Bushesha jr
JF-Expert Member
- Apr 26, 2020
- 677
- 690
Hii tabia ya kuanza kufanya uchambuzi wa kuwalinganisha viongozi wetu wakuu naona ingali bado inaendelea, binafsi nilimsikia Mhe. Rais mara kadhaa akikemea jambo hili lakini bado kuna watu tena wateule wa rais wanaendelea na hii tabia
Uwaziri ni cheo cha heshima sana sasa inakuwaje mtu anaacha kazi za uwaziri na kuanza kuzungumzia vitu visivyohusika?
Tumesikitishwa sana na kitendo cha Waziri Fedha tena kwenye hotuba nyeti ya bajeti anaacha kufafanua Mambo muhimu ya kibajeti ili wananchi waelewe anaanza kudemka
Kwa mtu unayefikiri kwa kina huwezi kuanza kuwachambua Marais viongozi wako waliokuamini kwa muda mrefu na huku wew ukiwa mteule wao hayo siyo maadili kabisa. Waziri Mwigulu kama anataka kuwachambua Marais wetu aachie ngazi Kwanza
Ni afadhali angeishie kwenye vibwagizo vya yanga tu japo hata hivyo navyo havifai kwa sababu tukio hilo lilikuwa nyeti mno likifuatiliwa na mamilioni ya watu walioko ndani na nje ya nchi sasa kwanini mtu unashindwa kuwa serious na kazi
Inasikitisha sana labda atajirejebisha lakini ametukosea sana
Mungu ibariki Tanzania
Uwaziri ni cheo cha heshima sana sasa inakuwaje mtu anaacha kazi za uwaziri na kuanza kuzungumzia vitu visivyohusika?
Tumesikitishwa sana na kitendo cha Waziri Fedha tena kwenye hotuba nyeti ya bajeti anaacha kufafanua Mambo muhimu ya kibajeti ili wananchi waelewe anaanza kudemka
Kwa mtu unayefikiri kwa kina huwezi kuanza kuwachambua Marais viongozi wako waliokuamini kwa muda mrefu na huku wew ukiwa mteule wao hayo siyo maadili kabisa. Waziri Mwigulu kama anataka kuwachambua Marais wetu aachie ngazi Kwanza
Ni afadhali angeishie kwenye vibwagizo vya yanga tu japo hata hivyo navyo havifai kwa sababu tukio hilo lilikuwa nyeti mno likifuatiliwa na mamilioni ya watu walioko ndani na nje ya nchi sasa kwanini mtu unashindwa kuwa serious na kazi
Inasikitisha sana labda atajirejebisha lakini ametukosea sana
Mungu ibariki Tanzania