Kuwa makini, huruma zikizidi zitakuponza

mpasta

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
917
1,997
Kuna siku nilikuwa nasafiri na ndege ya Alfajiri pamoja na Bosi wangu, sasa pale Airport ghafla tupo foleni kajitokeza jamaa ana kifurushi chake anasema ni magazeti anataka nimsaidie kumbebea mpaka MWANZA kuna mtu atapokea. Nataka kukipokea Bosi akaniambia "Kuwa makini huruma zikizidi zitakuponza". Ikabidi nikatae, baadae akaniambia "binadamu sasa sio wazuri unaweza kubebeshwa mihadarati bure kidagaa kikakuozea". Basi toka siku hiyo nipo makini kweli kweli na huruma za kipumbavu sitaki kabisa.

Sasa leo Stendi ya Mbezi, tupo kwenye foleni ya MWENDOKASI Tunakata tiketi, nimeshuhudia kaja mkaka mmoja amevaa kizibao kama waendesha bodaboda, Kamuomba dada wa mbele yangu kwenye foleni achukue elfu 10 yake akatie tiketi ili apate chenji. Dada ikabidi aweke pembeni elfu 1 yake mkononi akachukua elfu 10 ya jamaa yule.

Wakaka wa kule kibanda cha tiketi walipopokea pesa wakaiangalia wakamwambia hatuna chenji. Ikabidi dada arudishe elfu 10 kwa yule bodaboda akatoa elfu 1 yake. Wale wakaka wakamwambia yule dada ile Pesa uliyotoa mwanzoni ni pesa bandia,tumekuonea huruma tu vinginevyo sasa hivi tungekutia mbaroni.

Dada wa watu akatahayari macho yamemtoka kwa hofu. Nikakumbuka msemo wa BOSI wangu "Huruma zikizidi zitakuponza"
 
Kweli mkuu. Huruma imeponza wengi na imewagharimu wengi kufungwa au kupewa kesi ngumu na nzito.

Kunamazingira unaweza kuwa makini sana lkn kuna mazingira huyakwepeki mkuu.

Zaidi ni kumuomba Mungu kwa yaletunayo yajua na yale tusioyajua.
 
"samahani kaka nishikie mtoto nikachimbe dawa hapo basi limesimama "

Watu wanaingia sister humuoni dereva anapiga honi watu waingie safari ianze baada ya kusubiri sana dereva anaanza kuondoa gari akiamini watu wameingia wote unaamka sitini kwako unaenda unamfuata konda kumwambia bado kuna mtu yupo nje

🤣🤣🤣🤣
 
Huo sio huruma ni ustarabu tu. Huruma ni ile unamsomesha demu na kumwezesha ili awe na uwezo kama wengine, ila anakuja kukugeuka nakukuona koma lofa au Fala.
Mkuu yamekukuta nini maana umeandika kwa hisia sana
 
Watu wengi huingia matatani sababu hii. Wahalifu na maantisocial hawaoni taabu kuwaingiza wenzao matatani. Mmoja kwenye treni enzi hizo akambiwa naomba unishushie mzigo nitapokelea dirishani. Jamaa alipofika nje huyu mwema wa ndani akaanza kumshushia. Ghafla anashangaa mtu anamwambia mbona unashusha mzigo wangu. Akasema huyu jamaa huku nje kasema nimshushie. Jamaa wa nje anasema hapana, mi sijamwambia. Basi wakazozana wakayamaliza. Jamaa safari nzima ilikuwa chungu maana kidogo tu watu wanasema, "Kuweni makini, humu ndani kuna wezi."
 
Kuna siku nilikuwa nasafiri na ndege ya Alfajiri pamoja na Bosi wangu, sasa pale Airport ghafla tupo foleni kajitokeza jamaa ana kifurushi chake anasema ni magazeti anataka nimsaidie kumbebea mpaka MWANZA kuna mtu atapokea. Nataka kukipokea Bosi akaniambia "Kuwa makini huruma zikizidi zitakuponza". Ikabidi nikatae, baadae akaniambia "binadamu sasa sio wazuri unaweza kubebeshwa mihadarati bure kidagaa kikakuozea". Basi toka siku hiyo nipo makini kweli kweli na huruma za kipumbavu sitaki kabisa.

Sasa leo Stendi ya Mbezi, tupo kwenye foleni ya MWENDOKASI Tunakata tiketi, nimeshuhudia kaja mkaka mmoja amevaa kizibao kama waendesha bodaboda, Kamuomba dada wa mbele yangu kwenye foleni achukue elfu 10 yake akatie tiketi ili apate chenji. Dada ikabidi aweke pembeni elfu 1 yake mkononi akachukua elfu 10 ya jamaa yule.

Wakaka wa kule kibanda cha tiketi walipopokea pesa wakaiangalia wakamwambia hatuna chenji. Ikabidi dada arudishe elfu 10 kwa yule bodaboda akatoa elfu 1 yake. Wale wakaka wakamwambia yule dada ile Pesa uliyotoa mwanzoni ni pesa bandia,tumekuonea huruma tu vinginevyo sasa hivi tungekutia mbaroni.

Dada wa watu akatahayari macho yamemtoka kwa hofu. Nikakumbuka msemo wa BOSI wangu "Huruma zikizidi zitakuponza"
Ninachofanya ni kujitenga sana kuepukana na watu omba omba. Ndo maana sipendi kutumia public transport au kuonekana maeneo ya uswazi kwenye mirundiko ya watu, hio inapunguza chances ya kukutana na watu kama hawa.

Kipindi ndio nimekuja dsm niliwahi kaa uswazi chumba kimoja kule mbagala aisee watu wanaombana hadi mifagio, sasa hii ombana ombana na toa toa ndo inaingiza watu wengi hatarini bila kujua
 
Watu wengi huingia matatani sababu hii. Wahalifu na maantisocial hawaoni taabu kuwaingiza wenzao matatani. Mmoja kwenye treni enzi hizo akambiwa naomba unishushie mzigo nitapokelea dirishani. Jamaa alipofika nje huyu mwema wa ndani akaanza kumshushia. Ghafla anashangaa mtu anamwambia mbona unashusha mzigo wangu. Akasema huyu jamaa huku nje kasema nimshushie. Jamaa wa nje anasema hapana, mi sijamwambia. Basi wakazozana wakayamaliza. Jamaa safari nzima ilikuwa chungu maana kidogo tu watu wanasema, "Kuweni makini, humu ndani kuna wezi."
Hahahahahaha imefanya niwaze saaana... safari ya kigoma Dar na ndo kwaaanza labda mpo uvinza huko ndo yanakukuta hayaaa....utaomba ardhi ipasuke
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom