fdizzle
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 1,891
- 2,367
Jana nilikuwa natokea kwenye mihangaiko yangu ya kutafuta ugali, ilikuwa ni nyakati za jioni hivyo nikasogea kituo cha daladala na kusubiri Usafiri( Najua mtanishangaa member wa JF kupanda daladala maana humu wengi wenu mnamiliki Ford Ranger na wachache wanamiliki Prado)
Sasa ikaja daladala nikaingia na kuanza safari mbele kidogo kama mita 20 hivi kwa nyuma ikatokea Toyota Hilux ya Police ikiwa imewasha zile taa za juu za blue na nyekundu (sijui maitaje wenyewe)
Ile gari ya police ikaja mpaka ubavuni mwa daladala na kumwambia dereva aweke gari pembeni.
Kisha zikasimama zote, kama kawaida, dereva wa daladala akashuka kwenda "kumalizana" na yule traffic police.
Sisi abiria tukiwa hatujui kinachoendelea mara ghafla tunaona yule traffic ameshuka kwenye gari anakuja huku anamfokea dereva kwa kutaka kumpa rushwa na matokeo yake ile hela aliyopewa na dereva akaitupa upande wa pili wa barabara kisha akavua na kofia yake.
Then akatoa sijui camera au nini akapiga picha ile gari akampa maelezo dereva then akaenda kupanda gari yake na kugeuza na kurudi alipotoka.
Hicho kitendo ni cha dakika chache kilijaza watu na pia ilimfanya dereva kama kufadhaika fulani.
Hii inaonesha madereva waache kuishi kwa mazoea, sio kila mtu anaendekeza rushwa za kijinga.
Sasa ikaja daladala nikaingia na kuanza safari mbele kidogo kama mita 20 hivi kwa nyuma ikatokea Toyota Hilux ya Police ikiwa imewasha zile taa za juu za blue na nyekundu (sijui maitaje wenyewe)
Ile gari ya police ikaja mpaka ubavuni mwa daladala na kumwambia dereva aweke gari pembeni.
Kisha zikasimama zote, kama kawaida, dereva wa daladala akashuka kwenda "kumalizana" na yule traffic police.
Sisi abiria tukiwa hatujui kinachoendelea mara ghafla tunaona yule traffic ameshuka kwenye gari anakuja huku anamfokea dereva kwa kutaka kumpa rushwa na matokeo yake ile hela aliyopewa na dereva akaitupa upande wa pili wa barabara kisha akavua na kofia yake.
Then akatoa sijui camera au nini akapiga picha ile gari akampa maelezo dereva then akaenda kupanda gari yake na kugeuza na kurudi alipotoka.
Hicho kitendo ni cha dakika chache kilijaza watu na pia ilimfanya dereva kama kufadhaika fulani.
Hii inaonesha madereva waache kuishi kwa mazoea, sio kila mtu anaendekeza rushwa za kijinga.