Kuwa Mtanzania katika Tanzania (ndani au nje ya nchi) kuna manufaa gani kwa nchi ya Tanzania?

S.M.P2503

JF-Expert Member
Nov 25, 2008
1,643
2,607
Kama ni michango ya harusi- sote tunalipa
Kama ni michango ya ujenzi wa shule- tunalipa
Kaka sina Ada- tunalipa
Dada sina karo ya shule-tunalipa
Mama mwaka huu mvua haikunyesha- tunalipa
Mwanangu nikakufa na njaa- tunalipa
Mwanangu nyumba inaniangukia- tunalipa
Kaka sina viatu vya shule wala uniform – tunalipa
Kaka board ya mikopo inataka lazima uwe na kiasi Fulani ndio ukopeshwe- tunalipa
Kaka tuma hela za kiwanja- tunalipa
Dada bado kidogo tu tufukuzwe kwenye pango- tunalipa
Baba niongezee mchano wa karo- tunalipa
Mama nina deni la Saccos – tunalipa
Na mengineyo mengi,

sasa kwa nini mnatunyanyasa na mnaendelea kututumia ? Mirija lazima ifungwe mpaka akili zenu ziamke zianze kung'amua mambo kwamba sote tuko sawa, watoto wa tumbo moja, baba mmoja na nchi yetu sote moja , ndugu wa damu kuzaliwa Tanzania na ni katika kutafuta tu maisha ndio maana wengine tuko huku ngambo ya mbali, wengine Dar es salaam toka mikoani mianka nenda rudi bila mtu kurudi kwao hata kusalimia tu; sote twajua huku ulaya na marekani kwamba fainali uzeeni na hili tunalijua sana tu . Acheni kutubagua wakatu sote ni wamoja , wachina , wapakistani na wengineo munawapa uraia na sisi munasuasua , maana yake nini… hamuna mapenzi ya dhati kwetu ili hali michango yetu munaiomba kwa udi na uvumba na mchana pia usiku ni kupanga namna ya kutuchoma fedha tu huku.

Hakuna tofauti yeyote kati yetu na ndugu zetu wa Arusha wenye asili ya musoma na kwingineko wanochukua masaa 12 kusafiri kwa basi mbugani serengiti au hata miaka kenda bila kwenda salimia makwao toka Dar Es Salaam ili hali sisi ni masaa 8 tu… haijalishi kama tuko huku au la na tunakuja kila likizo na wake na watoto zetu.

Haki yetu ya Urai isiwe mpira wa miguu kupigwa huku na kule , haki tunaitaka na msitulazimishe kuwakana wazazi wetu na uraia wetu maana kukaana uraia maana yake ni kuwakana wazazi wako waliokupa uraia huo na hakuna kitu kama hicho huku ulaya na marekani…na ndio maana hata serikali hizi za huku hawakuambii uukane uraia wako… wanakutumia tu na wewe unawatumia tu… mtumikie kafiri upate mradi wako.

Vinginevyo kama hamtaki kututambua acheni kutufanya kitega uchumi na kuja na madili mengi tu ya ufisadi kifamilia ili muweze kutubomu fedha, mipango yenu ya kutufanya vitega uchumi tunaijua na sio kwamba kuishi huku hatujui kinachoendelea huko na habari za huko tunazisoma ili hali asilimia sabini bado wako usingizini tu… kama hamtutaki achezi kuja na vijisababu vya chehechea ili hali mna madeni ya kulipa kwenye board ya mikopo.. kwa nini basi mlienda kukopa wakati shule hamkuilewa?

