioumia kwa kumwagiwa Tindikali, waliopigwa mashoka na mapanga mungu awaongezee nguvu zaidi ya kupambana na hayo majambazi.
Shukrani za kipekee zieonde kwa Mbowe, Dr Slaa, Tundu Lisu, Myika, zito, Wenje, V. Nyerere, Kiwia, Machemli, Mch Petee,Mdee, Nasari, Sugu... na wengine wengi kwa kufanikisha ushindi

Katika List ya watu wa kuwazungusha Nchi Nzima naomba tumwongeze Godbles Lema ili kuvuta Hisia za watu dhidi ya Manyanyaso wanayofanyiwa viongozi wa CDM hasa wale wenye misimamo..
Ahsanteni Peoples Power
 
Ushauri mzuri.
Viongozi wetu wa cdm, tambueni kuwa 2015 cdm inachukuwa nchi, nawaombeni sana, mbinu zilizotumika kunyakuwa majimbo yote yaliyo chini ya cdm, inatakiwa iboreshwe na pia itumike 2015 in effective manner, hata kama itakuwa costy, hizo pesa tutachanga tu, tunataka ccm watoke 2015.
 
Nimeipenda sana hii ya kumzungusha nassar nchi nzima. Maana itaamusha ari mpya na kuleta msisimko kwa chama. Peopooooz power.
 
Stain hivi CDM ndio wakwenda kuchukua nchi 2015?

Kimsingi Nchi iko mikononi mwa CDM kwani CDM wana nguvu ya umma na CCM ina nguvu ya Dola, Ndiyo maana hata sasa Serikali inatekeleza ilani ya CDM mfano Katiba mpya etc...

2015 ni kwenda tu kumweka Dr. Slaa pale magogoni ili kuharakisha maamuzi hasa ya kushughulukia mafisadi na kuwaondoa walowezi kama wahindi, Wazungu, Makaburu, wachina na waarabu ambao wanatamba duniani eti Tanzania ni nchi ambayo unachukua kila unachokitaka bila hata kuulizwa lakini lakini mtanzania akigusa tu au kunusa analo Risasi mfano Madini na Wanyama....

Huu nu Unyama tunafanyiwa na CCM.... kwani tunaona watu wetu wakipigwa risasi kwa kuwinda digidigina sungura wakati twiga, simba etc wanavushwa KIA kwenda Uarabuni bure.. Hii ainiingii akilini..
 
Stain hivi CDM ndio wakwenda kuchukua nchi 2015?

Nilichogundua hapa wewe siyo Mtanzania,Basi kama ni mtanzania ni mmoja wa Mafisadi
wakubwa ktk hii nchi,au la basi una matatizo ya akili unapaswa kwenda wodi ya vichaa
kupimwa"
 
oin Date : 25th January 2012Posts : 93
Rep Power : 329
Likes Received19
Likes Given33


Nilichogundua hapa wewe siyo Mtanzania,Basi kama ni mtanzania ni mmoja wa Mafisadi
wakubwa ktk hii nchi,au la basi una matatizo ya akili unapaswa kwenda wodi ya vichaa
kupimwa"

Kichaa hujulikana kwa hulka yake, kurusha mawe na lugha za mtusi na kutoa pofu mdomoni. Mimi nilishapimwa mara nyingi tu niko fiti sijui wewe. Kwanza unaonekana una matatizo ya kufikiri. Mimi niliuliza swali tu la kiuchokozi kupata mtazamo, lakini wewe unaniita sio mtanzania, fisadi na kichaa. Mbona unanionea hivyo? Hebu angalia Stain mwenyewe alivyojipambanua. amenieleza sababu anazojua, kama Graph ya kukubalika kwa CDM inapanda (Sijui kama wewe hata unaelewa maana yake). Hili sio jukwaa la matusi. Na matusi huwa hayanidhuru hata kidogo. Na mimi sitaki kukutusi.
 
Sasa wewe unashangaa nii? Angalia graph ya CDM na CCM ipi ina rise na ipi ina fall kila kukicha?NANI AMEANZA NA USHINDI WA MEZANI?NAJUA HATA SEGEREA HAMTAKUBALI.HIVI 2015 NI MBALI?

Sishangai bali nataka taarifa yakinifu. Pale kuna alama ya kuuliza sio mshangao.
 
Kimsingi Nchi iko mikononi mwa CDM kwani CDM wana nguvu ya umma na CCM ina nguvu ya Dola, Ndiyo maana hata sasa Serikali inatekeleza ilani ya CDM mfano Katiba mpya etc...

2015 ni kwenda tu kumweka Dr. Slaa pale magogoni ili kuharakisha maamuzi hasa ya kushughulukia mafisadi na kuwaondoa walowezi kama wahindi, Wazungu, Makaburu, wachina na waarabu ambao wanatamba duniani eti Tanzania ni nchi ambayo unachukua kila unachokitaka bila hata kuulizwa lakini lakini mtanzania akigusa tu au kunusa analo Risasi mfano Madini na Wanyama....

Huu nu Unyama tunafanyiwa na CCM.... kwani tunaona watu wetu wakipigwa risasi kwa kuwinda digidigina sungura wakati twiga, simba etc wanavushwa KIA kwenda Uarabuni bure.. Hii ainiingii akilini..

Stain mimi nakubaliana na wewe sana, na ninajua unachozungumza, na sasa tunarudi Arusha, Hapa CCM inabidi waipate fresh ili wajue kwamba milango ya ushindi kwa CDM i wazi 2015.
 
ushauri mzuri.
Viongozi wetu wa cdm, tambueni kuwa 2015 cdm inachukuwa nchi, nawaombeni sana, mbinu zilizotumika kunyakuwa majimbo yote yaliyo chini ya cdm, inatakiwa iboreshwe na pia itumike 2015 in effective manner, hata kama itakuwa costy, hizo pesa tutachanga tu, tunataka ccm watoke 2015.


hebu nenda kwenye web site ya chadema.com utakuta email za viongozi watumie ushauri huu pia maana si wote wanaotazama jf
 
Stain mimi nakubaliana na wewe sana, na ninajua unachozungumza, na sasa tunarudi Arusha, Hapa CCM inabidi waipate fresh ili wajue kwamba milango ya ushindi kwa CDM i wazi 2015.


wera wera !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Peoples Power? Thank you for joining M4C....
 
Kimsingi Nchi iko mikononi mwa CDM kwani CDM wana nguvu ya umma na CCM ina nguvu ya Dola, Ndiyo maana hata sasa Serikali inatekeleza ilani ya CDM mfano Katiba mpya etc...

2015 ni kwenda tu kumweka Dr. Slaa pale magogoni ili kuharakisha maamuzi hasa ya kushughulukia mafisadi na kuwaondoa walowezi kama wahindi, Wazungu, Makaburu, wachina na waarabu ambao wanatamba duniani eti Tanzania ni nchi ambayo unachukua kila unachokitaka bila hata kuulizwa lakini lakini mtanzania akigusa tu au kunusa analo Risasi mfano Madini na Wanyama....

Huu nu Unyama tunafanyiwa na CCM.... kwani tunaona watu wetu wakipigwa risasi kwa kuwinda digidigina sungura wakati twiga, simba etc wanavushwa KIA kwenda Uarabuni bure.. Hii ainiingii akilini..

Kwa upande wa wahindi tutaanza na Sabodo halafu tunakuja kwa Prof Shivji au sio?.........................
 
Back
Top Bottom