Kuwa makini sana na watu wanaotoa tafasiri za ndoto (yajue haya kabla haujapewa tafasiri ya ndoto)

KijanaHuru

JF-Expert Member
Jan 7, 2017
1,822
2,290
Habari ya mchana

Poleni na mapambano dhidi ya cov19, tuendelee kujihami nakutumia wakati tulionao kujiwekea kinga zaidi.

Sasa acha niende katika hoja moja kwa moja,

Tumekuwa ni watu ambao tunaishi kwa kuota ndoto, mbalimbali zakutisha kufurahisha kuhuzunisha napia za kuchekesha.

Huenda ndoto nyingi huwa nikweli katika maisha ya kawaida pia yaweza kuwa kweli katika maisha ya kiroho, yaweza kuwa ni jambo lililopita ama pia ni jambo lijalo.

Leo hii nimeona niandike haya nikutokana na kuwepo wimbi kubwa sana la watu ambao kila leo huweza kutoa tafasiri za ndoto kwa namna zao mbalimbali kwa kadri wanavyojua na kuelewa, lakini katika asilimia 100 za maisha ya ndoto za mwanadamu mara nyingi ni asilimia ndogo sana huwa tunapata ukweli wa kile ambacho tumeweza kukiota.

Jambo la msingi na kubwa nivyema kujua yakuwa Ndoto ni lugha, ya mawasiliano katika ulimwengu wa kiroho, maana huwezi ota ndoto ukiwa upo macho zaidi zaidi yawe ni maono(nitaongelea mbele juu ya maono)

Sasa suala linakuja hivi je Mimi ni Mngoni huyu mkinga kaweze kuelewa maana ya lugha yangu?
Je una uhakika anayekupa hiyo maana anaelewa fika lugha yako ilivyo?

Polepole tu tutaelewana ndugu zangu, ngoja ninawe kujikinga na corona.

Haya naendelea.

Kwanini ujihadhari na wanaotoa tafasiri za ndoto? nikwasababu wengi wao wanajua kusoma hali ya mwongeaji wala sio kujua maana ya kile kimeongelewa

Kwanini nasema hivyo?

Mfano; Mtu yeyote wa lugha yoyote ile duniani akiwa anaongea kwa ukali utajua kabisa anakukalipia ama anakatazia kitu kufuatana na lile utaliona mbele yako, lakini hautaelewa nini anaongea.

Hivyo anayetoa tafasiri ya ndoto atasema unakataziwa ama kuonywa kama jambo ni baya ama atasema unaambiwa fanya haraka kama jambo ni zuri ila hataongea nini maana sahihi ya kile kimeongelewa,, sijui mnanielewa hapo?

Mfano wapili: katika ndoto kuna zile ndoto za ta wanyama wadudu nk ka ulimwengu wa kiroho kila mnyama ama mdudu anakuwa na maana yake ama anakuwa na kitu anachokiwakirisha. Mfano Nyoka mara nyingi huwakirisha mambo kama haya:

1. Mapenzi
2. Usaliti
3. Huruma
4. Upole
5.Subira
6.Usikivu nk

Hayo ni mambo vbaadhi tu ambayo watafasiri wengi wa ndoto huweza kuyachukua na kuyaweka katika uhalisia wa ndoto kitu ambacho ni tofauti na ni kinyume kabisa japo kinaweza kuwiana kwa asilimia ndogo sana.

Sasa leo unaweza ota unang'atwa na nyoka lakini mtoa tafasiri akakuambia kuna mchawi anakuwinda ama kuna jambo linakuja utafeli nk

Mwingine anaweza kukuambia jihadhari na mtu uliyenaye katika mahusiano maana anaweza akakusaliti ama kukufanyia jambo lolote jema

Pia unaweza ukaota labda labda nyoka wa kijani anapita mbele yako. Wanaotoa tafasiri kuna mmoja anaweza akakuambia kwamba kuna jambo unataka kulifanya unapaswa kuwa makini au vuta subira kwanza usianze kulifanya nk

Najaribu kutoa kidogo ufafanuzi juu ya misingi ya wanaotoa tafasiri ya ndoto, kwa njia na namna ambayo nitofauti kabisa.

