Kuvunja soko la Kariakoo ni upumbavu kabisa...

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,108
115,842
Nimeshangazwa sana na habari hiii.

Nnimesoma kwenye gazeti la tafakari kuwa soko la Kariakoo limepata mchina anaetaka kulivunja na kujenga jengo lingine hapo hapo la ghorofa 15..........

Nafahamu hii nchi tumeishiwa viongozi wenye akili but this is too much..........

Hivi kuna jengo maarufu Tanzania zaidi ya soko la Kariakoo? Hivi sisi hatuna policy ya ku protect historical sites na historical buildings? Hakuna sheria ya kuzuia upuuzi kama huu? Hivi hawa watu wanamjua hata bj amuli?

Aliye design soko la Kariakoo na Nyerere Airport na jengo la Ushirika (CRDB Lumumba)? Hivi wanajua hata historia ya majengo hayo? Na hivi huo msongamano wa katikati ya jiji watau address vipi wakiongeza ukubwa wa soko? Mara kumi na tano?

Kama kuna mwana JF ambaye ana contacts zenye nguvu anaeweza ku put stop on this non sense naomba please afanye hivyo......

Hivi unaweza vunja 'Empire State Building' kwa sababu ya kujenga jengo lingine refu zaidi? Au unaweza vunja 'The Eifel Tower' kwa sababu unataka jenga mnara mwingine mkubwa zaidi?

Hivi sisi hatujui how history is priceless? Hivi hatuna kabisa viongozi wenye kutumia common sense hapa Tanzania?
 
ina maana wamekosa sehemu zingine za kujenga soko? waende huko tandika kama vipi!
 
Wapumbavu hawa.
Kuna boko,mbagala tegeta kimara ote huko kuna shida ya masoko.
 
hii ndo bongo, hakuna viongozi kabisa.hatujakuja endelea chini ya mafisadi ccm
 
jamni kama wantaka kujenga jengo la kisasa wasifanye hivyo?hebu waacheni wajenge jengo la kisasa zaidi.jamani acheni kuwa conservative
 
masoko makubwa ya katikati ya majiji yapaswa kuwa ardhini na juu kunafanyika shughuli nyingine tofauti na barabara zinapita na majumba yanajengwa............. hii itasababisha wafanyabiashara wengi wa kutoonekana juu ya ardhi hasa wamachinga n.k. ....................nafikiri hao wachina wakifanikiwa kutujengea jengo moja la aina hiyo hapo kariakoo ndio mtajua kuwa dar hakuna watu! kwa maana litameza, machinga complex zote, wahindi wote, mchikichini yote, manzese yote..............nk.

amini usiamini kuna majiji hapa duniani unaweza kutembea umbali mrefu sana na ukiambiwa kuwa chini eneo lote hilo kuna maghorofa ya kwenda chini hadi gorofa sita ama zaidi na kuna maduka matupu makubwa kwa madogo, kuanzia ya jumla mpaka madogo, mama ntilie mpaka watembeza pweza, washona viatu mpaka kumbi za snema..............


yaani karibu theluthi moja ya wakazi wa jiji watakuwa wanafanya shughuli zao chini ya ardhi............ na wakimaliza shughuli zao wanakutana na sub-way/metro, inawachukua chini kwa chini hadi huko kimara, sijui gongo la mboto nk na kuacha daladala juu ya ardhi zikiwa nyeupe 24/7 .............. na hii ingepunguza sana msongamano juu ya ardhi............. kama ni mawazo kama hayo, mi naunga mkono ujenzi huo mia kwa mia..............
 
Nimeshangazwa sana na habari hiii.

Nnimesoma kwenye gazeti la tafakari kuwa soko la Kariakoo limepata mchina anaetaka kulivunja na kujenga jengo lingine hapo hapo la ghorofa 15..........

Nafahamu hii nchi tumeishiwa viongozi wenye akili but this is too much..........

