Usilishe watu maneno. Weka ushahidi hapa kama Lissu alisema sababu pekee ya kumpitisha Lowasa kugombea urais ni umaarufu wake! Usivyo na aibu unamshukuru Mungu kutuepusha na hilo unalolisema, lakini huoni kama nchi inatembea kwenye laana kutokana na upuuzi wenu! Hii damu mnayoimwaga itawagharimu sana!Better the devil you know than the devil you don't, hakika mungu alituepusha na hili janga.
Hawa bado ni wachanga mno kuwakabidhi taifa.
Niliogopa sana siku nilipomsikia Sumaye akikili mwenyewe kuwa wapinzani hawana hazina ya viongozi wa kutosha na wenye uzoefu wa kuunda selikari.
Pili, Mh lissu alipodai kuwa waliamua kumpitisha Lowasa kutokana na kuwa maarufu sababu hicho ndio kilikuwa kigezo au kipaumbele muhimu kwa watanzania wakati huo.
Tatu, UKAWA kutaka kutumia katiba ya chadema kuunda selikari.
Mwisho ni Lowasa kushindwa kueleza ni wapi angetoa pesa ili kutoa elimu bure kwa watanzania,na amejipangaje kukabiliana na ufisadi nchini.
Kwa sasa hili limebaki kama genge la mbweha wanaogombea kuingia ndani ya zizi la mbuzi.
Aksante Mungu kwa kutuepusha na hili.