Mwana Mtoka Pabaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 15,118
- 16,470
Kwa miaka kadhaa hapa Tanzania imekuwepo sheria ya Mabasi ya Abiria kutotembea usiku. Sheria hii inavyoonekana ipo hapa Tanzania tu kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati na imekuwa kikwazo kwa biashara za ndani na zile nchi jirani kwani inapunguza uwezo wa wafanyabiashara kusafiri kwa wakati.
Sababu kubwa za serikali yetu kutekeleza mfumo huu ni USALAMA. Asubuhi hii, kamanda wa Vikosi vya Usalama barabarani Kamishna Mpinga akiongea na Radio One amesema, ni kweli kuwa nchi jirani magari ya abiria yanatembea masaa 24 lakini kwa Tanzania imekuwa ni changamoto kwa kuwa nchi yetu ni kubwa ukilinganisha na Kenya na Uganda, Kongo na Rwanda.
Swali la kujiuliza ni hili; hii Tanzania ni kubwa kwa ardhi tu?
Idadi ya watu ni sawa na Kenya na Uganda? Rasilimali ni sawa na Kenya na Uganda? Jeshi letu ni sawa na Kenya na Uganda?
Hapa utaona kuwa sisi ni watu tusiokosa sababu kwa madhaifu yetu. Mimi binafsi sioni sababu ya majambazi kutufanya tujifiche ndani kwa kuhofia mabasi yatatekwa. Huko Kenya, kwa wafanyabiashara watakubaliana na mimi, ukipita usiku, utaona Road Blocks na wanajeshi wakiwa na taa zao pembeni wapo pundamilia wakila maganda ya machungwa na hali ya usalama wa barabara ni shwari.
Sisi tunaotembea mchana, wastani wa ajali za barabarani kwetu bado upo juu na tunakufa mchana huo huo. Binafsi sielewi kuona POLISI NA JESHI WANAWEZAJE KUTUMIWA KUTULIZA MAANDAMANO LAKINI UKASHINDIKANA KUPATIKANA UTARATIBU WA KUTULINDA TUKAFANYA BIASHARA ZETU KWA UHURU.
Wengi yawezekana msione umuhimu wa hili, lakini mimi niliwahi kuwa mwajiriwa na mfanyabiashara kwa wakati mmoja. Biashara ilikuwa ngumu sababu ya utaratibu huu mbaya. Laiti kama tungefanya kama wenzetu, basi kulikuwa kuna uwezekano wa mimi kutoka DAR usiku, nikaingia Mombasa asubuhi, nikafunga mizigo yangu mchana kutwa, na usiku nikaingia tena safarini asubuhi ikanikuta Dar na nikafungua duka langu na kuendelea na biashara zangu. Lakini piga picha inanichukua muda gani kukamilisha zoezi lile lile kwa utaratibu huu uliopo?
Mimi nafikiri umefika wakati wa serikali kuacha hii primitive attitude na kuishi kwa malengo. Haiwezekani changamoto za namna hii ziitwe sababu muafaka za sisi kuwa nyuma na tukachekelea. Tanzania si kubwa kama Congo. Na nchi ikiwa kubwa ni more advantageous kuliko ingekuwa ndogo kwa hiyo serikali itutoe hapa bila visingizio.
Sababu kubwa za serikali yetu kutekeleza mfumo huu ni USALAMA. Asubuhi hii, kamanda wa Vikosi vya Usalama barabarani Kamishna Mpinga akiongea na Radio One amesema, ni kweli kuwa nchi jirani magari ya abiria yanatembea masaa 24 lakini kwa Tanzania imekuwa ni changamoto kwa kuwa nchi yetu ni kubwa ukilinganisha na Kenya na Uganda, Kongo na Rwanda.
Swali la kujiuliza ni hili; hii Tanzania ni kubwa kwa ardhi tu?
Idadi ya watu ni sawa na Kenya na Uganda? Rasilimali ni sawa na Kenya na Uganda? Jeshi letu ni sawa na Kenya na Uganda?
Hapa utaona kuwa sisi ni watu tusiokosa sababu kwa madhaifu yetu. Mimi binafsi sioni sababu ya majambazi kutufanya tujifiche ndani kwa kuhofia mabasi yatatekwa. Huko Kenya, kwa wafanyabiashara watakubaliana na mimi, ukipita usiku, utaona Road Blocks na wanajeshi wakiwa na taa zao pembeni wapo pundamilia wakila maganda ya machungwa na hali ya usalama wa barabara ni shwari.
Sisi tunaotembea mchana, wastani wa ajali za barabarani kwetu bado upo juu na tunakufa mchana huo huo. Binafsi sielewi kuona POLISI NA JESHI WANAWEZAJE KUTUMIWA KUTULIZA MAANDAMANO LAKINI UKASHINDIKANA KUPATIKANA UTARATIBU WA KUTULINDA TUKAFANYA BIASHARA ZETU KWA UHURU.
Wengi yawezekana msione umuhimu wa hili, lakini mimi niliwahi kuwa mwajiriwa na mfanyabiashara kwa wakati mmoja. Biashara ilikuwa ngumu sababu ya utaratibu huu mbaya. Laiti kama tungefanya kama wenzetu, basi kulikuwa kuna uwezekano wa mimi kutoka DAR usiku, nikaingia Mombasa asubuhi, nikafunga mizigo yangu mchana kutwa, na usiku nikaingia tena safarini asubuhi ikanikuta Dar na nikafungua duka langu na kuendelea na biashara zangu. Lakini piga picha inanichukua muda gani kukamilisha zoezi lile lile kwa utaratibu huu uliopo?
Mimi nafikiri umefika wakati wa serikali kuacha hii primitive attitude na kuishi kwa malengo. Haiwezekani changamoto za namna hii ziitwe sababu muafaka za sisi kuwa nyuma na tukachekelea. Tanzania si kubwa kama Congo. Na nchi ikiwa kubwa ni more advantageous kuliko ingekuwa ndogo kwa hiyo serikali itutoe hapa bila visingizio.