Eti usalama, eti Uzalendo , upuumzi mtu, hivi mkiruhusini huo uraia pacha maana yake ni ndio mtaanza tena madili ya kuwagiwia akina awilo longomba kama njugu huo uraia wa Tanzania? Mtawapa tu bila masharti? Mnatupa tu kichefu chefu kwa jinsi mnavyo tufanyia sisi ndugezeni wa huku, jifunzeni kisa cha mwana mpotevu, kaka yake na baba yake
 
Lazima yazidi mpaka akili ziwaingie ndo maana ya knowledge Transfer

one good thread would do rather than diluting the concept with emotional and passionate posts without any follow-up committment

hoja yako sio mbaya ila nyepesi sana... iweke vizuri au changia kwenye thread zilizopo tayari with key substance kurespond kwa hoja hasi za uraia pacha hasa security, usaliti kwa waliobaki nyumbani etc

watanzania wengi wanadanganywa na wanasiasa na hivyo hawaelewi hoja nzima ya dual citizenship

wanakataa uraia pacha lakini wamejenga dar na wanakwenda kugombea ubunge nachingwea... it is a similar scenario and kama kawa, unafiki unatuumbua tu

you'd do better kwa kusaidia exisiting threads, na kuchangia pesa ili kamati zinazopigania uraia pacha zipate kuwezeshwa
 
haya mathread ya utanzania ndani na nje sasa yamezidi

kha

Hahahaa. Yaani siku mbili tatu hizi zile threads za CCM vs Chadema zimekosa wachangiaji.

Jamani punguzeni wale wa buku saba wanapata loss ya kufa mtu.

Hata hivyo, ni JK mwenyewe aliwaasa diaspora kuwashawishi wajumbe wa Bunge la Katiba ili wakubali hoja zao za uraia pacha kuwa ndani ya katiba kwa kuwa hili siyo jambo haramu.

JK akawashauri Watanzania hao kutumia muda wao, kujenga hoja zao hata kwenye mitandao ya kijamii, badala ya kubishania mambo ya kisiasa zaidi (CCM vs Chadema).

Labda ndicho wanachokifanya sasa.
 
Kama ni michango ya harusi- sote tunalipa
Kama ni michango ya ujenzi wa shule- tunalipa
Kaka sina Ada- tunalipa
Dada sina karo ya shule-tunalipa
Mama mwaka huu mvua haikunyesha- tunalipa
Mwanangu nikakufa na njaa- tunalipa
Mwanangu nyumba inaniangukia- tunalipa
Kaka sina viatu vya shule wala uniform – tunalipa
Kaka board ya mikopo inataka lazima uwe na kiasi Fulani ndio ukopeshwe- tunalipa
Kaka tuma hela za kiwanja- tunalipa
Dada bado kidogo tu tufukuzwe kwenye pango- tunalipa
Baba niongezee mchano wa karo- tunalipa
Mama nina deni la Saccos – tunalipa
Na mengineyo mengi,
sasa kwa nini mnatunyanyasa na mnaendelea kututumia ? Mirija lazima ifungwe mpaka akili zenu ziamke zianze kung’amua mambo kwamba sote tuko sawa, watoto wa tumbo moja, baba mmoja na nchi yetu sote moja , ndugu wa damu kuzaliwa Tanzania na ni katika kutafuta tu maisha ndio maana wengine tuko huku ngambo ya mbali, wengine Dar es salaam toka mikoani mianka nenda rudi bila mtu kurudi kwao hata kusalimia tu; sote twajua huku ulaya na marekani kwamba fainali uzeeni na hili tunalijua sana tu . Acheni kutubagua wakatu sote ni wamoja , wachina , wapakistani na wengineo munawapa uraia na sisi munasuasua , maana yake nini… hamuna mapenzi ya dhati kwetu ili hali michango yetu munaiomba kwa udi na uvumba na mchana pia usiku ni kupanga namna ya kutuchoma fedha tu huku…
Hakuna tofauti yeyote kati yetu na ndugu zetu wa Arusha wenye asili ya musoma na kwingineko wanochukua masaa 12 kusafiri kwa basi mbugani serengiti au hata miaka kenda bila kwenda salimia makwao toka Dar Es Salaam ili hali sisi ni masaa 8 tu… haijalishi kama tuko huku au la na tunakuja kila likizo na wake na watoto zetu.
Haki yetu ya Urai isiwe mpira wa miguu kupigwa huku na kule , haki tunaitaka na msitulazimishe kuwakana wazazi wetu na uraia wetu maana kukaana uraia maana yake ni kuwakana wazazi wako waliokupa uraia huo na hakuna kitu kama hicho huku ulaya na marekani…na ndio maana hata serikali hizi za huku hawakuambii uukane uraia wako… wanakutumia tu na wewe unawatumia tu… mtumikie kafiri upate mradi wako… Vinginevyo kama hamtaki kututambua acheni kutufanya kitega uchumi na kuja na madili mengi tu ya ufisadi kifamilia ili muweze kutubomu fedha, mipango yenu ya kutufanya vitega uchumi tunaijua na sio kwamba kuishi huku hatujui kinachoendelea huko na habari za huko tunazisoma ili hali asilimia sabini bado wako usingizini tu… kama hamtutaki achezi kuja na vijisababu vya chehechea ili hali mna madeni ya kulipa kwenye board ya mikopo.. kwa nini basi mlienda kukopa wakati shule hamkuilewa?
Eti usalama, eti Uzalendo , upuumzi mtu, hivi mkiruhusini huo uraia pacha maana yake ni ndio mtaanza tena madili ya kuwagiwia akina awilo longomba kama njugu huo uraia wa Tanzania? Mtawapa tu bila masharti? Mnatupa tu kichefu chefu kwa jinsi mnavyo tufanyia sisi ndugezeni wa huku, jifunzeni kisa cha mwana mpotevu, kaka yake na baba yake…