Hivi kuna jengo maarufu Tanzania zaidi ya soko la Kariakoo? Hivi sisi hatuna policy ya ku protect historical sites na historical buildings? Hakuna sheria ya kuzuia upuuzi kama huu? Hivi hawa watu wanamjua hata bj amuli?

Aliye design soko la Kariakoo na Nyerere Airport na jengo la Ushirika (CRDB Lumumba)? Hivi wanajua hata historia ya majengo hayo? Na hivi huo msongamano wa katikati ya jiji watau address vipi wakiongeza ukubwa wa soko? Mara kumi na tano?

Kama kuna mwana JF ambaye ana contacts zenye nguvu anaeweza ku put stop on this non sense naomba please afanye hivyo......

Hivi unaweza vunja 'Empire State Building' kwa sababu ya kujenga jengo lingine refu zaidi? Au unaweza vunja 'The Eifel Tower' kwa sababu unataka jenga mnara mwingine mkubwa zaidi?

Hivi sisi hatujui how history is priceless? Hivi hatuna kabisa viongozi wenye kutumia common sense hapa Tanzania?

Kama soko linalojengwa ni kuongeza idadi kubwa ya wafanyabiashara (ajira) na pia kuwa jengo bora lenye miundombinu muhimu basi bora Wachina wafanye hivyo. Ukitembelea hiyo sehemu, kweli utaona umuhimu wa kujenga soko la kisasa lenye barabara bora za kuingizia biadhaa na watu.

Tatizo ni je tunauwezo wa kusimamia hicho kitu kweli WACHINA wakakijenga? Mchina ni mchuuzi vile vile, usipombana toka mwanzo anaweza akabomoa na akajenga ghorofa moja tu na usijue uwafanye nini maana mikataba ulishasaini. Ukiwauliza watakwambia watajenga tokana na mapato ya soko.

Naamini mfanyabiashara yeyote toka China akiwa na mkataba wa kujenga upya Kariakoo, basi serikali yake itampa mkopo kiurahisi tu, lakini si lazima kua hizo pesa kweli atazitumia ktk huo mradi.
 
Nimeshangazwa sana na habari hiii.

Nnimesoma kwenye gazeti la tafakari kuwa soko la Kariakoo limepata mchina anaetaka kulivunja na kujenga jengo lingine hapo hapo la ghorofa 15..........

Nafahamu hii nchi tumeishiwa viongozi wenye akili but this is too much..........

Hivi kuna jengo maarufu Tanzania zaidi ya soko la Kariakoo? Hivi sisi hatuna policy ya ku protect historical sites na historical buildings? Hakuna sheria ya kuzuia upuuzi kama huu? Hivi hawa watu wanamjua hata bj amuli?

Aliye design soko la Kariakoo na Nyerere Airport na jengo la Ushirika (CRDB Lumumba)? Hivi wanajua hata historia ya majengo hayo? Na hivi huo msongamano wa katikati ya jiji watau address vipi wakiongeza ukubwa wa soko? Mara kumi na tano?

Kama kuna mwana JF ambaye ana contacts zenye nguvu anaeweza ku put stop on this non sense naomba please afanye hivyo......

Hivi unaweza vunja 'Empire State Building' kwa sababu ya kujenga jengo lingine refu zaidi? Au unaweza vunja 'The Eifel Tower' kwa sababu unataka jenga mnara mwingine mkubwa zaidi?

Hivi sisi hatujui how history is priceless? Hivi hatuna kabisa viongozi wenye kutumia common sense hapa Tanzania?

Tumewachagua sisi wenyewe, na tutawarudisha sisi wenyewe madarakani.
 
masoko makubwa ya katikati ya majiji yapaswa kuwa ardhini na juu kunafanyika shughuli nyingine tofauti na barabara zinapita na majumba yanajengwa............. hii itasababisha wafanyabiashara wengi wa kutoonekana juu ya ardhi hasa wamachinga n.k. ....................nafikiri hao wachina wakifanikiwa kutujengea jengo moja la aina hiyo hapo kariakoo ndio mtajua kuwa dar hakuna watu! kwa maana litameza, machinga complex zote, wahindi wote, mchikichini yote, manzese yote..............nk.

