STRATON MZEE
Member
- Jan 4, 2012
- 59
- 17
Wajameni kuna hili jambo ambalo limetokea kwa hawa jamaa wanaojiita CCM kuwaengua wazee waastaafu kutoka katika NEC yao, na kuwaundia baraza lisilo na meno, yaani baraza la washauri. Mi nionavyo, hii ni ushindi kwa mafisadi wanaoutaka urais 2015, hasa ukizingatia kuwa wazee hawa wakianzia na Nyerere mwenyewe, ndo waliokuwa wanaongoza harakati za kuamua nani awe rais na nani asiwe rais. Kama tutakumbuka, Mwl. aliwahi kumwambia mmoja wa makada wa CCM ambaye anatajwa kwenye harakati za kuwania urais 2015 kuwa hafai kuwa kiongozi hapa duniani. Hivyo, ili harakati zao za kuingia ikulu zitimie, ilikuwa ni lazima hawa wazee waliokuwa wanaweka kauzibe waondolewe kwenye vikao vya maamuzi. na kwa hilo wamefanikiwa. Wajameni! Kuna ahueni yoyote ambayo CCM wameipata kutokana na kuwaondoa wazee hawa?