Kuzungumza na wataalamu wa Afya miaka mitatu bila Nyongeza ya Mishahara ni Ghiriba

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Nov 29, 2018
10,506
12,974
Naam,
bwana mkubwa leo ameezungumza na watalam wa Afya sijui anazungumza nini?
unazungumza na watu wenye njaa . watu hawa uliowatukana, kuwasimanga na kuwakebehe nchi nzima leo bila soni ati unawaita ikuli kwenda kuwaonesha maghorofa au kitu gani?
Mshahara sio hisani, upo kwa mujibu wa sheria hujaongeza kwa siku zote ati wajenga madaraja na kununua ndege alokwambia wanakula ndege nani?
 
yaani mioyo yao ingepasuka na kuona ndani ya watumishi wote wa sirikali NAMNA WALIVYO WAZALENDO INGEFURAHISHA
 
Kiukweli wafanya kazi wengi wa idara ya afya wamechoka sana. Wengi wamepoteza morale ya kazi. Utakuta mtu amemaliza masters tangu mwaka 2014 lakin mpka leo analipwa mshahara wa registrar( Daktari mwenye bachelor). Niliwahi kufanya kazi thetre moja hapa mjini, yaan mwanzo mpaka mwisho wa operation surgeon anatukana tuu kisa mshahara mdogo. Yaani kuna wakati wagonjwa wanasympathise wakidhani wao ndio chanzo. Pia, maslahi madogo ya wahudumu wa afya yamewafanya wafanya kazi wa afya kuanzia mlinzi wa geti la wodi mpaka specialist kuishi kwa kuscore almaarufu kama CCD( Chakula cha daktari).
So sad.
 
Back
Top Bottom