amini usiamini kuna majiji hapa duniani unaweza kutembea umbali mrefu sana na ukiambiwa kuwa chini eneo lote hilo kuna maghorofa ya kwenda chini hadi gorofa sita ama zaidi na kuna maduka matupu makubwa kwa madogo, kuanzia ya jumla mpaka madogo, mama ntilie mpaka watembeza pweza, washona viatu mpaka kumbi za snema..............


yaani karibu theluthi moja ya wakazi wa jiji watakuwa wanafanya shughuli zao chini ya ardhi............ na wakimaliza shughuli zao wanakutana na sub-way/metro, inawachukua chini kwa chini hadi huko kimara, sijui gongo la mboto nk na kuacha daladala juu ya ardhi zikiwa nyeupe 24/7 .............. na hii ingepunguza sana msongamano juu ya ardhi............. kama ni mawazo kama hayo, mi naunga mkono ujenzi huo mia kwa mia..............
Akili kichwani unachokisema ni sawa lakini kwa nini tuvunje kariakoo? kwa nini lisijengwe jengo jingine mbadala wa kariakoo? mbona katika nchi nyingine duniani miji yote ya kale imeachwa na kujengwa miji mipya kabisa. Kwa mtindo huu hakuna historia itakayohifadhiwa dar hasa kama tukianza kuvunja hadi majengo ya serikali. The idea is good but not for demolition of the current kariakoo structure
 
Wapumbavu hawa.
Kuna boko,mbagala tegeta kimara ote huko kuna shida ya masoko.
Wapumbavu haswa? huu msongamano unaoongezeka kila siku katikati ya jiji hawauoni kabisa. Labda kwa kuwa wenyewe wanapita na ving'ora.
 
Hii ndio brand ya leaders tulio nao leo. Hawa ndio viongozi wetu.
Hivi kwani kujenga lazima uvunje cha zamani?
Ninaijua Dar ina maeneo mengi ya kujenga kwa nini wavunje soko la kariakoo?
 
Ni jambo la kushangaza kwa sababu wengi wanaotumia soko la kariakoo sio wakazi wa kariakoo...kwa hiyo ni wazi kama watumiaji wanao ishi maeneo yaliyo mbali na kariakoo wakijengewa masoko huko waliko hawatakuwa na uhitaji wa kufunga safari kuja kujazana hapo kariakoo. Na hivyo tutakuwa tumetatua tatizo la msongamano na pia kulinda heshima ya majengo yetu ya ukumbusho.

Lakini swali linabaki,huyo alietoa 'mawazo mtindi' kama hayo ya kubomoa soko la kariakoo halifahamu hili wazo la kuwasogezea huduma wana nchi huko waliko ili kupunguza msongamano hapo sokoni kariakoo????

Au ndo ile wanatengeneza naman nyingine ya ulaji....tunakumbuka ni juzi juzi tu tuliambiwa bora tufe njaa lakini lazima ndege ya raisi na rada zinunuliwe, matokeo yake tumeyaona watu walipiga mamilioni ya hela wakatia mfukoni....nhi yetu bwana,kama kajishamba ka bibi!!
 
DUH ...ama kweli tumekosa ma"thinkers".....Hizi kelele wadau zinawafikia?
 
Haya ni matokeo ya kuwa na viongozi wenye Tamaa, Waongo, wasiowajali Wananchi waliowachagua, na pia....wenye akili za Ki-Taahira. Soko la Kariakoo ni "Historical site"....na pia ni "Land-mark" kwa watu wengi....Hao waChina labda wafanye "renovations" katika soko...lakini sio kulivunja.

Ndio nakubali panahitajika juhudi kubwa za Usafi pale sokoni Kariakoo....lakini sio kulivunja.
 
Hakuna haja ya kuvunja Kariakoo...

Tunachotakiwa kufanya ni kujenga Masoko 6 kama Kariakoo kila Wilaya ya Dar es salaam. Kila Wilaya iwe na Masoko 2....
 
Back
Top Bottom