Wadau,
Huenda katika masuala ya kitaifa aliboronga na kuhujumu, LAKINI JIMBONI KWAKE NI LULU ISIYO KIFANI.
Tutafakari, tupime na kisha tujadili kwa mapana.
igunga ilikuwa wilaya haina maendeleo lakini katika uongozi wake amewafanyia makubwa
Hayo ndio mazingira ya bunge letu la sasa...dhana ya kazi ya mbunge kwa sasa ni "kutoa misaada", kujenga barabara etc na sio kusimamia serikali, kutunga sheria n.k.
Ndio maana wanagombania posho eti ni kwa ajili ya kuwasaidia wapiga kura wao!! Ndio maana hata mbunge asipochangia chochote mjengoni lakini hana wasiwasi anajua akirudi jimboni kwake na burungutu wananchi watajipanga mstari kuomba hela ya kula na nauli then kwisha kazi! Tusishangae watu kumlilia RA huko Igunga sababu aliweza kukidhi matarajio yao..MISAADA basi!
Mnakumbuka ile story ya Jambazi maarufi wa Jamaica DUDUZ? wakazi wa eleo alilokuwa anaishi yule mjamaa waligoma kutoa ushirikiano kwa polisi ili jamaa akamatwe kisa alikuwa ndio mfadhili wao, walifanya maandamano na kuweka bango moja limeandikwa "Jesus died for us, We will die for DUDUZ!"
Njaa mkuu haina heshima... kuna wakubwa wengine wanapishikwa na njaa kali wanashindwa kujizuia na kuwa kama watoto, wanaliaNilishangaa mababa mazima yanalia dahh kumbe za EPA alikuwa anakula na wapiga kura wake
Sio kweli Rostam hajamkodi mtu, ila wale walikuwa wanalia kwamba vibaruwa vyao ndio vimefikia tamati, au wewe haujui kama kuna watu wanaishi kwa kubomu? ile ni njaa inawasumbuwa.Rostam alikodisha watu wa kuzimia!
igunga ilikuwa wilaya haina maendeleo lakini katika uongozi wake amewafanyia makubwa
Njaa mkuu haina heshima... kuna wakubwa wengine wanapishikwa na njaa kali wanashindwa kujizuia na kuwa kama watoto, wanalia
Wednesday, 13 July 2011 20:57 0digg
Fidelis Butahe, Igunga
MJI wa Igunga na vitongoji vyake jana ulizizima, Mbunge wa Igunga Rostam Aziz alipotangaza kuachia ubunge wa jimbo hilo.Tukio hilo liliambatana na matukio kadhaa ya wananchi kuonyesha mabango yaliyokuwa na ujumbe tofauti, wengine kuzirai na mara kadhaa kumvamia ili asiendelee na uamuzi wake huo.
Mbunge huyo aliwasili Igunga saa saba mchana na baada ya kufika akaingia katika ofisi za CCM wilaya na kuzungumza na Baraza la Vijana la Wilaya. Aliwambia vijana hao kwamba, halikuwa lengo lake kuingilia mkutano wao bali alitaka kuzungumza na wazee.
Wakati akiingia katika mkutano huo, alipokewa na mabango yaliyokuwa na ujumbe uliosomeka kwamba "Kama wakikufukuza na sisi tutaondoka CCM, Igunga bila Rostam hakuna maendeleo, Rostam umeboresha huduma za kijamii Igunga, Mbunge wetu tunakupenda sana na Tuna imani na wewe.
Alitumia dakika saba kuzungumza na vijana kabla ya kukutana na viongozi wa CCM wa wilaya hiyo, akiwamo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazee, Kassim Ally. Akiwa na viongozi hao alizungumza nao kwa dakika 49.
Saa nane mchana aliondoka kwenda kwenye Ukumbi wa Sakao uliopo kilomita moja kutoka jengo la CCM wilaya hiyo.
Akiwa huko alipokewa na kisha kuanza kusoma hotuba yake ndefu ya kurasa takribani 10, lakini mara baada ya kutangaza kuachia nafasi zake ndani ya CCM huku akilengwa na machozi, baadhi ya wanachama walianza kulia huku wengine wakivamia meza kuu kumtaka mbunge huyo abadili uamuzi yake.
Wananchi hao walikuwa wamebeba mabango yenye maneno wao CCJ, sisi CCM, huku wakilitaja jina la Nape Nnauye, ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho.
