Kuwa Mpinzani au CCM haimaanishi uwachukie na kuwatukana Upande wa Pili

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,744
CCM ina watu wengi wa hovyo ambao wanaishi kwa kujipendekeza na kuangalia maslah yao. Tuna mfano wa Nape Nnauye huyu tunafahamu kwa kiasi kikubwa alikosa malezi mazuri baada ya kulelewa na baba ambaye si wa damu yake.

Kipindi kile anapambania tumbo lake wapinzani hawa hawa walianza mpamba na kumwona ni shujaa. Nliwahi wauliza Nape ninayemfahamu mimi kilaza huyu toka lini alikuwa shujaa? Leo nape amerudi kwenye default anaendelea kutoa choo kupitia mdomo.

Katika Upinzani yupo Mwanasiasa Mbunge Joseph Haule. Huyu jamaa nmekuwa nikimwangalia sana aina yake ya siasa.humwoni akifanya siasa za kitoto kama za akina Joseph Mbilinyi. Ingawa wote ni wenyeji wa Ruvuma.

J.Mbilinyi anafanya siasa za kitoto sawa na za Nape. Watu hawatataka kuliangalia hilo. Ni aina ya siasa za Musukuma au Lusinde. Siasa taka.zisizo na faida kwa wananchi.

Ondoeni uchafu wa namna hiyo katika vyama vyenu.jengeni watu kufanya siasa za kistaarabu na zenye uelewa. Mibangi haitakiwi kwenye siasa.

Joseph Haule si mwongeaji Mzuri ndo maana nadhani anaweka speed governer mdomo wake. Joseph Mbilinyi ni mwongeaji asiyejua kupanga hoja na pia anaropoka sana.

Lusinde na Musukuma na mwenzao mmoja Goodluck kama sikosei hawa wanakuwa kama pipe za kutolea maji taka hivyo hulishwa uchafu wakaumwage sehemu yenye makazi.

Nape Nnauye huyu ukimwangalia anaukosefu mkubwa wa busara na hekima.lakini pia elimu yake ni ya kumjenga kuwa mpumbavu zaidi.
 
Mawazo mazuri mkuu ila Nature ya Sugu ni harakati ,mtu wa harakati hakubali kupelekwa pelekwa!! Nape anamtukana hadi Membe???
 
Kama kweli unasema sugu Ni mropokaji Basi wewe Ni chizi kweli,nataka ulete hapa clip moja inayoonesha uropokaji,sugu Ni mmoja ya watu wanaoshusha nondo za hatari mle bungeni.

Halafu Karne ya 21 haihitaji siasa za kistaarabu Bali inahitaji siasa Safi.Siasa ambazo sio za kutekana,kupigana risasi,na kukatana mapanga.Lakini eti unataka ustaarabu wa kusema"tukwachie Mungu".Hakuna kitu Kama hicho Kaka,saiz ili uweze kuhit kwenye siasa lazima uteme mawe,nondo,cement n.k na sio rangi na chokaa.

Marais wanaotema rangi na chokaa Ndio Marais dhaifu Kama Obama.Magufuli mwenyewe Ndio anaongoza siasa za mawe na nyundo Ndio maana CCM wanamtaka ili chama kisurvive.
 
Back
Top Bottom