Kuvuja mitihani ya Form four kila mwaka NECTA na waziri wa elimu wajiuzulu!

Mzee Mkijiji ni kama umejichanganya... umesema wakuwajibika ni walimu na wakuu wa shule... hapo hapo unasema tusimhukumu mtu kabla ya uchunguzi kufanyika. Sasa kumwajibisha mtu (mwalimu au mkuu wa shule) si ni kumhukumu?
 
Mkkj kumbe ndo ulivyo!kumbe mkurungezi wa NSSF awajibike why wakati kuna kina;;;;;;;;;;!Pia why tusisubiri uchunguzi kabla ya kumuhukumu Bwana mkubwa wa NSSF?

Waziri wa elimu awajibike kwa mpango gani? Kwani huyo waziri wa elimu ni MUISLAM mpaka hawajibike? Angekuwa ni Muislam ingekuwa sawa swa kwake kuwajibika. Bahati mbaya si muislam... Ndo maana husikii shangwe na vifijo za kumtaka awajibike.... lol

Habari ndo hiyo
 
Wajiuzulu then what?Hata wakijiuzulu hili suala la kuvuja paper halita settle down!Every year paper linavuja ila suala linakuja pale ambapo tunasema to what extent paper limevuja?
Wakijiuzulu watakuja wapuuzi wengine ambao watafanya paper li leak!
Masuala kama haya yanapaswa yashughulikiwe kwa watu kuadhibhiwa vikali sana ili iwe fundisho!
Kila leo viongozi wanajiuzulu and then hamna kitu hii imeshakuwa fasheni
 
Wajiuzulu then what?Hata wakijiuzulu hili suala la kuvuja paper halita settle down!Every year paper linavuja ila suala linakuja pale ambapo tunasema to what extent paper limevuja?
Wakijiuzulu watakuja wapuuzi wengine ambao watafanya paper li leak!
Masuala kama haya yanapaswa yashughulikiwe kwa watu kuadhibhiwa vikali sana ili iwe fundisho!
Kila leo viongozi wanajiuzulu and then hamna kitu hii imeshakuwa fasheni

Umesema kweli Kevo, kwa suala kama hili kujiuzulu tu haitoshi......inabidi watu wapelekwe mahakamani na kufungwa. Lakini suala jingine la kujiuliza hawa watu wa baraza la mitihani/wizara wanajua kweli tatizo liko wapi?...manake inawezekana ikawa 'year in year out' tatizo ni lile lile kwa sababu hawajui wapi penye tatizo. Hivi waziri au mkurugenzi wa NECTA wakiulizwa wanaweza kutuambia tatizo liko wapi .....na wanahitaji nini ili kuliondoa isije ikawa hawapewi nyenzo zote wanazohitaji kufanikisha kazi.
 
Umesema kweli Kevo, kwa suala kama hili kujiuzulu tu haitoshi......inabidi watu wapelekwe mahakamani na kufungwa. Lakini suala jingine la kujiuliza hawa watu wa baraza la mitihani/wizara wanajua kweli tatizo liko wapi?...manake inawezekana ikawa 'year in year out' tatizo ni lile lile kwa sababu hawajui wapi penye tatizo. Hivi waziri au mkurugenzi wa NECTA wakiulizwa wanaweza kutuambia tatizo liko wapi .....na wanahitaji nini ili kuliondoa isije ikawa hawapewi nyenzo zote wanazohitaji kufanikisha kazi.


Mkuu believe me wanapewa nyenzo zote wanazohitaji shida hapa ni tamaa and irresponsibility.
Dr Ndalichako yuko juu sana kwenye kutoa adhabu kwa watu wanaocheat kwenye mitihani kwa nini hao wanaohusika kulikisha paper huko barazani asifanye juu chini wanyang'anywe vyeti vyao na kuwa stripped off all their powers as well as being taken to court?
Maana this is a matter of national level!
 
Habari za mtihani kuvuja zimepatikanaje? Tatizo liko hapa: Kama wana 'usalama' wamekamata vipande vya mitihani street, then tatizo ni kubwa zaidi maana haijulikani mtihani umevujia wapi. Na huo mpya wana uhakika gani kama hautaibiwa??

Kila mwaka tatizo ni lile lile. Wahusika wizarani na NECTA kwenyewe wameishiwa mbinu mbadala za kudhibiti hili. Ninaamini kama wangekuwa makini, wangepunguza mianya ya wizi huu.

Hii ni biashara ndugu zangu, na aliyefanya deal hili ataendelea kufanya tu, wakati huu atakuwa makini zaidi na wala fununu za kuibiwa hazitafumuka.
 
Hao wahusika wakuu hawataki tu, kudhibiti hiyo hali. Serikali kama ikitaka jambo lake lifanyike litafanyika tu bila mizengwe wala kupoteza muda.

