Kwa ajili ya x-mas:Kufunguliwa kutoka nguvu za giza katika maisha ya ujana na ndoa!

Kimbweka

JF-Expert Member
Jul 16, 2009
8,597
1,683
Umewahi kutumia dawa yoyote ya kuongeza nguvu za kiume ili kukuwezesha kufanya mapenzi kwa muda mrefu na mtu asiyemke wako au mke wako zinazotokana na wachawi?
· Umewahi kutumia dawa yoyote ya kutengeneza ubikira bandia ambayo ilitoka kwa wachawi ili kumfurahisha unayefanya naye UZINZI au UASHERATI au MUMEO?

· Umewahi kufanya uzinzi au uasherati na mtu ambaye amewahi kutumia dawa hizo zilizoambatana na nguvu za mizimu Na nguvu za kichawi pasipo wewe kujua au kwa kujua kwamba amewahi kutumia dawa hizo?
Yako madawa mbalimbali yanayopita kwenye mikono ya wachawi na waganga wanaotumia nguvu za giza. Mfano wa madawa hayo ni yale ya kuongeza nguvu za kiume ili kumfanya mwanamume afanye mapenzi kwa muda mrefu, kuongeza urefu wa uume na mengine hutumika kutengeneza ubikira bandia au zile zinazo tumuka kutongozea. Madawa haya hutengenezwa KUZIMU, tena huwa yanapandikizwa nguvu za giza hasa mapepo. Haya mapepo huwa ni yale ya UKAHABA kama pepo na jini MAIMUNA pepo WARU na MWARU. Kusudi la madawa haya kupandikizwa nguvu za giza ni kwamba shetani anaompango wa kuangamiza kizazi cha wanadamu na hata kama watakuwepo anataka kuwafanya wawe ni wenye kuteseka na kuhangaika na kuteswa na nguvu za giza kila inapoitwa sasa hivi. Binti au kijana anapotumia dawa mojawapo ya hizo tajwa hapo juu huwa anakumbwa na mapepo pasipo yeye kujua kuwa alipotumia madawa hayo alipokea mapepo na akafanya nao agano. Kwa kufanya hivyo mabinti na vijana wengi wamejisajiri kuzimu kule kwa shetani. Kitu ambacho ni hatari sana kwa maisha yao.

Umewahi kutumia dawa yoyote ya kuongeza nguvu za kiume ili kukuwezesha kufanya mapenzi kwa muda mrefu na mtu asiyemke wako au mke wako zinazotokana na wachawi?
Vijana wengi sana wameingia katika shida ya kutooa au uchumba wao kuvunjika au kukataliwa upande wa mwanamke kila anapotaka kuoa, ndoa zao kuleta shida kwa sababu waliwahi kutumia MADAWA YA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME na dawa hizo walizozitumia zinatokana na wachawi. Kwani kijana anapotumia dawa hizo:-ANAKUNYWA PEPO LINALOTEMBEA NA HIYO DAWA. Kijana anapoona nguvu zimeongezeka, zile nguvu sio zake bali nguvu za lile pepo linalotembea na ile dawa. Kwani kijana huwa anajua kabisa kwamba yeye hana nguvu kiasi hicho ila ni kwa sababu ya dawa alizokunywa. Kwa maana hiyo basi nguvu zinakuwa ni za yule pepo anayeambatana na dawa hizo.

KIJANA HUYU ALIYEKUNYWA HAYO MADAWA ANAPOFANYA UZINZI AU UASHERATI NA BINTI, Kwa sababu nguvu si za huyu kijana bali pepo ambaye amempa kijana hizo nguvu, huyo binti huwa anakuwa kwa huo wakati anahusiana AU anafanya mapenzi na pepo huyo kwani ndiye mwenye hizo nguvu na wala si huyo kijana. Binti huyo akimwaga damu ili kuandika agano huwa anaandika agano na pepo hilo. Kwa namna hii huyo pepo anao uwezo wa kumuingilia huyo binti wakati wowote na ndio maana mabinti wengi sana huwa wanaingiliwa kimwili na mapepo wakiwa usingizini na wengine huwa wanachafuliwa kabisa wakidhani kuna mwanamume alikuja kulala kimapenzi usiku kumbe ni pepo. Kwa namna hiyo mabinti wengi sana wameibiwa mayai yao ya uzazi na yamehusishwa na nguvu za kipepo na hatimaye wamezaa watoto kuzimu, wengine hawazioni siku zao. Mabinti wenye shida hii huingiliwa kimwili na mapepo kwa nguvu hata kama hawataki.

JAWABU LA SHIDA HII KWA MABINTI LIKO KWA YESU PEKE YAKE. Mabinti hawa huwa ni lazima wavunje kwa damu ya Yesu kila nguvu ambayo inawafuatilia watu waliowahi kufanya mapenzi na mwanamume au kijana aliyewahi kutumia madawa ya kuongeza nguvu za kiume. Wakisha kulivunja agano hilo huwa wanaishi kwa raha na amani na baada ya wao kukubali kumpokea Yesu afanyike BWANA na MWOKOZI wa maisha yao MUNGU huwa anarudisha kizazi kilichopotea ndani yao.

JAMBO LA MUHIMU LA KUFANYA. Inawezekana unaposoma unagundua kuwa umewahi kufanya uasherati au umewahi kufanya uzinzi na kijana au na mwanamume ambaye amewahi kutumia nguvu za giza na unatamani sana Yesu akutoe kutoka katika hicho kifungo; mwambie Yesu akufungue kabisa kutoka katika kifungo hicho.
 
Na huu ujumbe ubadilishe maisha ya wengi walioathirika na nguvu za giza.
 
Mungu akubariki sana kwa ujumbe huu. Ni kweli DELIVERANCE ni muhimu kwa watu wote - endelea kuleta jumbe za namna hii ili wengi wafunguliwe.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom