Tatizo la kuwashwa mwilini baada ya kuoga: Fahamu chanzo, ushauri na tiba

Lisa victor,
Pole sana, hilo tatizo kitaalam linaitwa AQUAGENIC URTICARIA, ni kwamba mwili wako unakuwa na allergy ya maji, nijuavyo mimi tatizo hili halina tiba ila unaweza kulipunguza sana kwa kuoga maji ya moto au vugu vugu na pia hakikisha unaoga kwa muda mfupi kadiri iwezekanavyo na jitahidi ukishamaliza tu kuoga hakikisha mwili umeufunika vizuri usipate upepo au baridi,( nunua bathrobe) adha ya muwasho ikizidi tafuta strong anti allergies kama LORATIDINE au nyingine yeyote, nirudie kukupa pole sana
 
Uwiiii jamani kumbe kuna wenzangu, nilijua hii ni shida yangu pekeangu, mi toka nimejitambua/ nimejijua nawashwa sana nikioga hasa nikijisugua, nimabadili maji sana maana nimeishi mikoa mingi lakini haisaidii chochote.

nimebadili sana sabuni wapi, nimeacha maji ya baridi naoga ya uvuguvugu au moto muwasho unapungua but bado utawashwa tu, nimebadili material ya vitambaa ninavyoogea haisaidii, sasa natumia kitaulo laini kabisa ule ulaini wa mwisho lakini wapi, na nikioga nakianika juani haisaidii, nimeenda hosp hadi nimechoka! Lisa victor i feel you ☹
 
Uwiiii jamani kumbe kuna wenzangu, nilijua hii ni shida yangu pekeangu, mi toka nimejitambua/ nimejijua nawashwa sana nikioga hasa nikijisugua, nimabadili maji sana maana nimeishi mikoa mingi lakini haisaidii chochote, nimebadili sana sabuni wapi, nimeacha maji ya baridi naoga ya uvuguvugu au moto muwasho unapungua but bado utawashwa tu, nimebadili material ya vitambaa ninavyoogea haisaidii, sasa natumia kitaulo laini kabisa ule ulaini wa mwisho lakini wapi, na nikioga nakianika juani haisaidii, nimeenda hosp hadi nimechoka! Lisa victor i feel you ☹
Duuh tupo wengi Mkuu. But mim huwa nikwa msimu, alafu nikianza dalili za kuashwa huwa najiskia vibaya kwenye mind. Yaan nawaza kila kitu ni kichafu. Nilisha acha kujisugua na aina yoyote ile ya kitu mwilini mwangu pale napooga. Hii ndo dawa iliyosababisha kutoka daily kuwasha na sasa ni kwa msimu
 
Mkuu unaweza kutumia medicated soap ya Tetmosol ziko maduka ya dawa makubwa ni kiboko ya muwasho nyingi nilizotumia ni za Nigeria na India.
 
Nini kinasababisha kuwashwa mwili baada ya kutoka kuoga? Tatizo limenisumbua miaka 10 sasa.. Nikijisugua ndo nawashwa kabisa, nisipojisugua nawashwa kidogo afadhali lkn mtu huwezi kuoga bila kujisugua. Najisugulia kitambaa laini kabisa, nikitoka kuoga nachanganyikiwa kwa kuwashwa mno na daktari aliniambia ninywe piriton kila kabla sijatoka kuoga na nikitoka kuoga lkn haikunisaidia kabisa.

Naombeni ushauri nifanye nn manake nimekata tamaa sina raha ya kushika maji hata kidogo. Mvua ikininyeshea nawashwa haswaa. Mwili unatutumka unavimba kila nikijikuna.

Aisee, nimekumbuka mbali sana, huo ugonjwa ulinitesa sana, mpaka nikawa nahisi ninaumwa UKIMWI. lakini kwa sasa nilipona baada ya kupitia mateso makubwa. Ilikua nikitoka kuoga nawashwa mwili mzima, hasa kwenye mapaja na miguu, pia kuzunguka kiuno.

Nilishawahi kuandika tangazo kama hili kuomba msaada wa kupata Ushauri nifanyeje nipate nafuu. Niliambiwa SCABIES kama ulivyoambiwa wewe hapa, nikatafuta hiyo SCABOMA nikawa napaka kila nikitoka kuoga, Pia nilishauriwa nifue nguo zangu zote kwa maji MOTO ili bacteria wa SCABIES wafe, pia nizifungie nguo katika mfuko wa nylon (PLASTIC) ili bacteria wakose hewa wafe hayo yote ninifanya.

Lakin haikusaidia au ilisaidia in long run, yaan labda matibabu hayo yalikua yanasaidia kwa taratibu sana. Mpaka sasa sikumbuki hali ile iliisha lini maana ilikua inapungua taratibu taratibu sana. Nilishaenda hadi kwa wamasai wakanipa dawa za kupaka zina harufu mbaya sana, nilipaka lakini hazikuonyesha kusaidia kabisa.Hata ngozi ya maeneo yaliyokua yanapata adha hiyo ya miwasho haikua na muonekano mzuri, kiukweli niliogopa hata kupima nikajua lazima ntakua VICTIM.

Kuna Siku nikaenda kwenye Hospital moja inaitwa SINO Hospital, ipo SINZA mapambano, kupima full blood picture nione labda Vitu kama CD4 kwa uwelewa mdogo nilionao vinaweza vikanipa picha halisi ya afya yangu, lakin yalitoka fresh, component zote za damu zipo OK.

Wife alipopata ujauzito baada ya kukaa muda mrefu tunapiga gem bilabila, Hatimae akapata Mimba, alivyopima akawa NEGATIVE ndipo nikapata HOPE niko sawa, nami ndio nikaenda sasa Kupima. lakin wakati huo miwasho imeshakwisha. Mwili kuna kipindi huwa unawashwa lakini sio kwa kiwango kile.

Kwa hiyo ndugu mtoa mada, pambana sana. Fanyia kazi ushauri unaopewa hapa, na wewe jiongeze kwa tiba mbadala za mitishamba.
 
Pole sana mkuu. Hata Mimi ni mhanga wa kadhia hiyo!! Tafadhari ukipata utatuzi naomba uni tag!!
Mwanzoni hata Mimi nilikuwa mhanga wa tatizo hili, ili kuepukana nalo baada ya kuoga tu jifute maji na upake mafuta ya mgando hapo utakuwa umemaliza muwasho labda iwe tofauti kwa wengine.
 
Hata Mimi ni muhanga wa hilo tatizo kwa miaka kama mitano hivi
Sometimes huwa nahisi labda aina ya maji nayo inachangia kwa sababu nikiwa Dar nikioga siwashwi Ila sasa nikiwa Dodoma nikioga lazima niwashwe
Ni kweli maji ya moto ama vuguvugu yanapunguza muwasho kiasi flan
 
Duuh tupo wengi Mkuu. But mim huwa nikwa msimu, alafu nikianza dalili za kuashwa huwa najiskia vibaya kwenye mind. Yaan nawaza kila kitu ni kichafu. Nilisha acha kujisugua na aina yoyote ile ya kitu mwilini mwangu pale napooga. Hii ndo dawa iliyosababisha kutoka daily kuwasha na sasa ni kwa msimu
Yaani kama mimi mkuu! Ila mimi ninapooga asubuhi ndiyo hali inakuwa mbaya zaidi! Hizo hisia mbaya ndiyo usiombe! Hasa huwa nawashwa miguuni! Ninachokifanya huwa ni kujikausha kwa taulo kisha najipuliza na hot blower,then nalala kitandani na kujifunika kwa blanket,taratibu hali inaanza kurudi kawaida hadi inaisha kabisa! Ila nikifanya mazoezi ama kazi nikatoka jasho ndiyo nikaoga na kulala muda huo huo(hasa usiku) hilo tatizo silipati sana! Tatizo kubwa hili kumbe!!
 
Uwiiii jamani kumbe kuna wenzangu, nilijua hii ni shida yangu pekeangu, mi toka nimejitambua/ nimejijua nawashwa sana nikioga hasa nikijisugua, nimabadili maji sana maana nimeishi mikoa mingi lakini haisaidii chochote, nimebadili sana sabuni wapi, nimeacha maji ya baridi naoga ya uvuguvugu au moto muwasho unapungua but bado utawashwa tu, nimebadili material ya vitambaa ninavyoogea haisaidii, sasa natumia kitaulo laini kabisa ule ulaini wa mwisho lakini wapi, na nikioga nakianika juani haisaidii, nimeenda hosp hadi nimechoka! Lisa victor i feel you ☹
tumia Scobama lotion na uhakikishe umefungua nguo zote na maji ya moto.
 
Hata Mimi ni muhanga wa hilo tatizo kwa miaka kama mitano hivi
Sometimes huwa nahisi labda aina ya maji nayo inachangia kwa sababu nikiwa Dar nikioga siwashwi Ila sasa nikiwa Dodoma nikioga lazima niwashwe
Ni kweli maji ya moto ama vuguvugu yanapunguza muwasho kiasi flan
Hata mimi dar huwa siwashwi kihivo..ila nikienda mikoani hali inakuwa mbaya sana
 
Wakuu nawashukuru sana maana nina hili tatizo zaidi ya miaka 10 sasa, ila leo nimeoga nimewashwa sana ..ndo nikapata wazo la kusearch google mara paa nakutana na huu uzi ..ofcoz nimepata pakuanzia ..nawashukuru sana
 
Back
Top Bottom