The iron batterfly
JF-Expert Member
- Jul 31, 2018
- 1,952
- 2,521
Habari za mchana wanaJf.Swaumu njema kwa walofunga na lunch njema kwa sie wa imani tofauti.
Iko hivi Kuna rafiki yangu,yeye alizaliwa peke yake upande wa mama yake,Baba yake alimwacha yeye na mamake angali akiwa tumboni kwa mama,so hana mahusiano na upande wa baba yake .Mama yake bahati mbaya alishafariki akiwa shule ya msingi,so kwa sehemu kubwa alilelewa na Bibi na Babu mzaa mama.Uzuri Babu yake alikuwa na ajira nzuri na Bibi alikuwa mjasiriamali mdogo.
Upande wa Bibi na Babu mzaa mama walijaliwa kuwa na watoto saba akiwemo mama yake huyu rafiki yangu.Bahati mbaya mama yake na nduguze wawili waliokuwa wanamsapoti nao walishatangulia mbele ya haki kitambo.Hivyo walibaki watoto wa 4 wa Babu na Bibi yake,wakike mmoja na wakiume wa 3,ambao kwa sehemu kubwa wote baada ya kumaliza elimu ya msingi walikataa kuendelea na masomo ingawa baba yao(Babu yake)alikuwa na uwezo wa kuwasomesha.
Hivyo kwa sehemu kubwa Bibi na Babu yake walijitahidi kumsomesha huyu mjukuu wao,kwakuwa alikuwa na Nia ya kusoma.Wakati watoto wao wale wa 4 wakiwa busy tu mjini wakijaribu hili na lile .Rafiki huyu alifanikiwa kusoma hadi level ya chuo kikuu,na akafanikiwa kufaulu vyema.Wakati huo Hawa watoto wanne wakiwa busy na maisha yao na wakiwa wana watoto kadhaa Kila mmoja.
Baada ya kumaliza elimu ya chuo ,mjukuu huyu alifanikiwa kuajiriwa kwenye kampuni Fulani mkoa Fulani Kanda ya ziwa,na akawa anawasapoti Bibi na Babu yake kwani ndio waliomhangaikia tangu mama yake aondoke duniani.Bahati mbaya hawa Bibi na Babu yake nao wameshatangulia mbele ya haki Sasa,wakiacha nyumba mbili walizoweza Jenga.
Baada ya wazee wale kufariki wale watoto wote wanne wamerejea kwenye mji wa wazee wao,wakagawana vyumba kwenye nyumba moja na nyingine wameipangisha wakipokea kodi,na huyu mjukuu hawampi hata senti.Ila hilo siyo dhumuni la huu uzi.
Tatizo Hawa watoto wanne ambapo ni watu wazima wenye kuanzia miaka 40 na kuendelea,wanamtaka huyu mjukuu,awe anawatumia hela ya chakula,maji,umeme, hospital wakiumwa na kuwasomeshea watoto zao kwani walezi wake (Bibi na Babu)walipokuwa hai alikuwa anawahudumia yeye,ila baada ya kufariki akawakabidhi Hawa watoto nyumba na kuendelea kujiimarisha kwenye mji wake.
Sasa suala ni je ni sahihi,yeye awahudumie hao wajomba na shangazi,ilhali ni watu wazima,hawana ulemavu wowote,wana nyumba hizo mbili za urithi na wanapokea kodi.Wote hao hawafanyi kazi wanategemea hizo nyumba za urithi kuishi.Wanamlaumu kuwa Ana roho mbaya,asipowatumia hela,je ni sahihi?isitoshe wanalalamika kuwa wazazi wao ndio wamemsomesha huyu mjukuu.
Iko hivi Kuna rafiki yangu,yeye alizaliwa peke yake upande wa mama yake,Baba yake alimwacha yeye na mamake angali akiwa tumboni kwa mama,so hana mahusiano na upande wa baba yake .Mama yake bahati mbaya alishafariki akiwa shule ya msingi,so kwa sehemu kubwa alilelewa na Bibi na Babu mzaa mama.Uzuri Babu yake alikuwa na ajira nzuri na Bibi alikuwa mjasiriamali mdogo.
Upande wa Bibi na Babu mzaa mama walijaliwa kuwa na watoto saba akiwemo mama yake huyu rafiki yangu.Bahati mbaya mama yake na nduguze wawili waliokuwa wanamsapoti nao walishatangulia mbele ya haki kitambo.Hivyo walibaki watoto wa 4 wa Babu na Bibi yake,wakike mmoja na wakiume wa 3,ambao kwa sehemu kubwa wote baada ya kumaliza elimu ya msingi walikataa kuendelea na masomo ingawa baba yao(Babu yake)alikuwa na uwezo wa kuwasomesha.
Hivyo kwa sehemu kubwa Bibi na Babu yake walijitahidi kumsomesha huyu mjukuu wao,kwakuwa alikuwa na Nia ya kusoma.Wakati watoto wao wale wa 4 wakiwa busy tu mjini wakijaribu hili na lile .Rafiki huyu alifanikiwa kusoma hadi level ya chuo kikuu,na akafanikiwa kufaulu vyema.Wakati huo Hawa watoto wanne wakiwa busy na maisha yao na wakiwa wana watoto kadhaa Kila mmoja.
Baada ya kumaliza elimu ya chuo ,mjukuu huyu alifanikiwa kuajiriwa kwenye kampuni Fulani mkoa Fulani Kanda ya ziwa,na akawa anawasapoti Bibi na Babu yake kwani ndio waliomhangaikia tangu mama yake aondoke duniani.Bahati mbaya hawa Bibi na Babu yake nao wameshatangulia mbele ya haki Sasa,wakiacha nyumba mbili walizoweza Jenga.
Baada ya wazee wale kufariki wale watoto wote wanne wamerejea kwenye mji wa wazee wao,wakagawana vyumba kwenye nyumba moja na nyingine wameipangisha wakipokea kodi,na huyu mjukuu hawampi hata senti.Ila hilo siyo dhumuni la huu uzi.
Tatizo Hawa watoto wanne ambapo ni watu wazima wenye kuanzia miaka 40 na kuendelea,wanamtaka huyu mjukuu,awe anawatumia hela ya chakula,maji,umeme, hospital wakiumwa na kuwasomeshea watoto zao kwani walezi wake (Bibi na Babu)walipokuwa hai alikuwa anawahudumia yeye,ila baada ya kufariki akawakabidhi Hawa watoto nyumba na kuendelea kujiimarisha kwenye mji wake.
Sasa suala ni je ni sahihi,yeye awahudumie hao wajomba na shangazi,ilhali ni watu wazima,hawana ulemavu wowote,wana nyumba hizo mbili za urithi na wanapokea kodi.Wote hao hawafanyi kazi wanategemea hizo nyumba za urithi kuishi.Wanamlaumu kuwa Ana roho mbaya,asipowatumia hela,je ni sahihi?isitoshe wanalalamika kuwa wazazi wao ndio wamemsomesha huyu mjukuu.