Hao watayarishaji wa mitihani wanajulikana, wanaoingiza Data kwenye Computer wanajulikana, wachapishaji wanajulikana, wanao hifadhi hiyo mitihani pia wanajulikana. Sasa tatizo liko wapi?
Mbona hatujawahi kusikia kuwa PESA mpya zinazo chapishwa zimepotea?

Siku Serikali itakapo amuwa kuwaadhibu wale wote wanao husika na UFISADI huu, tena kwa adhabu ya kupigiwa mfano, watakao fuwata watatia akili.

Angalieni mfano wa nchi ya China, mafisadi wanawafanya nini. Serikali ijifunze kutoka kwao.
 
Leo imeripotiwa kuwa mtihani wa Mathematics kwa Form IV umehairishwa kufanyika leo kwa sababu umevuja na utafanyika jumatatu ijayo. Hii ni habari mbaya kwa vijana waliojiandaa kufanya mtihani leo kutokana na uzembe wa wizara ya elimu na baraza la mitihani kushindwa kutimiza wajibu wao wa kulinda mitihani.

Hii sio poa na waziri wa elimu anawajibika kujiuzulu akifuatiwa na uongozi wa baraza ili kuruhusu uchunguzi zaidi kwa nini hawa jamaa bado wanatoa mitihani. Utaratibu wa huu wa mithani una walostisha sana vijana ambao wasingeweza kupata hata huo mtihani fake wenyewe.

Inawezekana pia ushindani wa shule uliopo sasa unaweza kuwa ndio kichocheo zaidi kila mtu anataka mtoto wake au shule yake iwe ya kwanza hata kama haina uwezo ukizingatia wasimamizi wa mitihani wako corrupted lazima mtihani uvuje. Lakini hii sio sababu pekee manake na walimu pia wanahusika kuvujisha.

Miaka yote paper inavuja na business as usual sio poa.

"...........Endapo habari za kuvuja mitihani zitakuwa ndivyo zilivyo hapo juu watu wa kwanza kuwajibika itabidi wawe Waziri wa Elimu Prof. Jumanne Maghembe na Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Dr. Joyce Ndalichako............"
 
Hao wahusika wakuu hawataki tu, kudhibiti hiyo hali. Serikali kama ikitaka jambo lake lifanyike litafanyika tu bila mizengwe wala kupoteza muda.

Hao watayarishaji wa mitihani wanajulikana, wanaoingiza Data kwenye Computer wanajulikana, wachapishaji wanajulikana, wanao hifadhi hiyo mitihani pia wanajulikana. Sasa tatizo liko wapi?
Mbona hatujawahi kusikia kuwa PESA mpya zinazo chapishwa zimepotea?

Siku Serikali itakapo amuwa kuwaadhibu wale wote wanao husika na UFISADI huu, tena kwa adhabu ya kupigiwa mfano, watakao fuwata watatia akili.

Angalieni mfano wa nchi ya China, mafisadi wanawafanya nini. Serikali ijifunze kutoka kwao.
You nailed it buddy!
 
Ipo Haja ya kudefine rules za Viongozi kuwajibika!!!

Maana imekuwa jambo jepesi likitokea tatizo, somewhere, Wachangiaji Hujump X,Y, Z wajiuzulu...
1-Tatizo latakiwa kuwa la namna gani ili Kiongozi ajiuzulu?
2- Ktk RANK za Uongozi tulizonazo WHO and WHO wanatakiwa Kuwajibika?
3- Kuwajibika means kujiuzulu kwa wakuu? au Kuwajibika means waliopo ktk chain ya tatizo ndio wachukuliwe hatua za Kinidhamu?
4- Mfano Wizara ya Elimu ni kubwa MNO...maana imekusanya hadi Vyuo Vikuu...Hivi walim wa primary wakigoma...Waziri, Naibu,Katibu, Wakurugenzi..etc Wajiuzulu?
au Waalimu wa sekondari wakigoma?
au Waalim wa Vyuo wakigoma?
au wanafunzi wakifa ktk Bwawa la kuogelea la Chuo Kikuu?...
 
back ktk Kuvuja!!!

Kuvuja kwa mitihani si jambo tu la tanzania pekee, Hii haimaanishi natetea kuvuja ni jambo linaloisumbua DUNIA ya sasa...kuanzia kuvuja, fake certifications...na mfamo wake...ni ngumu lkn msingi ni kudhibiti UKUBWA wa tatizo!!!..ila wakianza kutolewa kafara wachache itakuwa discipline ya kuanzia...
Kuvuja kwa Mitihani sio siri, ni KERO kubwa hasa kwa wale waliojiandaa...
 
