Kuwa mwanasheria ndani ya mwezi mmoja tu

Mnaokosoa wote naona mnashindwa kuelewa tofauti ya MWANASHERIA na WAKILI.

Mwanasheria ni mtu yeyote ambaye amejifunza na anaijua sheria.

Wakili ni mtu aliyepewa idhini ya kuwakilisha watu kwenye kesi Mahakamani. Ili kuwa Wakili ndo inabidi usome degree na ufaulu Law School. Lakini Mwanasheria sio lazima kupitia kote huko.

Nifafanue tu kwamba kozi hii haitakufanya uwe Wakili, ila itakufanya uwe Mwanasheria.

Jambo la Muhimu kwa mnaotaka kujifunza kufahamu ni kwamba MAHAKAMA ZIKO WAZI KWA KILA MTU. SIO KWA MAWAKILI TU. MTU YEYOTE ANAKARIBISHWA KUFUNGUA KESI YAKE MAHAKAMANI AU KUJITETEA KWENYE MASHTAKA DHIDI YAKE MAHAKAMANI. SIO LAZIMA ATETEWE NA WAKILI.

Kwa hiyo kozi hii ndo imelenga hapo. Kukuwezesha uweze kuitumia Mahakama vizuri kwenye ishu zako za Kisheria.

Natumai mpaka hapo tumeelewana.
Wewe utakuwa na tatizo kwenye ubongo wako. Mwanasheria ni mhitimu wa shahada ya sheria kutoka kwenye chuo kilichosajiliwa na serikali. Wakili ni mhitimu wa shahada ya sheria plus aliyefaulu Bar Exams au Law School.

Wacha utapeli kijana, tafuta pesa kihalali vinginevyo utajuta!
 
Pumbavu mkubwa wewe!

Watu wanakaa darasani miaka mitano mpaka saba kusoma taaluma ya sheria halafu unakuja mpuuzi mmoja wewe.... eti sheria mwezi mmoja!

Jinga wewe!

Ungekuwa karibu ningekutandika viboko!
 
Narudia tena naomba muwapuuze hawa wakosoaji sio kosa lao. Ni kosa la mfumo wetu wa elimu.

Ukijiunga na darasa langu somo la kwanza kabisa nitaeleza kwa undani kwanini Sheria ni somo rahisi kuliko yote, lakini mfumo wetu wa elimu ndo umesababisha sheria kuonekana ni somo gumu sana.

Karibuni sana.

Link ya kujiunga ni hii hapa

GUARANTEE

MAFUNZO NI YA MWEZI MMOJA. ILA NDANI YA WIKI MOJA YA KWANZA UKIONA MAFUNZO YANGU NI MIYEYUSHO NAKURUHUSU KUJIONDOA NA NITAKURUDISHIA ADA YAKO YOTE KAMILI BILA MASWALI YOYOTE.
 
Mwaka huu njaa zitawaua watu kwa kweli. Huwezi ukawa mwanasheria kwa namna ulivyoelezea labda tu kama watakuwa Vishoka mtaani kutokana na sababu zifuatazo:-

Kwanza, Wewe ni nani utoe cheti cha uanasheria?

Pili, kwa lugha nyepesi haujui nini maana ya mwanasheria na wakili.

Tatu, hujui ni nani mwenye haki ya kusimama mahakamni na kumwakilisha mteja kati ya Mwanasheria na Wakili.

Nne, Taaluma ya sheria ina wigo mpana sana hivyo huwezi kuwa mwanasheria kwa mwezi mmoja.

Tano, njaa isikuendeshe mpaka unataka kuharibu taaluma ya watu Mkuu.
 
Narudia tena naomba muwapuuze hawa wakosoaji sio kosa lao. Ni kosa la mfumo wetu wa elimu.

Ukijiunga na darasa langu somo la kwanza kabisa nitaeleza kwa undani kwanini Sheria ni somo rahisi kuliko yote, lakini mfumo wetu wa elimu ndo umesababisha sheria kuonekana ni somo gumu sana.

Karibuni sana.

Link ya kujiunga ni hii hapa

GUARANTEE

MAFUNZO NI YA MWEZI MMOJA. ILA NDANI YA WIKI MOJA YA KWANZA UKIONA MAFUNZO YANGU NI MIYEYUSHO NAKURUHUSU KUJIONDOA NA NITAKURUDISHIA ADA YAKO YOTE KAMILI BILA MASWALI YOYOTE.
Pumbavu mkubwa. Huna nidhamu wewe?????