Kufuatia tukio hilo Rostam alilazimika kuacha kuendelea kuisoma hotuba hiyo kwa dakika 15 baada ya kuvamiwa na kundi la baadhi ya vijana waliomtaka kusitisha uamuzi wake huo na kuwasihi wasimzuie, ili amalizie hotuba hiyo na baadaye watoe maoni yao.
Baada ya wanachama hao kutulia walipewa nafasi ya kutoa maoni yao wakasema kwamba akiendelea na uamuzi huo watarudisha kadi za CCM.
"Hatukubali wewe kwetu ni muhimu sana umetufanyia mengi, yanayosemwa yavumulie nakuomba ubadili msimamo wako na kama hautabadili msimamo huo hatuoni haja wa kubakia ndani ya chama cha CCM," alisema Hamis Kanama.
Watu wazirai
Baada ya Rostam kumaliza kusoma hotuba, Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Nzega, Daudi Ngutu, na Katibu wa Uchumi Kata ya Igoweko, Athuman Kanyama, walizirai na kupandishwa katika gari la Halmashauri ya kupelekwa hospitalini wakiwa katika hali mbaya.
Mjumbe wa Barala la Utekelezaji la UVCCM, Hussein Bashe, alikuwa miongoni mwa mashuhuda wa tukio la Rostam kutangaza kungatuka. Bashe ambaye alikuwa sambamba na Rostam tangu akiwa katika ofisi za wilaya aliliambia Mwananchi kuwa uamuzi wa Rostam ni mwiba mchungu kwa wananchi wa jimo hilo.
"Alichokifanya Rostam ni haki yake, lakini pamoja na hayo hawatendei haki wananchi wa Igunga, ila kwa kuwa ni maamuzi yake hakuna jinsi,"alisema Bashe na kusisitiza kwamba, CCM isipokuwa makini uchaguzi wa mwaka 2015 ukimalizika, utakiacha kikiwa chama cha upinzani na si chama tawala.
"Sekretarieti ya CCM itakabidhi chama kikiwa cha upinzani Watanzania wana matatizo mengi , lakini viongozi badala ya kuangalia hayo wanaendekeza siasa za chuki na kinafiki," alisema Bashe.
Rostam aondolewa na mabaunsa
Wanachama wa CCM waligoma kumruhusu Rostam kutoka katika ukumbi huo mpaka abadili uamuzi wake hali iliyosababisha vurugu na kufanya Askari wa kutuliza Ghasia(FFU) kuingilia kati.
Hata hivyo baadhi ya viongozi wa CCM walimtoa Rostam katika ukumbi huo kwa kuwatumia mabaunsa waliokuwa wanawazuia wananchi wasimzuie Rostam kuondoka.
Wakati Rostam akiwa njiani kuondoka kwenda Dar es Salaam wanachama wengine ambao ni Katibu mwenezi kata ya Chabutwa, Athumani Mihayo, Catherine Mabula na Zainabu Athumani walizirai.
Viongozi wa CCM waliokuwapo
Viongozi wa CCM wengi kutoka wilaya zote za mkoa wa Tabora walihudhuria ambao ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Igunga, Katibu Tawala wa Wilaya, Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Tabora, wajumbe wa kamati ya siasa wa wilaya na Baraza la Wazee la Wilaya na Mbunge wa Viti Maalumu, Munde Tambwe
Wadau wa JF, mimi binafsi nimepigwa na bumbuwazi baada ya kusikia watu wamezirai eti kisa ni kujiuzulu kwa Mh.Rostam Aziz,hebu naombeni mnisaidie hii maana yake nini???Najua Igunga kuna wana JF itakuwa vyema mkitupa ukweli wa mambo kuhusu taarifa hizi za kuzirai kama zina ukweli wowote au la!!
igunga ilikuwa wilaya haina maendeleo lakini katika uongozi wake amewafanyia makubwa
kuna ukweli maana wakati jamaa katangaza tu kuwa kang'atuka, ule ukumbi ulizizima kwa simanzi na sintofahamu. Niliona (kupitia tv) wamama kwa wababa wakilia. And i ask to my self, what a wonderful world!Hii habari sioni kama inaweza kuwa na ukweli ndani yake,
Wadau wa JF, mimi binafsi nimepigwa na bumbuwazi baada ya kusikia watu wamezirai eti kisa ni kujiuzulu kwa Mh.Rostam Aziz,hebu naombeni mnisaidie hii maana yake nini???Najua Igunga kuna wana JF itakuwa vyema mkitupa ukweli wa mambo kuhusu taarifa hizi za kuzirai kama zina ukweli wowote au la!!