Nimeipenda sana hii habari jinsi ulivyoiandika.mimi mni mtanzania naishi tz.nimekuea nafuatilia sana sakakata hili la uraia pacha sioni shida yoyote, ili wanasiasa watz na hsa ccm ni watu wabaya sana,kazi yao kubwa ni kuwadanganya watu.ila mwisho wao utafika tu.mlioko nje mna msada mkubwa sana ada .ujenzi nk.siyovya kuambiwa nimeona mengi kwaa macho yangu.
 
Hao viongozi wa Tanzania wa ccm na vyama vya upinzani wanapokuja nchi za ulaya na USA, Asia na Australia wanakutana na watanzania wanaoishi nje ya nchi sasa ni kina nani hao watanzania? Kama sio unafiki na usengerema tu. Sitauzulia tena mkutano wa ---- yeyote tena
 
Hahahaa. Yaani siku mbili tatu hizi zile threads za CCM vs Chadema zimekosa wachangiaji.

Jamani punguzeni wale wa buku saba wanapata loss ya kufa mtu.

Hata hivyo, ni JK mwenyewe aliwaasa diaspora kuwashawishi wajumbe wa Bunge la Katiba ili wakubali hoja zao za uraia pacha kuwa ndani ya katiba kwa kuwa hili siyo jambo haramu.

JK akawashauri Watanzania hao kutumia muda wao, kujenga hoja zao hata kwenye mitandao ya kijamii, badala ya kubishania mambo ya kisiasa zaidi (CCM vs Chadema).

Labda ndicho wanachokifanya sasa.

Naam... ila hata kwa hii dual citizenship agenda, tusipoiangalia, tutaiweka vilevile wanasiasa wanavyotaka, kusifia kizuri vs kibaya, badala ya kuchambua hoja ya uraia pacha kwa kina na ku counter-punch misleading people humu ndani
 
one good thread would do rather than diluting the concept with emotional and passionate posts without any follow-up committment

hoja yako sio mbaya ila nyepesi sana... iweke vizuri au changia kwenye thread zilizopo tayari with key substance kurespond kwa hoja hasi za uraia pacha hasa security, usaliti kwa waliobaki nyumbani etc

watanzania wengi wanadanganywa na wanasiasa na hivyo hawaelewi hoja nzima ya dual citizenship

wanakataa uraia pacha lakini wamejenga dar na wanakwenda kugombea ubunge nachingwea... it is a similar scenario and kama kawa, unafiki unatuumbua tu