Tafuta ujasiriamali mwingine lakini sio ujasiriamali wa kitaaluma. Tutakuadhibu kwa njia yoyote inayowezekana.

Wacha ujuha!
 
Narudia tena naomba muwapuuze hawa wakosoaji sio kosa lao. Ni kosa la mfumo wetu wa elimu.

Ukijiunga na darasa langu somo la kwanza kabisa nitaeleza kwa undani kwanini Sheria ni somo rahisi kuliko yote, lakini mfumo wetu wa elimu ndo umesababisha sheria kuonekana ni somo gumu sana.

Karibuni sana.

Link ya kujiunga ni hii hapa

GUARANTEE

MAFUNZO NI YA MWEZI MMOJA. ILA NDANI YA WIKI MOJA YA KWANZA UKIONA MAFUNZO YANGU NI MIYEYUSHO NAKURUHUSU KUJIONDOA NA NITAKURUDISHIA ADA YAKO YOTE KAMILI BILA MASWALI YOYOTE.
Mi naomba ada ipungue kwanza tumalize kulipa baada ya kupata cheti
 
Mleta hoja amesema anafundisha watu wapate msingi (basic) ya sheria iwasaidie kuelewa mambo ya kisheria na kusimamia mambo yao wenyewe yahusuyo sheria, kitu ambacho kinawezekana tu. It is just basics..

Hajasema anamuandaa mtu kuwa wakili, au hajasema vyeti atavyotoa vitakuwa vya kielimu na vitatumika wapi..sasa hii kumshambulia sijui hata sababu ni nini..

Mwanafalsafa usife moyo kwa lengo lako hilo, wataopenda kujiunga acha wajiunge, sioni utapeli hapo kulingana na tangazo lako, kujiunga ni hiyari na kufanya due diligence ni jukumu la kila mtu anayetaka kufaidika na kitu.
 
Link iko wapi mkuu halafu huwezi kushusha ada mpaka kwenye elfu 10 hii si kama kusaidiana tu halafu ukizingatia wengine sisi sio watu wa mikesikesi
 
Kigezo cha elimu kipoje kwa anaehitaji kujifunza sheria?
Habari zenu Wadau,

Kama unatembelea jukwaa hili la sheria, ina maanisha tayari unafahamu umuhimu wa sheria katika maisha yako ya kila siku.

Lakini ukitaka kujifunza sheria program zilizopo Tanzania kwa sasa ni ndefu na za gharama. Inabidi ujipange.

Hivyo basi, baada ya kuwa nimepitia Program za Mafunzo ya Sheria Tanzania, na kufanya practical za kuendesha kesi Mahakamani nimewatengenezea Program ya Ukweli YA MWEZI MMOJA TU ambayo itakufundisha mambo yote ya msingi ya kukuwezesha kutatua matatizo yako yote ya kisheria wewe mwenyewe.

Ukitaka Wakili basi iwe umeamua tu. Mfano ubize umekubana,

Program nii inatwa ONE-MONTH LAWYER.

MAFUNZO YATAANZA JUMATATU YA 23/9/2019


Mada (Silabasi) ni kama ifuatavyo:

1. SHERIA NI NINI?
=> Maana, historia, na tofauti kati ya jinai na madai.

2. VYANZO VYA SHERIA
=> Katiba, Sheria za Bunge, Sheria za Mapokeo, Sheria za Kimataifa, Mila na Utamaduni, Hukumu za Mahakama

3. SHERIA MUHIMU ZA JINAI UNAZOTAKIWA KUJUA
=> Kanuni ya adhabu, Mwenendo wa jinai, Sheria ya Ushahidi, na jinsi ya kuvibaini vifungu vya jinai kwenye sheria zote

4. SHERIA MUHIMU ZA MADAI UNAZOTAKIWA KUJUA
=> Madhara, Mkataba, Mwenendo wa madai, Ndoa, Ardhi, n.k.

5. MAHAKAMA
=> Sheria iko Mahakamani. Hapa utajifunza aina zote za Mahakama, ziko wapi na zinafanyeje kazi

6. JINSI YA KUSHINDA KESI MAHAKAMANI
=> Kutathmini kesi, kuandaa nyaraka, kuandaa ushahidi, milango ya kutokea (loopholes), na jinsi ya kuongea.


ADA NI

TSHS. 50,000/- Kwa darasa la mtandaoni (kupitia app ya Telegram)

TSHS. 100,000/- Kwa darasa la uso kwa uso

SI HAYO TU...

Ukishamaliza kozi hii utapatiwa Cheti cha Kuhitimu, na utaunganishwa na Group Exclusive la Mtandaoni la wahitimu wote na wakufunzi wao ambapo lengo kuu ni kuhakikisha hakuna kesi yoyote ambayo itakusumbua milele. Ukiwa na kesi utaileta hapo kwenye group na utapewa nyenzo zote za kuimaliza hiyo kesi kuanzia Vyanzo vya Kisheria vya Kutumia, Nyaraka za Kupeleka Mahakamani, na Hoja za Ushindi.

Kama umevutiwa ingia Waiting Room kupitia link hii ya Telegram

Waiting Room unaweza ukauliza maswali, na utapewa maelekezo zaidi.

lawyer-03-300x225.jpg
 
Mkuu@Mwanafalsafa binafisi nimekuelewa lengo lako hasa ni kuwafanya watu wajue mambo muhimu katika sheria, kusema ukweli mimi katika taaluma ya sheria huwa naona giza giza mara mahakama imemkuta na kesi ya kujibu mwisho wa siku mhusika anaachiwa huru , mara mahakama imetupilia mbali mapingamizi ..OK kwa upande nitajiunga na hilo darasa at least nizinue a,b,c za sheria .
 
Mnaokosoa wote naona mnashindwa kuelewa tofauti ya MWANASHERIA na WAKILI.

Mwanasheria ni mtu yeyote ambaye amejifunza na anaijua sheria.

Wakili ni mtu aliyepewa idhini ya kuwakilisha watu kwenye kesi Mahakamani. Ili kuwa Wakili ndo inabidi usome degree na ufaulu Law School. Lakini Mwanasheria sio lazima kupitia kote huko.

Nifafanue tu kwamba kozi hii haitakufanya uwe Wakili, ila itakufanya uwe Mwanasheria.

Jambo la Muhimu kwa mnaotaka kujifunza kufahamu ni kwamba MAHAKAMA ZIKO WAZI KWA KILA MTU. SIO KWA MAWAKILI TU. MTU YEYOTE ANAKARIBISHWA KUFUNGUA KESI YAKE MAHAKAMANI AU KUJITETEA KWENYE MASHTAKA DHIDI YAKE MAHAKAMANI. SIO LAZIMA ATETEWE NA WAKILI.

Kwa hiyo kozi hii ndo imelenga hapo. Kukuwezesha uweze kuitumia Mahakama vizuri kwenye ishu zako za Kisheria.

Natumai mpaka hapo tumeelewana.
Kanjanja at work
 
Mtoa mada mbona unajifedhehesha?

Huoni kwamba unaichafua taaluma?

Hatakama hali ni ngumu tusifikie hatua hii!

Nakuchukia Mtoa mada kutokana na hiki ulichokileta hapa!
mna shidwa kuelewa labda sababu ya kukarili ukweli ni kwamba kwa mtu makini akijifunza basic knowledge ya law + practice ya kutosha ktk changamoto ya different case anaweza kuwa mwanasheria mzuri tuu pia tambua kuwa law is an art of arguing to the facts. kitu atakosa ni parmit ya kuwakilisha watu wengine lakini kwa matter zake binafisi anaweza kuwa fit kuliko hata wakili kuna nchi zingine unaweza wakilishwa na mtu yeyete utakaye mchagua na kumuamini hata kama sio public advocate na unakuta anamshinda hata public advocete tena tecnicality
 
Wewe utakuwa na tatizo kwenye ubongo wako. Mwanasheria ni mhitimu wa shahada ya sheria kutoka kwenye chuo kilichosajiliwa na serikali. Wakili ni mhitimu wa shahada ya sheria plus aliyefaulu Bar Exams au Law School.

Wacha utapeli kijana, tafuta pesa kihalali vinginevyo utajuta!
sifa ya kuwa hakimu wa mahakama ya wilaya ni ipi tuanzie hapo mimi nawafahamu mahakimu wengi sana wa mahakama za wilaya wenye just diploma tuu ya law
 
Pumbavu mkubwa wewe!