Pia unaweza kutana ana watu ambao wanakupa tafasiri ya ndoto mapema kabisa kabla haujaota ndoto anakuambia ukiota hivi ujue kuna hili nk

Sasa mambo kama hayo inakuwa ni uongo na upotoshaji kwa hali ya juu sana kuliko uhalisia.
Anawezaje kujua lugha yako na maana yake na kabla haujaongea?

NIliwahi kutana na mtoa tafasiri mmoja maarufu sana nikamwambia bibi yangu(Alikwisha fariki mwaka 2008)anaota sana gari(Ambulance) linagonga nyumba, inamtokea mara mbili hata tatu kwa mwaka,
je maana yake nini?
Alichoniambia nilitamani kucheka japo nilikuwa najifunza ikabidi niwe mpole tu,
Lakini yeye bibi aliweza kujua maana ama tafasiri ya ndoto hiyo, Yeye kila akiota gari ya wagonjwa imegonga nyumba basi katika nyumba husika au ndugu wa nyumba husika kunakuwa na msiba ndani ya siku tatu zijazo, aliweza kujua maana ya ndoto hii sababu ya ile kujirudia mara kwa mara.

Lakini pia ukiachilia mbali huyu Bibi yangu jaribu kuangaia katika vitabu vya dini watu walioweza kuota ndoto zilizoandikwa na wakawepo wale wakufasiri ndoto husika,
Unakuta ni ndoto na maana ni vitu viwili tofauti kabisa yaani unapopata maana ndio unaona vinaendana ila pasipo maana hauiwezi kufikiria kabisa kama itakuwa ni hiii ndio maana yake.
Angalia mfano wa ile .......ndoto nyota na mwezi na jua vinanisujudia...... kuna ile ya sanamu pia kuna ile ya miaka saba ya njaa na miaka saba ya shibe.

Ukiangalia hizo ndoto na maana zake nikwamba utaona kuna wimbi kubwa sana lakudanganywa juu ya maana na tafasiri za ndoto kuliko kile ulipaswa kukijua katika uhalisia.

Kwamiaka ya sasa unaambiwa ng'ombe ni ishara ya pepo au roho chafu katika ulimwengu wa ndoto, lakini je ng'ombe anaashiria nini ulimwengu wa roho? yule aliota ng'ombe wanavuka mto mbona hatujaona tafasiri kama ni roho chafu au mapepo?

Sijui tunaelewana hapo kidogo?Usisite kuuliza
Kwahiyo najaribu kwanza kukupa uelewa uone kwamba uwiano wa ndoto na maana haswa tunazotolewa na watu wengi wasio sahihi haswa hawa wanajiita manabii,wachungajii,masheik,waganga wanajimu nk huwa wanapotosha maana.

Sasa utawezaje kujua maana sahihi ya ndoto? Pasipo kudanganywa na kupotoshwa?
Jambo La kwanza na msingi lakujua nikuwa wewe pekee ndie wakwanza unaijua na kuielewa lugha yako, Hakuna mwingine anayejua nini ulichosikia au nini unataka kuongea niwewe wakwanza binafsi unayejua ukweli na uhalisia.

Jambo la pili na la msingi niwewe kuziandika ndoto zako, weka kumbukumbu yakile unachokuwa unakiota andika kumbukumbu zako kwa kile unakuwa unakiota kila siku. Hii itakusaidia kujua na kukumbuka na kuielewa lugha yako ya ndoto

Jambo la tatu hakikisha unajifunza maana yake kiroho yakile unachokuwa umekiona katika ndoto(Main character) mfano umeota nyoka anakukimbiza basi mjue nyoka maana yake kiroho, umeota mbuzi kaingia ndani basi mjue mbuzi maana yake kiroho, umeota nyasi zinaungua basi jua maana ya moto au nyasi kiroho nini humaanisha, (Ukiingia google utapata maana ya viumbe na vitu vingi maana yake kiroho)

Hatua Ya NNE
hapa sasa utaenda kujua maana ya ndoto yako
Ukishamaliza hatua ya tatu unarudi katika uhalisia wa maisha yako kutokana na maana ya mhusika mkuu katika ndoto yako angalia sasa anahusianaje katika maisha yako kwa kuangalia maana husika,
Kaa tulia tafakari polepole ndipo unaichukua na ndoto yako katika maisha yako ya kawaida inaweza kukaa kwa namna gani?

Hiii njia ndio husaidia watu wengi sana kujua m,aana halisi na zikawa kweli katika maisha yao ya kila siku kuliko zile za wale wanaojiita mafundi. Nikweli wapo watu wenye karama zao, lakini huwezi kuwakuta google ama katika mitandao ni kwa nadra sana zaidi zaidi huko utawakuta wanaojua kuhesabu nyota tu.

Ukiwa na swali usisite kuuliza pia kumbuka kujua maana ya ndoto sio lazima uijue kwa siku moja zingine unaweza jua baada ya miaka ama siku kadhaa maana vingine unaandaliwa mambo ya mbele vingine ni mambo yaliyopita ndio maana ni muhimu kuweza kuandika ndoto ili uwe na kumbukumbu sahihi.................



Over
 
Mleta uzi hebu fafanua vizuri, hizi ndo sifa za kiroho za nyoka kweli!!?
-Huruma
-Upole
-Usikivu.
 
Mleta uzi hebu fafanua vizuri, hizi ndo sifa za kiroho za nyoka kweli!!?
-Huruma
-Upole
-Usikivu.
Nyoka anahuruma sana kwa zaidi ya asilimia kubwa ya jamii za nyoka hawawezi kukudhuru hadi umewadhuru hiyo hupelekea kuwa na sifa ya upole hata kiroho pia utakuta wakiwa na sifa hiyo jaribu kupitia maandiko zaidi utaona ufafanuzi wake zaidi

Pia nyoka ni mpole mno mara nyingi huamua kukimbia ili aweze kuepuka kukudhuru japo anaweza akawa na uwezo mkubwa wa kukudhuru pia jamii chache sana za nyoka ambao ndio hatrari zaidi kwa mwanadamu ndio maana nanakuwa na nasifa ya upole nk

Usikivu nyoka anakuwa nao sana kwasababu unaweza fanya naye mawasiliano ukiwa na elimu ya nyoka na akakutii kwa kama utamuamuru aondoke au hauwezi kumdhuru wew esio aduni nk
Hivyo nyoka ndio hupata sifa ya kuwa msikivu kwa phisical na kiroho pia
 
Huota niko na class mate wangu na tunafanya mtihani,lakini mimi huwa nakuwa na kikwazo fulani ,ama kuchelewa ,ama kalamu kutoandika ama dharura fulani hivi wakati wa mtihani.
Ilhali nilikuwa mwanafunzi iaka mingi iliyopita,tangu miaka ya 94.Sijaenda tena school bali naendelea na maisha ya kawida .
sasa. Ndoto gani hii,ambayo huja mara kwa mara?
 
Huota niko na class mate wangu na tunafanya mtihani,lakini mimi huwa nakuwa na kikwazo fulani ,ama kuchelewa ,ama kalamu kutoandika ama dharura fulani hivi wakati wa mtihani.
Ilhali nilikuwa mwanafunzi iaka mingi iliyopita,tangu miaka ya 94.Sijaenda tena school bali naendelea na maisha ya kawida .
sasa. Ndoto gani hii,ambayo huja mara kwa mara?
Kuna mtu anakufunga usiendelee kimaisha ubakie hapohapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutafsiri ndoto ni kitu kizito! Hiki ni kipaji ambacho Mungu anakupa moja kwa moja na kama mtu akikisomea ataelewa kwa kiasi tu. Naungana na wewe kuna watu wanatafsiri ndoto kirahisi rahisi tu.

