Kuwa Serious Na Maisha Yako Ndugu Yangu

Ambiele Kiviele

JF-Expert Member
Dec 29, 2014
15,271
29,879
Huwezi Kuwa Serious Na Maisha Afu Mwaka Mzima Unajadili Lowassa Na Magufuli Wakati Hela Huna. Utakuwa unahitaji Kusaidiwa Kifikira Mambo Yanayohusu Tundu Lissu,

Sijui Lema, Sijui Nape, Arsenal Na Liverpool Yataendelea Kuwepo Tena Yatazidi Kuongezeka.

Usiwe "Teja" Wa Mambo Ya Aina Hiyo. Hayataisha. Sasa Usipoangalia Mambo Yako Utashanga Umefika Miaka 40 Bado Unaishi Nyumba Ya Kupanga Bado Unapanda Daladala Bado Unaongelea Maisha Ya Watu Eti Unatoa Hoja.

Time Is Money. Be Careful. Point Yangu Ni Kuwa Ni Kweli Kabisa Mambo Yanayotokea Kwenye Jamii.

Ila Usichojua Ni Kwamba Bakhressa Naye Anajua Yanatokea Ila Tofauti Ni Kwamba Yeye Anaangalia Maisha Yake Wewe Ndio Unatumia Mda Wote Kuwa Mchambuzi Mara Siasa, Mara Mpira, Mara Wasanii.

Kila Mada Unajua Magufuli Kamaliza Mwaka Wewe Unajadili Atamaliza Mwaka Wa Pili Bado Unazidi Kukasirika Na Kujadili Wa Tatu Hvyo Hivyo.

Uchaguzi Ujao Unakukuta Uko Hivyo Hivyo Afu Unasema Humpi Kula. Wengine Wanampa.

Unarudi Kujadili Tena 2020 Hadi 2025 Kisha Unasema Unataka Kuwa Kama Bakhressa Kweli? Utaacha Kufa Maskini Kweli...??
 
Tusipangiane jinsi ya kuishi. Mkulu alishasema hataki kupangiwa, basi tusipangiane jinsi ya kuishi, mtu akiishi nyumba ya kupanga au ukifikisha miaka 50 bado anaishi kwao wewe inakuhusu nini?
 
Thread nzuri sana hii kwa kufanyia TAFAKURI, nikiwa navuta muda wa kula DAKU
 
Ogopa sana mtu kila mada anajua na kila story anachangia na mkimsikiliza anayatawala hata mazungumzo yenu,
Kila kitu mpaka akiskia mtu kasonya utaskia huo msonyo unanikumbusha nikiwa mkoa mflani then analiamsha dude mzee unajiuliza hyu jamaa nmemtolea wapi
 
Back
Top Bottom