Watu wanakaa darasani miaka mitano mpaka saba kusoma taaluma ya sheria halafu unakuja mpuuzi mmoja wewe.... eti sheria mwezi mmoja!

Jinga wewe!

Ungekuwa karibu ningekutandika viboko!
lete hoja za kisomi sasa matusi ya nn kukaa darasani mda mrefu sio kigezo cha moja kwa moja cha kujua au kuto kujua jambo sheria ni kitu kipana sana hata ukikaa miaka 20 huwezi imaliza vitu vingine utaishia kuvijua kwa ujuu tuu utavijua vizuri zaidi na kubobea kadri utakavyokuwa unapractise huo ndo ukweli
 
lete hoja za kisomi sasa matusi ya nn kukaa darasani mda mrefu sio kigezo cha moja kwa moja cha kujua au kuto kujua jambo sheria ni kitu kipana sana hata ukikaa miaka 20 huwezi imaliza vitu vingine utaishia kuvijua kwa ujuu tuu utavijua vizuri zaidi na kubobea kadri utakavyokuwa unapractise huo ndo ukweli
Wewe ni mwalimu pia katika hicho chuo cha kuwa mwanasheria ndani ya mwezi mmoja?
 
Mwaka huu njaa zitawaua watu kwa kweli. Huwezi ukawa mwanasheria kwa namna ulivyoelezea labda tu kama watakuwa Vishoka mtaani kutokana na sababu zifuatazo:-

Kwanza, Wewe ni nani utoe cheti cha uanasheria?

Pili, kwa lugha nyepesi haujui nini maana ya mwanasheria na wakili.

Tatu, hujui ni nani mwenye haki ya kusimama mahakamni na kumwakilisha mteja kati ya Mwanasheria na Wakili.

Nne, Taaluma ya sheria ina wigo mpana sana hivyo huwezi kuwa mwanasheria kwa mwezi mmoja.

Tano, njaa isikuendeshe mpaka unataka kuharibu taaluma ya watu Mkuu.
jamani tusimnukuu vibaya ajasema kuwa ukimaliza unakuwa wakili sio kweli tumuelewe yeye amesema utaweza kujitetea mwenyewe na nikatika baadhi ya kesi tuu sio kwa kila matters
 
Pumbavu mkubwa. Huna nidhamu wewe?????

Tafuta ujasiriamali mwingine lakini sio ujasiriamali wa kitaaluma. Tutakuadhibu kwa njia yoyote inayowezekana.

Wacha ujuha!
utamuadhibu kwa kosa gani hebu eleza? jamani dunia inabadilika inabidi tuwe na mitazamo ya kufanya vitu mbadala kuboresha taaluma zetu ziendane na mabadiliko ya dunia tayari kuna nch zimesha anza kuruhusu upande wote katika kesi kuwakilishwa na either advocate, institition au asasi yoyote ya kijamii mfano trade union au mtuyeyote ambaye upande utamlidhia auwakilishe ikifikia hatua hiyo hautamuwakilisha mteja tena kwa sababu ww ni wakili umesoma sana na kufaulu vizuri darasani bali ni kwasababu tu unauwezo wa kushinda changamoto za kesi husika bila kujali ukubwa wa taaluma yako sasa itafikia hatua baadhi ya watu wenye vipaji vyao vya kuchanganua , kujenga na kupangua hoja watakuwa wanaaminika pia kutokana na matokeo ya kesi wanazo fanya. mimi natoa rai kwa wanataluma wezangu kwamba sheria ni kitu kipana sana unaweza ukajua kwa kujifunza kidogo na kupractise kwa kubobea kwenye aina flani tuu ya kesi usije ukamdharau mtu wa namna hiyo ukikutana naye anaweza kukutoa nishai pamoja na qulification zote law is an art of arguing.
 
Wewe ni mwalimu pia katika hicho chuo cha kuwa mwanasheria ndani ya mwezi mmoja?
mimi nimesoma sheria na ninafanya kazi zangu binafsi napenda watanzania wengi wajue sheria za msingi sasa unakuta hata mtu hajui utaratibu wa kumuwekea dhamana ndugu yake pesa hana na kesi yenyewe ni ya praimary court wakili haupaswi ku involve kwenye vijikesi kama ivo mtu akiwa na basic knowledge anatakiwa ajisaidie mwenyewe labda kuwe na complication zingine
 
Back
Top Bottom