Kwa anayofanya Rais Magufuli leo, yana tofauti gani na ya Kinjekitile Ngwale wa mwaka 1905? Tuwe wakweli na huru kujadili!

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Katika historia ambayo nilijikuta nakasirika baada ya kuisoma basi ni ya Kinjekitile Ngwale na vita yake ya majimaji mwaka 1905 hadi 1907. Ni historia inayochefua mno ukiisoma. Na kwakweli sijui hata ni kwanini inafundishwa kwenye mitaala.

Tunaambiwa kuwa Kinjekitile aliwaambia watu wake endapo risasi zikifyatuliwa na wajerumani basi waseme "maji" na risasi ile papo hapo itageuka kuwa maji hivyo hawatadhurika nazo. Watu wake wakamuamini wakaingia vitani kwa miaka miwili huku wakiteketea.

Leo miaka takribani zaidi ya mia moja tunashuhudia kiongozi wetu wa kitaifa akituambia kuwa tukimtanguliza Mungu mbele na kuendelea na mishe zetu basi hatutadhurika na COVID 19. Matokeo yake ni vifo vya kuogofya vinavyofululiza ambavyo hata hatujui vinakotoka.

Ajabu anao wafuasi wake wanamtetea mchana kweupeee eti kiongozi wetu yupo sawa! Hapana! Tunampotosha na kuzidi kujidanganya wenyewe! Wapo wanaosema eti anasifiwa mpaka kimataifa! Wapi?

Yani kwa haya wanayofanya baadhi yetu tena tukiwa peke yetu inadhihirisha kuwa watanzania wameongezeka uwezo wa kufikiri kwa ratio ndogo sana huku wengi wetu wakiwa hawana tofauti yoyote kifikra na wale wakazi wa kusini wa mwaka1905. Ni aibu kubwa kwetu.

Emb tujitafakari, the tupo mahali sahihi kwa haya tunayofanya? Yanakubalika kijamii? Nini hasa kinaisumbua jamii yetu?
 
Au yule mfalme wa nchi ya kusadikika. Kwa walio soma kitabu cha Shaaban Robert
 
Kuwa na heshima na Kinjekitile ..
Kinjekitile alikuwa kiongozi halisi alieweka historia na alama Kwa watu wake..

Waliokwenda ujerumani wanajua history halisi ya Vita ya majimaji..


Kinjekitile alikuwa na PhD?
Alikuwa na wasomi wa kumshauri?..
Alikuwa na jeshi lenye bunduki?..
Alikuwa hata na bajeti?


Tafuta mifano ya kuweka badala ya kukejeli wanaostahili kuheshimiwa..

Kumlinganisha jiwe na Kinjekitile ni kebehi Kwa Kinjekitile
 
Kuwa na heshima na Kinjekitile ..
Kinjekitile alikuwa kiongozi halisi alieweka historia na alama Kwa watu wake..

Waliokwenda ujerumani wanajua history halisi ya Vita ya majimaji..


Kinjekitile alikuwa na PhD?
Alikuwa na wasomi wa kumshauri?..
Alikuwa na jeshi lenye bunduki?..
Alikuwa hata na bajeti?


Tafuta mifano ya kuweka badala ya kukejeli wanaostahili kuheshimiwa..

Kumlinganisha jiwe na Kinjekitile ni kebehi Kwa Kinjekitile
Kiukweli kinjikitile alikuwa ni bonge la shujaa, yaani watu hawana silaha lakini aliwahamasisha na waliendesha Vita kwa muda wa miaka miwili, watu wanabunduki na mizinga jamaa Wana rungu na panga, na kwenye Vita Ile mjerumani alikuja kushinda baada ya kuyachoma Moto mashamba ya chakula
 
Anamtafuta mbuzi wa kafara baada ya kushindwa, anataka kuficha aibu.
Pascal na wenziwe wanalijua hili wanamsaidia kuepusha aibu
 
Almost 100 years ago, a leader from the Southern Tanganyika told his countrymen to drink a herbal liquid so as to turn the German bullets into water!!! As a result, 120,000 among his people died.
100 years later, in the same country, this time from the North, a leader is telling his countrymen to inhale the herbal steam at 100°C as a cure to COVID19. But this time the leader is a PhD holder in Chemistry!!!
 
Mi naitazama tofauti kwa upande (view) tofauti.
Kinjekitile alistick na dawa yake Moja tu, Mzee baba alikuja na mzigo wa kujifusha, hatujakaa vizuri akaibuka na mzigo wa nyungu,kufumba na kufumbua Kuna connection ya Madagascar. Sasa wanajeshi wake hatujui tushike lipi.
So hawalingani kwa kweli.
Hahahhahha
 
Hivi sheria za WHO zinasemaje kuhusu upotoshaji wa makusudi juu ya magonjwa hatari na kupelekea wanadamu kupoteza maisha?

In God we Trust
 
Back
Top Bottom