Kuwa tajiri kwa mtaji wa laki 3 tu kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji

Kuwa Tajiri kwa Mtaji wa Laki 3 tu, Kupitia Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji
Kuku-kupatana.jpg

LEO TUANGALIE MCHANGANUO WA TSHS 300,000/= (LAKI TATU) KWA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI.

Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanao taga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu 300 au na zaidi kama unataka.
Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.

Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.

Usinunue kuku kabla hujaandaa banda na Chakula.
Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.

Mchanganuo Wa 69500 ni:-
Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.

Paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.
Mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500
layer's consetraite

Kilo 25 kifuko. = 21500.

Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.

Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.

Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku
Hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300.
Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.

TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.
Mchanganuo wake Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.

Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500

-Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wakutaga Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.

Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.
Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.

Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200. Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe.

Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.

Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote.
Hamna banda la sh 60,000 labda ukate miti na fimbo porini ndio utapata,juu uezeke na majani ya miti utayoyakata Ila hayo mabati ya reject hata ulikute lina kutu kiasi gani Huuziwi chini ya 2000 - 3000 sasa bado mbao,misumari,usafiri,nk

Laki 3 unayoiongelea ukipigia hesabu ya KUKU TU kidogo nakuelewa ila sio kuanzia banda hadi kuku wenyewe na chakula Juuu Hapana hapo unaingiza watu kwenye majuto mkuu.

Sijaona mahali umeweka gharama za DAWA za hao kuku,maana kwa kuku wote hao kuwapa dawa na dawa zenyewe ndio zipo kwenye vichupa vidogo na zinauzwa BEI hapana sikubaliani la hilo.

Kwa mradi huo tena wa kuwaachia kuku wazurure wenyewe ni kumtakia mtu anaeanza kufuga HASARA sio kila mtu ana endeo la kuachia kuku hivyo,wezi hawapo hivi eeh? magonjwaaa?? tena kuku wazururaji ndio kabsaaa sio wakutegemea kibiashara.

Kidogo ungeshauri watu wafungie kuku ndani na kuwajengea eneo la kuzurura ambalo mtu utaweza li control ila sio kufunglia kuku wakazurure,Hapo ni kumsababisha mwenye ki LAKI 3 chake akipoteze bureeee AJE kulaani BIASHARA ambayo ni nzuri kumbe tatzo ni mwalimu kalisha wanafunzi matango PORI.

banda ulilosema lijengwe kwa gharama uliyotaja ni banda la kufugia NJIWA AU sili au Sungura sio KUKU tena kuku wa biashara.HAPANA.
 
Ni rahisi sana kwa kusoma nenda shule yake sasa

Uvumilivu na kujituma ni mhimu sana.
 
Hii kitu sio lahisi kama wengi wanavyofikiria,ukizingatia makadirio yamewekwa juu sana.mimi nilianza hivyo mwaka jana lakini mpaka leo nina kuku kama ishirini tu maana niliamua kuwala baadhi.changamoto kubwa nilioiona ni kutunza vifaranga ili waongezeke hao kuku,hapo ndo kimbembe:confused:
Mbona vinapatikana vyote ?
Ona hii Incubator ya mayai SABA.
haifiki hata 100,000/=

HTB1GtF_ldbJ8KJjy1zjq6yqapXab.jpg
Nataka hiyo incubator, ntaipataje??
 
Kuwa Tajiri kwa Mtaji wa Laki 3 tu, Kupitia Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji
Kuku-kupatana.jpg

LEO TUANGALIE MCHANGANUO WA TSHS 300,000/= (LAKI TATU) KWA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI.

Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanao taga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu 300 au na zaidi kama unataka.
Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.

Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.

Usinunue kuku kabla hujaandaa banda na Chakula.
Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.

Mchanganuo Wa 69500 ni:-
Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.

Paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.
Mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500
layer's consetraite

Kilo 25 kifuko. = 21500.

Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.

Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.

Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku
Hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300.
Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.

TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.
Mchanganuo wake Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.

Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500

-Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wakutaga Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.

Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.
Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.

Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200. Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe.

Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.

Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote.
Nimekuelewa vzr sn mkuu
 
Ni idea sahihi na ina ukweli unaowezekana ndani yake...

Binaafsi pia ni mfugaji... Alichosahau ni suala la magonjwa na urahisi wa kufa kwa mifugo.... Izo kinga alizozisem mazee zinatibu kibahat bahat unaweza ukawapa na ukakuta woote wamekufa asubuh.....

Alafu karahisisha saaana..... Lazima upambane sio simple kama unavyosoma.


Changamoto ya kuku ni hapo tu..... Kwingine koote hakuna tatizo kabiisa. Na inawezkan...
 
Tatizo kubwa hapa watu wengi wamezoea kupinga kila kitu! naomba niwambie kitu kimoja.
Kija jambo unaloliona lilianzia kwenye wazo. Hata binadamu alianzia kwenye neno (biblia inatuambia hivyo)
Hata wewe unayesoma hapo ulianzia kwenye neno toka kwa baba yako kwenda kwa mama yako, walipokubaliana ndo wakatenda - mimba ikapatikana ... mama akalea mimba .. miezi 9 ukafunguka!
Acheni kupinga kila kitu - tenda!
 
Tatizo kubwa hapa watu wengi wamezoea kupinga kila kitu! naomba niwambie kitu kimoja.
Kija jambo unaloliona lilianzia kwenye wazo. Hata binadamu alianzia kwenye neno (biblia inatuambia hivyo)
Hata wewe unayesoma hapo ulianzia kwenye neno toka kwa baba yako kwenda kwa mama yako, walipokubaliana ndo wakatenda - mimba ikapatikana ... mama akalea mimba .. miezi 9 ukafunguka!
Acheni kupinga kila kitu - tenda!
Watu wanapinga pinga saana. sijui wao wanafanya shughuli gan ambayo haina hasara wala changamoto
 
Watu wanapinga pinga saana. sijui wao wanafanya shughuli gan ambayo haina hasara wala changamoto
Ni roho za kishetani ...
Mimi niliwahi kununua vifaranga chotara 100, wakafa sana wakabaki vifaranga nane (8) tu na kati ya hao walikuwepo majogoo 2. Sipaswi kutoa ushuhuda huo kwa wengine kwa sababu nilijua kosa langu ...
Baada ya hapo nilinunua tena vifaranga 200; wife alichukia sana akisema naharibu hela ... hawa 200 walikua 187 hadi kuanza kutaga .. majike walikuwa 145, majogoo 42; huyo huyo aliyechukia (wife) ndo alikuwa wa kwanza kunishawishi atafute wateja wa kuyanunua hayo majogoo na kunishauli nitoe jogoo mmoja nimpeleke kanisani kama shukrani ya pekee.
Namaanisha nini?
Wapinzani wa maendeleo / mafanikio yetu sio mitandaoni tu; wengine tuko nao majumbani.
Ushauri, usisite kuthubutu!
 
Ni roho za kishetani ...
Mimi niliwahi kununua vifaranga chotara 100, wakafa sana wakabaki vifaranga nane (8) tu na kati ya hao walikuwepo majogoo 2. Sipaswi kutoa ushuhuda huo kwa wengine kwa sababu nilijua kosa langu ...
Baada ya hapo nilinunua tena vifaranga 200; wife alichukia sana akisema naharibu hela ... hawa 200 walikua 187 hadi kuanza kutaga .. majike walikuwa 145, majogoo 42; huyo huyo aliyechukia (wife) ndo alikuwa wa kwanza kunishawishi atafute wateja wa kuyanunua hayo majogoo na kunishauli nitoe jogoo mmoja nimpeleke kanisani kama shukrani ya pekee.
Namaanisha nini?
Wapinzani wa maendeleo / mafanikio yetu sio mitandaoni tu; wengine tuko nao majumbani.
Ushauri, usisite kuthubutu!
Safii mkuu, vp mradi mpaka sasa umefikisha kuku wangap
 
76 Reactions
Reply
Back
Top Bottom