Kuvaa saa enzi hizi za dijitali ni mbwembwe au usharobaro?

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,796
18,218
saa.jpg
Mimi nashindwa kuelewa kabisa watu (hasa wanaume) wanaovaa saa enzi hizi za dijitali kama wanafanya hivyo kwa makusudi au ni mbwembwe tu. Kwanini nasema hivyo? Siku hizi yapata 98% ya watanzania wote wanamiliki simu na kwenye simu kuna saa.

Utamkuta mwanamume sharobaro anamiliki simu 3 kwa mpigo na wakati huo huo katupia bonge ya saa kiganjani mwake. Kuvaa saa kwa wanawake inaleta maana kidogo kwa kuwa inachukua nafsi ya bangili &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; ni pambo la kike.

Sikumbuki mara ya mwisho kuvaa saa na sitegemei kuivaa tena labda nikiwa kwenye chumba cha mtihani nitaibeba na kwenda nayo na baada ya kumaliza kupiga paper nitampa demu wangu avae kama bangili. Uvaaji wa saa enzi hizi unawafaa zaidi wanafunzi wa shule za msingi kwa kuwa wengi wao hawamiliki simu. Tujifunze kuishi kulingana na wakati.

:israel:
======

Mada hii ni moja kati ya zilizojumuishwa kwenye kipindi cha Jamii Leo katika chaneli yetu ya YouTube. Kuona habari nyingine zaidi, tazama video hii hapa chini:
 
Kaka saa na simu ni vitu tofauti ,anayetumia saa kuangalia muda anaonekana muungwana kuliko yule anayetumia simu,kuna wakati unatakiwa ufunge simu ,je utajuaje muda,pia unasafiri charger imeisha,utafanyaje au ndio wale wa kusema samahani kaka/mzee eti saa hizi saa ngapi.Pia saa zina hadhi yake,ukivaa saa kama Tissot,Omega na brand nyinginezo hata ukienda kwenye interview kwa muonekano ukiwa umeulamba na huku umevaa saa ni rahisi kupata kazi,kwani wale walio kwenye panel watakuona ni mtu unayejali muda na ni mtu wa tahadhali.
 
Duh haya bhana!
Na hata unapokuwa unafanya "presentation" ofisini kwako au mahali popote ambapo ni "official" mbele za watu, toa simu yako/zako uangalie muda!


Watu wengine huchukulia mambo kiurahisi matokeo yake hukosa mambo muhimu,nimependa hapo kwenye red,sijui watakuwa wanamsubiri akitoa simu na kuanza kuiwasha ili aangalia kama muda aliopewa umefika.
 
Nashukuru mtoa mada amesema hakumbuki mara ya mwisho yeye alivaa saa lini, kwa lugha rahisi huo ni mtazamo wake mbadala kuhusu matumizi ya saa na ieleweke hivo, ahsante mfianchi maana nilichotaka miasma tayari umenitangulia, uungwana ni kitendo kwa muelewa ataelewa; hapa nina gear ya Samsung pia OMEGA flan ya hayari japo cyo mvaaji sana na nikitupia wanaojua maana wananipa respect, by the way ni kama aseti kwangu kama yaani kama waume wanaovaa mzigo wa madini shingoni & other; nawasilisha
 
Last edited by a moderator:
Utakuja kukosa hata kazi hvhv kwenye makampuni ya watu kwa kwa kujifanya unaenda na digitali.kwahiyo unataka kusema wanaume wote wanaovaa saa ni mademu au wazee wa analogue?
 
Simu ni kila kitu. stopwoch. rimainda. aram cloku nk tena hata kama umeizima inaweza kukuamsha. mnao sema pambo nawaunga mkono. mimi naona mzigo tu
 
Back
Top Bottom