Dumelambegu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,052
- 257
Wandugu,Kwa mtazamo wangu, umeme ni kila kitu kwa maisha ya kisasa. Bila umeme nchi inayumba kiuchumi na katika nyanja zote za maisha ya mwananchi. Kinachonisikitisha ni kuwa katikati ya janga hili la nchi kuwa gizani kutokana na upungufu wa umeme, mkuu wetu wa nchi yupo busy na safari za nje. Mbaya zaidi safari zenyewe ni za kustarehe tu. Nimetafakari sana hali hii na kuhitimisha kuwa nchi yetu bado haijapata kiongozi. Sijui mnasemaje wadau?