you'd do better kwa kusaidia exisiting threads, na kuchangia pesa ili kamati zinazopigania uraia pacha zipate kuwezeshwa
Mkuu hili swali nimeliuliza mahusu baada ya kusoma nyuzi nyingi humu za wachangiaji kwa wiki nzima sasa na wachangaji wengi wtoka huko nyumbani wanauliza u dual citizenship una manufaa gani kwao.. kibai ni kile kile , je wao kuwa wa Tanzania huko walipo Tanzania wana manufaa gani ili hali wengine ni wakepwaji wakubwa wa kodi.. leo hii kwa sisi huku ngambo ukiambia habari za michangi huchomoki.. unafuatiliwa kweli kweli mpaka inafikia wakati unafikiria kubadili number yako ya simu... na mara nyingi watu hao haow wakikubeep wanasema nilikua nakusalimia tu kumbe ndio njia ya kuomba msaada... na hao maafisa wa uhamiaji wanaokaa huu upacha wa Utanzania ni wa ajabu sana , wanaposari kuja huku utasikia njoo unipokee airport, sijui habari za winter , nisaelimishe kuhusu hili na lile, nitafutie gari, na mambo mengine kibao.. kama hivi ndivyo kwa nini wanapenda vya kunyonga na vya kuchinja hawataki? kwa nini wanapenda kula vibudu wakati ni wacha mungu haswa? ni lazima watambue umuhimu wetu na kwamba sote tu kaka na dada...
Hoja kwamba hii swali ni jepesi ni maoni yako kama yalivyo maoni yangu na kama ningeyaweka kwenye nyuzi nyingine ningeambiwa pia nifunguye yangu..... kuchangia pesa si tatizo , tatizo ni kwa nini tutumie fedha nyingi kuwashawishi nfugu zetu kwamba na sisi tupo ili wakati wa kuomba michango tunatambulika...? Wakati wa misiba tunatambulika.. KJ AKIJA ANATUTAMBUA.. ni suala la yeye kuongea na watanzania na kuwaambia umuhimu wa jambo hili maana kwa sisi tulioko huku nu fimbo ya mbali .. nyoka hauwawi...
 
Hao viongozi wa Tanzania wa ccm na vyama vya upinzani wanapokuja nchi za ulaya na USA, Asia na Australia wanakutana na watanzania wanaoishi nje ya nchi sasa ni kina nani hao watanzania? Kama sio unafiki na usengerema tu. Sitauzulia tena mkutano wa ---- yeyote tena

Halafu tunaambiwa eti piganieni suala hili, achaeni kujali mambo yasiyo na maana.. yaani tunapangiwa hata na cha kuongea wakati sote tu nyumba moja, adui yetu sote ni CCM .. yenye serikali na watu wasio na weredi wa kuelezea jambo wawapo madarakani na wananchi wakawaelewa kwa ufasaha ... kila waongeapo nu mtafarukuna mkanganyiko tu kwa wananchi na kuwazidishia maumivu ya maisha yao kila siku... matokeo ya shule za kata ni hatari sana .. kila wakati ni ku-downgrade maksi ili mradi mambo yaende visivyo... na ndio maana hata uwezo wa watu katika jamii katika kuelewa na kupambanua jambo ni mdogo sana.. kama wao wanashindwa kuwaelimisha .. sisi tutawezaje? Kila chama na sasa kiweke msimamo wake katika hoja hiina tujue mbivu na mbichi na ni akina nani wa sizitaki mbivu hizi...
 
kwa mtz yoyote,haijalishi kaishi ughaibuni miaka mingapi,kulalamika ni jadi yetu.

Inategemea una maanisha nini kusema nin jadi yetu... kila binadamu hata wale wa Brazil wa polini walilalamika kwamba wanachomewa misitu yao.. kama kulalamika kuna maana zaidi ya kufikisha kilio chako .. basi ni njia sahihi tofauti na ile ya kuandamana barabarani na kukumbana na virungu.. yaani kuandika na kutoa ya maoni nisifanye kwa kuogapa ntaambiwa nalalamika, barabarani nisende kwa kuogapa virungu na maji ya washawasha halafu nikae kimya tu.. ndio mambi gani hayo kama sio kuninyanyasa kwa namna moja au nyingine? Wanatunyanya sana sisi wa diaspora kutucheleweshea kitu tunachotaka.. wakati wa michango hawakumbuki kuwa ni directely related na uraia pacha... sasa waamke na watuoe yunachohitaji kabla ya kuendelea na michango katika mambo mbalimbali
 
