Kuwafariji watu wa Chato sawa lakini si wale wa Kagera!

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Friday, December 30, 2016
Rais Magufuli awafariji majirani Chato

Magu+Chato.jpg



Kwa ufupi
Familia ya Manyama imefiwa na baba yao, Mbabe Manyama aliyekuwa maarufu eneo la Chato na familia ya Lufunga ambayo iliondokewa na baba yao, Mchele Lufunga.


By Baraka Rwesiga, Mwananchi brwesiga@mwananchi.co.tz
Chato. Rais John Magufuli, ametumia mapumziko yake ya mwisho nwa mwaka kuwatembelea na kuwafariji majirani zake waliofiwa na baba zao Desemba 27.

Familia ya Manyama imefiwa na baba yao, Mbabe Manyama aliyekuwa maarufu eneo la Chato na familia ya Lufunga ambayo iliondokewa na baba yao, Mchele Lufunga.

Rais Magufuli ambaye yuko nyumbani kwake Chato mkoani Geita, ametoa ubani wa Sh1 milioni na ng’ombe mmoja kwa kila familia.

Familia ya kwanza aliyoitembelea ni ya Lufunga ambaye ni jirani yake wanayetenganishwa na ukuta aliyefariki dunia katika Hospitali ya Wilaya ya Chato alikokuwa akipatiwa matibabu.

Pia, Rais Magufuli aliitembelea familia ya Manyama ambaye alifariki nyumbani kwake. Licha ya kuwa maarufu wilayani humo, Manyama pia alikuwa rafiki mkubwa wa baba mzazi wa Rais Magufuli.

“Msiba kama huu wa kufiwa na mzazi ambaye ni nguzo ya familia unapotokea, familia nyingi huanza kufarakana na kugawanyika. Naomba msifarakane ninyi wenyewe kwa wenyewe wala msifarakanishwe na watu,” amesema Rais Magufuli alipokuwa akiifariji familia ya Mbabe.

Akitoa shukrani kwa Rais, mdogo wa marehemu Lufunga, Charles Lufunga amesema familia imefarijika kutembelewa na kiongozi huyo na kuahidi kudumisha umoja na ushirikiano.

Mdogo wa Manyama, Theodatus Manyama amemhakikishia Rais Magufuli kuwa familia hiyo itazingatia ushauri wake kwa kuendeleza umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwao na kwa wote wanaowazunguka.
 
tulifanya makosa makubwa sana katika uchaguzi 2015, hatutakiwi kurudia makosa. kuna watu wameumbwa kuwa viongozi na wanaweza, ila kuna watu wengine wameumbwa kwa kazi nyingine tu ila si kuwa viongozi. wapo viongozi wengi tu serikalini ambao wameshika nyadhifa ambazo Mungu hakuwaumba nazo na wanalazimisha tu labda kwasababu imewadondokea kama ngekewa, kama wanafanyia majaribio kwenye maisha ya watu vile. hata hivyo, nampongeza magufuli, na ninamwombea Mungu afanye kazi kwa mapenzi ya Mungu.
 
tulifanya makosa makubwa sana katika uchaguzi 2015, hatutakiwi kurudia makosa. kuna watu wameumbwa kuwa viongozi na wanaweza, ila kuna watu wengine wameumbwa kwa kazi nyingine tu ila si kuwa viongozi. wapo viongozi wengi tu serikalini ambao wameshika nyadhifa ambazo Mungu hakuwaumba nazo na wanalazimisha tu labda kwasababu imewadondokea kama ngekewa, kama wanafanyia majaribio kwenye maisha ya watu vile. hata hivyo, nampongeza magufuli, na ninamwombea Mungu afanye kazi kwa mapenzi ya Mungu.
Hata msipoipigia kura CCM inashinda sijui ni maajabu gani hutokea.
 
Kutoka kuwa wahanga wa tetemeko la ardhi mpaka kuwa wahanga wa fedha za misaada
 
Hii ni kwa sababu chato hawana kijiji kiitwacho katelelo wala mto unaoitwa ngono.mchuma janga hula na wakwao bro kajiokotea embe dodo mchangani acha ale na nduguze na wahaya na mabalaa yao acha wale na ndugu zao.
 
hii imenikumbusha ile simulizi ya kwenye biblia ya yule mwanamke msamaria ambaye alitaka Yesu amponye mwanae. Yesu akamjibu "chakula cha watoto huwez ukawapa mbwa" lakin mwanamke was very wise akamjibu "ila hata mbwa huokota makombo chini ya meza ya bwana wake"
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Subirini akija kuomba kura,mwambieni ajipigie mwenyewe ,mwambieni afanyekazi ache kutafuta vya burebure
 
tulifanya makosa makubwa sana katika uchaguzi 2015, hatutakiwi kurudia makosa. kuna watu wameumbwa kuwa viongozi na wanaweza, ila kuna watu wengine wameumbwa kwa kazi nyingine tu ila si kuwa viongozi. wapo viongozi wengi tu serikalini ambao wameshika nyadhifa ambazo Mungu hakuwaumba nazo na wanalazimisha tu labda kwasababu imewadondokea kama ngekewa, kama wanafanyia majaribio kwenye maisha ya watu vile. hata hivyo, nampongeza magufuli, na ninamwombea Mungu afanye kazi kwa mapenzi ya Mungu.

Kwani bukoba mlimpa kura?akina Lwakatare ni chama gani?si mumuombe lowassa na mbowe wakupeni msaada mnaoutaka?nani aliekwambia serikali inajenga nyumba binafsi za matetemeko duniani?
 
Mlivunja nyumba zenu kwa kutegemea kujengewa?tetemeko ni janga la kitaifa,kinachotakiwa kurekebishwa au kujengwa ni barabara,shule maofisi ya umma na hospitali,nani aliesema serikali ikujengee nyumba baada ya tetemeko?tatizo mlijiachia yule mama aliepewa msaada na rais mwanzoni kabisa alijitambua na alisoma nyakati na ndio maana akaanza kujenga nyumba yake mwenyewe na Rais akamsaidia,tatizo mlijipweteka.
 
Back
Top Bottom