Kuna jamaa mmoja mashariki ya kati miaka ya nyuma kutokana na vita mama yake akatekwa na kwa bahati mbaya hakuwahi kuiona hata picha ya mama yake kwani kipindi hicho alikuwa ni mdogo kimakamo. Alipishana na mama yake kwa umri wa miaka 15. Baadaye akahama mji na kwenda nchi nyengine hapo hapo mashariki ya kati. Akakutana na mwanamke wakapendana lakini yule mwanamke alikuwa ni mkubwa kuliko yeye lakini hakuwa ni miongoni mwa wanawake wenye kuzeeka mapema. Wakapanga kufunga ndoa na huyo mwanamke.

Kabla ya kumtambulisha kwa ndugu zake ili afunge naye ndoa moja miongoni mwa siku aliota anaunyofoa mzaituni pamoja na mizizi yake. Hakuelewa ndoto hiyo ina maana gani! Akaenda kwa mfasiri wa ndoto na kumsimulia alichokiota, mtafsiri wa ndoto akashtuka! Akamuuliza umeshoa? Yule kijana akajibu hapana! Mtafsiri wa ndoto akamjibu kwa kumwambia usioe unayetaka kumuoa kwani huyo ni mama yako mzazi!

Huwa najiuliza kuota kunyofoa mti wa mzaituni pamoja na mizizi yake kuna uhusiano gani na kuoa na kuambiwa huyo ni mzazi wake halisi?

Halafu kingine ndoto moja waliyoota watu wawili ina uwezo kabisa wa kutoa majibu mawili tofauti. Au ukiota kondoo ni bishara njema.Ajabu ukitizama JF watu wanatafsiri ndoto kiajabu ajabu mpaka unashangaa!
 
Huota niko na class mate wangu na tunafanya mtihani,lakini mimi huwa nakuwa na kikwazo fulani ,ama kuchelewa ,ama kalamu kutoandika ama dharura fulani hivi wakati wa mtihani.
Ilhali nilikuwa mwanafunzi iaka mingi iliyopita,tangu miaka ya 94.Sijaenda tena school bali naendelea na maisha ya kawida .
sasa. Ndoto gani hii,ambayo huja mara kwa mara?
Nyumba tuliyokuwa tunaishi miaka ya nyuma tulihama mwaka 2007. Ajabu kila ninapoota ndoto ya ajabu, aidha, nakutana na wafu au hali yoyote ya kuogofya huwa naota nikiwemo ndani ya hiyo nyumba. Kuna siku marehemu baba yangu akaita Sheikh kuja kuomba dua kwenye nyumba yetu 2009 tuliyohamia na kuombewa dua nyumba nzima.

Nikamsimulia huyo Sheikh kuhusu ndoto za namna hiyo! Sheikh akanijibu kwa kusema "pengine mlipokuwa mnaishi kwenye hiyo nyumba kulikuwa na mazingira ya ziada, jikurubishe zaidi kwa Mungu kwani yeye ni mwenye kusikia na mwenye kuona"

Kuhusu ndoto yako sijui ndoto yako ina maana gani, ninachokusihi muombe Mungu akulinde kama unaamini Mungu yupo! ikiwa ni heri akupatie na kama ikiwa shari akuepushie. Nakusudia wewe niliye reply koti yako!
 
Kutafsiri ndoto ni kitu kizito! Hiki ni kipaji ambacho Mungu anakupa moja kwa moja na kama mtu akikisomea ataelewa kwa kiasi tu. Naungana na wewe kuna watu wanatafsiri ndoto kirahisi rahisi tu.