Naam... ila hata kwa hii dual citizenship agenda, tusipoiangalia, tutaiweka vilevile wanasiasa wanavyotaka, kusifia kizuri vs kibaya, badala ya kuchambua hoja ya uraia pacha kwa kina na ku counter-punch misleading people humu ndani

Ndiyo maana inadaiwa kuwa katika semina hiyo, watoa mada walikuwa ni Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Dk. Philip Mpango na mtendaji mwandamizi kutoka Idara ya Uhamiaji.

Hata hivyo, katika kile kilichowashangaza wajumbe wengi, serikali haikuwaleta wataalamu wanaohusika na uraia pacha wanaofanya kazi katika Idara ya Uhamiaji.
 
Ndiyo maana inadaiwa kuwa katika semina hiyo, watoa mada walikuwa ni Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Dk. Philip Mpango na mtendaji mwandamizi kutoka Idara ya Uhamiaji.

Hata hivyo, katika kile kilichowashangaza wajumbe wengi, serikali haikuwaleta wataalamu wanaohusika na uraia pacha wanaofanya kazi katika Idara ya Uhamiaji.

Watanzania tuna sifa kubwa tatu: unafiki, usanii, mbayuwayu

Zote hizo chanzo chake ni akili ndogo

Hata hilo bunge la katiba halikujua linaongea na wrong person??

Eiiishhhh
 
Watanzania tuna sifa kubwa tatu: unafiki, usanii, mbayuwayu

Zote hizo chanzo chake ni akili ndogo

Hata hilo bunge la katiba halikujua linaongea na wrong person??

Eiiishhhh

Swadakta swadakta! Japo siwakubali rais Mkapa na Kikwete lakini kuna mambo mawili waliyasema yenye ukweli mtupu juu ya watanzania.
1: Mkapa alisema watu ni wavivu wa kufikiri na
2: Kikwete akasema ni wafuata mkumbo.
Watu hatuhoji mara mbili mbili, tunapenda kuamini vitu rahisi rahisi na vya kijinga! Nadhani kikwazo kikubwa ni elimu. ie 1. wengi hatuna elimu ya kutosha na 2. wale wenye elimu tumeipata kimagumashi na kwa kukariri, hivyo hatukuelimika
Back to the topic: Hawa watu wa immigration ambao ukiwa unasafiri unawakuta pale airport wamejaa ugiligili wa kufa mtu kamwe hawataweza kukubaliana na hoja
 
Probably, walijua ndiyo wengi wao wakashangaa na kuishia hapo.

huko kushangaa na kuishia hapo badala ya kuhoji ndio unafiki, ujinga, umabyuwayu

They should question the quality of the facilitators

Hii nchi inaweza kukufanya ukatoa povu hadi kufa
 
Swadakta swadakta! Japo siwakubali rais Mkapa na Kikwete lakini kuna mambo mawili waliyasema yenye ukweli mtupu juu ya watanzania.
1: Mkapa alisema watu ni wavivu wa kufikiri na
2: Kikwete akasema ni wafuata mkumbo.
Watu hatuhoji mara mbili mbili, tunapenda kuamini vitu rahisi rahisi na vya kijinga! Nadhani kikwazo kikubwa ni elimu. ie 1. wengi hatuna elimu ya kutosha na 2. wale wenye elimu tumeipata kimagumashi na kwa kukariri, hivyo hatukuelimika
Back to the topic: Hawa watu wa immigration ambao ukiwa unasafiri unawakuta pale airport wamejaa ugiligili wa kufa mtu kamwe hawataweza kukubaliana na hoja

Mkuu, inapofikia hadi watu wanakua na courage ya kutupublish kama top imbeciles duniani... ujue iko shiddaa
 
Back
Top Bottom