Serikali kupitia kampuni yake ya mashamba ya miffugo, NARCO imealika wawekezaji toka nje na ndani ya nchi kuwekeza katika shamba la mifugo la Ruvu, mkoa wa Pwani. shamba hilo lina uwezo wa kufuga ng'ombe 17,000.
Tofauti na sekta za madini, nishati na mawasiliano , sekta ndogo ya mifugo haihitaji teknolojia na utaalamu tusio nao Wa-Tanzania. Hivyo, kwa nini sekta ndogo kama hizo zisiachiwe kipekee (reserved) kwa wananchi hata baada ya miaka 51 ya uhuru? Mbona nchi nyingine wanafanya hivyo. Hatujifunzi toka Zimbabwe?
Kama ni suala la mtaji hilo pia si hoja. NSSF wamewekeza katika mkonge na kufanikiwa kuongeza uzalishaji.Kwa nini mashirika kama hayo yasiwekeze katika Ruvu Ranch? Kwani wananchi hawawezi kwekeza kupitia soko la mitaji (DSE) ukiwekwa mpango maalumu?
Yawezekana lengo ni kunufaisha watu wachache, lakini Wa-Tanzania tumechoka kubebwa na wazungu, waarabu na waasia katika mambo ya fedha na uchumi wetu.Inaleta kudharauliwa, kuonekana kukubali sisi ni wato watoto tu. Tuamue sasa kwamba hata katika uwekezaji tunaweza, hata kuwekeza kwa wazungu, waarabu na waasia.
Tofauti na sekta za madini, nishati na mawasiliano , sekta ndogo ya mifugo haihitaji teknolojia na utaalamu tusio nao Wa-Tanzania. Hivyo, kwa nini sekta ndogo kama hizo zisiachiwe kipekee (reserved) kwa wananchi hata baada ya miaka 51 ya uhuru? Mbona nchi nyingine wanafanya hivyo. Hatujifunzi toka Zimbabwe?
Kama ni suala la mtaji hilo pia si hoja. NSSF wamewekeza katika mkonge na kufanikiwa kuongeza uzalishaji.Kwa nini mashirika kama hayo yasiwekeze katika Ruvu Ranch? Kwani wananchi hawawezi kwekeza kupitia soko la mitaji (DSE) ukiwekwa mpango maalumu?
Yawezekana lengo ni kunufaisha watu wachache, lakini Wa-Tanzania tumechoka kubebwa na wazungu, waarabu na waasia katika mambo ya fedha na uchumi wetu.Inaleta kudharauliwa, kuonekana kukubali sisi ni wato watoto tu. Tuamue sasa kwamba hata katika uwekezaji tunaweza, hata kuwekeza kwa wazungu, waarabu na waasia.