Kuna jamaa mmoja mashariki ya kati miaka ya nyuma kutokana na vita mama yake akatekwa na kwa bahati mbaya hakuwahi kuiona hata picha ya mama yake kwani kipindi hicho alikuwa ni mdogo kimakamo. Alipishana na mama yake kwa umri wa miaka 15. Baadaye akahama mji na kwenda nchi nyengine hapo hapo mashariki ya kati. Akakutana na mwanamke wakapendana lakini yule mwanamke alikuwa ni mkubwa kuliko yeye lakini hakuwa ni miongoni mwa wanawake wenye kuzeeka mapema. Wakapanga kufunga ndoa na huyo mwanamke.

Kabla ya kumtambulisha kwa ndugu zake ili afunge naye ndoa moja miongoni mwa siku aliota anaunyofoa mzaituni pamoja na mizizi yake. Hakuelewa ndoto hiyo ina maana gani! Akaenda kwa mfasiri wa ndoto na kumsimulia alichokiota, mtafsiri wa ndoto akashtuka! Akamuuliza umeshoa? Yule kijana akajibu hapana! Mtafsiri wa ndoto akamjibu kwa kumwambia usioe unayetaka kumuoa kwani huyo ni mama yako mzazi!

Huwa najiuliza kuota kunyofoa mti wa mzaituni pamoja na mizizi yake kuna uhusiano gani na kuoa na kuambiwa huyo ni mzazi wake halisi?

Halafu kingine ndoto moja waliyoota watu wawili ina uwezo kabisa wa kutoa majibu mawili tofauti. Au ukiota kondoo ni bishara njema.Ajabu ukitizama JF watu wanatafsiri ndoto kiajabu ajabu mpaka unashangaa!
Kabisa mkuu nakubariana nawewew nikamara na kipaji cha pekee mno haya mambo maana ukiangalia na kufuatilia ndoto zote za ukweli maana yake inapotolewa huwa haiwi kama vile unavyofikiria
ila hawa wa uchwara unajikuta hata unawa naye pamoja kitu kimoja,
kwa uhalisia ndoto ni kitu cha kipekee na ziada mnooo wala haiwezi kuwa jambo la bla bla kama tunavyofikiria, uwezo wakutambua lugha za kiroho haswa kama hizi za ndoto ni kitu cha pekee mno wala hakipo kwa kila mtu
 
alianza vizuri ila hapo kwenye nyoka amenivuruga kabisa,tangu lini nyoka akawa mpole na nwenye huruma

Sent using Jamii Forums mobile app
Ha ha ha ha sio kukuvuruga ni ukweli kabisa sema nyoka unaweza kumjua kwa upande mmoja tu kama ni kiumbe hatari kwa mwanadamu.

Lakini ukiingia kujifunza katka namna nyigine utaweza kuelewa ukweli na uhalisia wake mwingine
 
Huota niko na class mate wangu na tunafanya mtihani,lakini mimi huwa nakuwa na kikwazo fulani ,ama kuchelewa ,ama kalamu kutoandika ama dharura fulani hivi wakati wa mtihani.
Ilhali nilikuwa mwanafunzi iaka mingi iliyopita,tangu miaka ya 94.Sijaenda tena school bali naendelea na maisha ya kawida .
sasa. Ndoto gani hii,ambayo huja mara kwa mara?
mkuu hiyo ndoto yako hata mimi huwa naota mara kwa mara.
hata juzi ililala nikaota niko shuleni na wanafunzi niliosoma nao shule ya msingi miaka mingi nyuma.
Niliwah kuwauliza wataalamu mbalimbali kuhusu tafsiri ya hii ndoto wakaniambia inamaanisha matatizo bado yataendelea,au mambo yako yatarudi nyuma badala ya kwenda mbele.
Na nikicheki ni kweli mambo yangu huwa yanakwenda mbele kidogo na kurudi nyuma miaka yote.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana kwa kunifungua macho nitakuwa naziandika ndoto zangu ili nisizisahau
Nalog off
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom