Kuwaambia watu wenye kesi za uhujumu uchumi watoe hela Serikalini ili waachiwe nakuchukulia kama ni kuhalalisha Serikali kupewa rushwa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,770
Ikitokea kwamba mwendesha mashitaka anamfutia mtu kesi baada ya kupewa fedha na mtuhumiwa, hiyo ni rushwa. Na inakuwa rushwa si kwa kuwa mwendesha mashitaka kafaidika na ile fedha kibinafsi badala ya serikali ili kumwachia huru mtuhumiwa, inakuwa ni rushwa kwa kuwa haki (justice) imepindishwa kwa mtuhumiwa kununua uhuru kinyume na sheria. LInakuwa kosa hata kama mwendesha mashitaka atasema nilitumia zile hela kuchangia mradi wa maji kijijini kwangu.

Sasa hebu tubadili picha, badala ya mwendesha mashitaka, tuiweke serikali. Je inakuwa halali kwa serikali kuomba "hongo" kwa watuhumiwa ili waachiwe huru? Kanuni ni zile zile, tatizo hapa ni kwamba hii "hongo" inahalalishwa na serikali. Huo ndio ukweli, mpende msipende.

Hakuna tofauti na trafiki kukukama kwa makosa barabarani, ukampa hela ili akuachie yaishe. Huyo trafiki ni mpokea rushwa. Sasa hapa serikali imekuwa kama trafiki mpokea rushwa, hata kama hiyo hela ni kwa ajili ya mboga nyumbani!

Na mbaya zaidi kuna kipengele cha haki katika sheria. Hawa ni watuhumiwa. Serikali inajuaje kama wasingeshinda kesi zao? Kuwaambia watoe "hongo" ni namna fulani ya kitu kinaitwa "blackmail". Ni wazi kwamba hata kama wanajua wangeweza kushinda kesi zao wataomba msamaha yaishe na kutoa hiyo "hongo" kwa serikali.

Hii serikali ina mambo ya ajabu sana.

Update:
Zaidi ya suala la serikali kuhalalisha kupewa rushwa katika kesi za namna hii, suala jipya lililojitokeza ni serikali kuwaonea watu na kuwafanya wanunue uhuru wao kwa lazima, wapende wasipende, hata kama hawana kosa na serikali inajua kwamba uwezekano wa kuwatia hatiani ni mdogo sana. Serikali inachofanya ni kuchelewesha makusudi kesi za namna hii, hasa kwa wale wanaobambikiwa haya mashitaka, kwa namna tu ya kuwakomoa kutokana na sababu za kisiasa.

Na mbaya zaidi wigo wa kesi za uhujumu uchumi unapanuliwa kisiasa hadi kufikia vitu kama kupiga picha ya barabara mbovu. Sasa nikipiga picha ya barabara mbovu sijui serikali itanitoza shilingi ngapi ili niachiwe huru "kwa makubaliano".

Kitu cha aibu sana ni kuona mhimili wa mahakama unashiriki katika ubakaji huu wa haki za raia na kutumiwa kuuhalalisha.
 
Kesi nyingi za wahujumu uchumi huisha kihuni kwa mafisadi kuhonga mfumo wa mahakama

Hii sheria ya kufanya mashauriano na Dpp ni nzuri mno
Ni swala la muhujumu uchumi kuamua afanye

Tanzania sio Nchi ya kwanza kufanya hivi huu mfumo unatumika pia kwa Nchi kubwa duniani kama USA na Russia
 
Wakikiri Na Kulipa Pesa Nashauri DPP Uwaachie
Taarifa Mpaka Sasa Hivi Mwitikio Ni Mkubwa Sana Watu Wengi Sana Wamerudisha Pesa.
Yaani Corruption Division Court Itakuwa Haina Wateja
Zaidi Itangoja Wapya Tu
 
Lakini Hiyo Anayolipa Ni Hela Ya Serikali, Na Inarudi Kwa Serikali Mwenye Nayo, Maana Huyo Anayerudisha Aliikwiba,.
 
Tanzania sio Nchi ya kwanza kufanya hivi huu mfumo unatumika pia kwa Nchi kubwa duniani kama USA na Russia

Nchi nyingine zinafanya hivyi ukitiwa hatiani, sio kutuhumiwa.

Tusipoangalia serikali ya Magufuli ikiishiwa hela itakuwa inabambikia matajiri kesi za uhujumu uchumi na kuwambia watoe hela ili waachiwe. Nyie fanyeni mzaha na hili, subiri Magufuli anogewe na haka kamchezo
 
Kutaifishwa bado wangeendelea na kesi. Na unataifishaje kabla kesi haijaisha?
Wanakubali wenyewe hivyo wanarahisisha upelelezi na wanalipa. Kwani nchi inapata faida gani kuwaweka magerezani huku wakilishwa na kodi zetu wakati wametuibia?
 
Ikitokea kwamba mwendesha mashitaka anamfutia mtu kesi baada ya kupewa fedha na mtuhumiwa, hiyo ni rushwa. Na inakuwa rushwa si kwa kuwa mwendesha mashitaka kafaidika na ile fedha kibinafsi badala ya serikali ili kumwachia huru mtuhumiwa, inakuwa ni rushwa kwa kuwa haki (justice) imepindishwa kwa mtuhumiwa kununua uhuru kinyume na sheria. LInakuwa kosa hata kama mwendesha mashitaka atasema nilitumia zile hela kuchangia mradi wa maji kijijini kwangu.

Sasa hebu tubadili picha, badala ya mwendesha mashitaka, tuiweke serikali. Je inakuwa halali kwa serikali kuomba "hongo" kwa watuhumiwa ili waachiwe huru? Kanuni ni zile zile, tatizo hapa ni kwamba hii "hongo" inahalalishwa na serikali. Huo ndio ukweli, mpende msipende.

Hakuna tofauti na trafiki kukukama kwa makosa barabarani, ukampa hela ili akuachie yaishe. Huyo trafiki ni mpokea rushwa. Sasa hapa serikali imekuwa kama trafiki mpokea rushwa, hata kama hiyo hela ni kwa ajili ya mboga nyumbani!

Na mbaya zaidi kuna kipengele cha haki katika sheria. Hawa ni watuhumiwa. Serikali inajuaje kama wasingeshinda kesi zao? Kuwaambia watoe "hongo" ni namna fulani ya kitu kinaitwa "blackmail". Ni wazi kwamba hata kama wanajua wangeweza kushinda kesi zao wataomba msamaha yaishe na kutoa hiyo "hongo" kwa serikali.

Hii serikali ina mambo ya ajabu sana.
Du watu buana mna manejo makali kama mikuki.
 
Una maono ya mbali sana kwa comment hii
Nchi nyingine zinafanya hivyi ukitiwa hatiani, sio kutuhumiwa.

Tusipoangalia serikali ya Magufuli ikiishiwa hela itakuwa inabambikia matajiri kesi za uhujumu uchumi na kuwambia watoe hela ili waachiwe. Nyie fanyeni mzaha na hili, subiri Magufuli anogewe na haka kamchezo
 
Wanakubali wenyewe hivyo wanarahisisha upelelezi na wanalipa. Kwani nchi inapata faida gani kuwaweka magerezani huku wakilishwa na kodi zetu wakati wametuibia?
Wanakubali wenyewe kwasababu wanajua serikali ndio imeshika mpini wao wameshika makali lakini sio hiari yao ni vile option inayobaki ni kusubiria kesi iishe ambayo hujui itaisha lini,kesi zina miaka minne eti upelelezi haujakamilika,yani nikuibie leo lakini niliekuibia miaka minne haujaweza kuthibitisha bila ya shaka kwamba nilikuibia!?
 
Wanakubali wenyewe hivyo wanarahisisha upelelezi na wanalipa. Kwani nchi inapata faida gani kuwaweka magerezani huku wakilishwa na kodi zetu wakati wametuibia?
Kama tunaangalia nchi inapata faida gani kwa kuwaweka magerezani huku wakilishwa na kodi zetu basi tuangalie wafungwa wote nao tuone tunafanyaje ili wasiendelee kututia hasara maana kuna watu wameiba kuku tu wapo magerezani,kuna watu wameua sasa yanini waendelee kututia hasara wakati hata tukiwafunga uhai wa waliowauwa haurudi?
 
Nchi nyingine zinafanya hivyi ukitiwa hatiani, sio kutuhumiwa.

Tusipoangalia serikali ya Magufuli ikiishiwa hela itakuwa inabambikia matajiri kesi za uhujumu uchumi na kuwambia watoe hela ili waachiwe. Nyie fanyeni mzaha na hili, subiri Magufuli anogewe na haka kamchezo
tutakoma sana sana hasa hapo baadae, hivi kama tumetuhumiwa wawili hela alikula mmoja bila mwingone kujua alieiba akilipa huyu anaebaki atafanywa nini?

Hii ni Rushwa Period.!
 
Ikitokea kwamba mwendesha mashitaka anamfutia mtu kesi baada ya kupewa fedha na mtuhumiwa, hiyo ni rushwa. Na inakuwa rushwa si kwa kuwa mwendesha mashitaka kafaidika na ile fedha kibinafsi badala ya serikali ili kumwachia huru mtuhumiwa, inakuwa ni rushwa kwa kuwa haki (justice) imepindishwa kwa mtuhumiwa kununua uhuru kinyume na sheria. LInakuwa kosa hata kama mwendesha mashitaka atasema nilitumia zile hela kuchangia mradi wa maji kijijini kwangu.

Sasa hebu tubadili picha, badala ya mwendesha mashitaka, tuiweke serikali. Je inakuwa halali kwa serikali kuomba "hongo" kwa watuhumiwa ili waachiwe huru? Kanuni ni zile zile, tatizo hapa ni kwamba hii "hongo" inahalalishwa na serikali. Huo ndio ukweli, mpende msipende.

Hakuna tofauti na trafiki kukukama kwa makosa barabarani, ukampa hela ili akuachie yaishe. Huyo trafiki ni mpokea rushwa. Sasa hapa serikali imekuwa kama trafiki mpokea rushwa, hata kama hiyo hela ni kwa ajili ya mboga nyumbani!

Na mbaya zaidi kuna kipengele cha haki katika sheria. Hawa ni watuhumiwa. Serikali inajuaje kama wasingeshinda kesi zao? Kuwaambia watoe "hongo" ni namna fulani ya kitu kinaitwa "blackmail". Ni wazi kwamba hata kama wanajua wangeweza kushinda kesi zao wataomba msamaha yaishe na kutoa hiyo "hongo" kwa serikali.

Hii serikali ina mambo ya ajabu sana.
Ni option, usihangaike kuandika ujinga !
 
Escobar alijenga jela yake mwenyewe na iliitwa La Catedral au The Cathedral
Duniani kuna mengi ya kujifunza
 
Back
Top Bottom