Chuma maelezo yako sawa lakini mwisho wa siku kiongozi wa juu ndio anabeba dhamana kama kazi nzuri anayepongezwa sio kiongozi wa chini na anayeomba budget ya taasisi zinazohusika na mitihani na elimu ni waziri.

Wizara ndio inayopewa pesa za walipa kodi wa nchi hii kama inashindwa kusimamia basi itawajibika. Kama baraza la mitihani linakula pesa za walipa kodi wa nchi hii wanapaswa pia kuwajibika. Waziri anatakiwa kuliona hili kabla na dhamana ya elimu ya nchi hii iko chini ya Wizara ya Elimu. Wamepewa pesa wakasimamie elimu na wameshindwa kusimamia elimu kwa gharama za walipa kodi.

lets "hug the neck" of the minister first others will follow the suit.
 
Jamani where are we going? Ni aibu kwa mitihani ya taifa kama darasa la saba, kidato cha nne, kidato cha sita na vyuo kuvuja kila kukicha. nimetafakari kwamba tatizo liko wapi sipati jibu. Hili tatizo limekuwa sugu kila mwaka.

Nimefuatilia habari za kuvuja kwa mitihani kwenye magazeti, kwenye blogu, kwenye jamii forums, TV, radio na vyombo vingine vya habari na kujiuliza mataifa ya nje nayo yanaaccess kwenye vyombo hivyo vya habari, je wataifiliria je Tanzania. Na tunaposafiri kwenda nje na mtu kujitambulisha kwa elimu yake si wanaweza wasiamini elimu mtu aliyonayo na kufikiri kwamba aliona mitihani iliyovuja kama huu wa hesabu?

Ni aibu kubwa iliyopo mbele yetu.
 
Huu uvujaji wa mitihani uliokithiri lazima wizara itafute namna ya kukomesha nayo ni kuwaadhibu Wale wote wanaosababisha hili litokee,kuwafutia wanafunzi mitihani siyo dawa ktk hili badala yake ni uonevu na kuwanyima haki kwa sababu hana uwezo sana wa kupigania haki yake.nionavyo mimi namna nzuri ya kukomesha hili ni kupata chanzo cha wapi ilikopatikana hii mitihani na kuwawajibisha Wahusika ambao pengine ni walimu ama wasimamizi ama watunga mitihani lakini tukiwa tumedhamiria kuwafahamu inawezekana kabisa kupitia haohao wanafunzi ambao ni watoto waliopotoshwa na watu wazima pengine kwa tamaa ya pesa pamoja na kukosa uadilifu wafutwe kazi pamoja na kushitakiwa ndiyo namna ya kukomesha hii tabia, ukiwafutia watoto mitihani na kuwaacha hawa watu ambao wameshafanya ya kuwa huu ni mradi mwakani wataendelea na mradi wao kama kawaida na kusababisha tena wengine kufutiwa mitihani lakini kwao kwa sababu wako salama zoezi litakuwa endelevu miaka yote...
 
Huu uvujaji wa mitihani uliokithiri lazima wizara itafute namna ya kukomesha nayo ni kuwaadhibu Wale wote wanaosababisha hili litokee,kuwafutia wanafunzi mitihani siyo dawa ktk hili badala yake ni uonevu na kuwanyima haki kwa sababu hana uwezo sana wa kupigania haki yake.nionavyo mimi namna nzuri ya kukomesha hili ni kupata chanzo cha wapi ilikopatikana hii mitihani na kuwawajibisha Wahusika ambao pengine ni walimu ama wasimamizi ama watunga mitihani lakini tukiwa tumedhamiria kuwafahamu inawezekana kabisa kupitia haohao wanafunzi ambao ni watoto waliopotoshwa na watu wazima pengine kwa tamaa ya pesa pamoja na kukosa uadilifu wafutwe kazi pamoja na kushitakiwa ndiyo namna ya kukomesha hii tabia, ukiwafutia watoto mitihani na kuwaacha hawa watu ambao wameshafanya ya kuwa huu ni mradi mwakani wataendelea na mradi wao kama kawaida na kusababisha tena wengine kufutiwa mitihani lakini kwao kwa sababu wako salama zoezi litakuwa endelevu miaka yote...
Watoto kuwafutia matokeo ni sawa na kuangalia tulipoangukia, badala ya tulipojikwa. Kwanini tusiannze na Waziri wa wizara husika,baraza la mitiani na ngazi zingine zinazofuatia mpaka kuja kumfikia mtoto ambaye ndio chanzo chetu cha kuwapata hao mafisadi wetu wa elimu.
 
Viongozi wote tupige kura ya kutokuwaruhusu watoto wao kusoma shule za binafsi
 
Viongozi wanaiba mitiani kwa sababu watoto wao wanasoma shule za binafsi kwa maana hiyo wao sio waathirika wa ubadhirifu huo ila ni watoto wa masikini.
 
Back
Top Bottom