Hapa nyumbani nina banda la uwani ambalo natumia kama stoo sasa njiwa wanaweka makazi yao sehemu ya juu ndani ya fisher board..naombeni njia ya kuwafukuza kwani sijui wametokea wapi na wanachafua mazingira na uchafu wao..
hao ni ndege wazuri saana, mimi binafsi nawapenda saana ndege hao, na nina mpango kabambe wa kuwafuga,tatizo nahofia hawa kunguru weusi, maana ni waharibifu saana na serikali inaleta usanii ktk kupambana nao eti wanaita mpango wa kuwaangamiza, mara utasikia zoezi letu limefanikiwa tumewaangamiza ,mmhh wakati bado wapo kibao na wanazaana ile mbaya. kuhusu hao njiwa nakushauri tengeneza banda mahususi kwa ajili yao , kisha liweke vzr njee, na wakishaa zoea kuingia kwenye banda basi ziba dari lako kusiwe na sehemu ya wao kuweza kuingia kisha wahudumie kwa kuwapa maji na chakula, kila unapowapa chakula piga mluzi wakizoea utafurahi kuwa nao.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.